Better than never is late
“Bora kuliko kamwe ni kuchelewa
-The Canterbury Tales, The Canon's Yeoman's Tale
Lilatini: potiusque sero quam numquam
Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa
- History of Rome, Book 4
It's never too late
Hakuna kuchelewa
Don't close the gate after the horse has bolted.
Usifunge mlango baada ya farasi kukimbia
जब जाति तब सवेरे
Wakati wowote unapoamka, ndo asubuhi yako
[M]tu hawezi kupata uzoefu wa mambo yote yahusuyo maisha kutoka kwa wazazi wake: lazima awe tayari kufunzwa na ulimwengu, yaani kujifunza kutoka kwa wengine zaidi ya baba na mama yake.
"na Ibrahim Nyanda 🏆 Shindano la Insha ya Methali
Creative Commons Attribution (CC BY 4.0) na Ibrahim Nyanda Ilichapishwa na Maktaba.org Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Mtaka cha mvunguni sharti ainame
Mulla [Nasreddin] alikuwa amepoteza pete yake sebuleni. Aliitafuta kwa muda, lakini kwa kuwa hakuipata, alitoka nje hadi uani na kuanza kuchungulia pale. Mkewe, ambaye aliona alichokifanya, akamwuliza: “Mulla, umepoteza pete yako sebuleni , kwa nini unaitafuta uani?” Mulla alishika ndevu zake akisema: “Chumbani kuna giza na sioni vizuri. Nilitoka nje kwenda uani ili kutafuta pete yangu kwa sababu kuna mwanga mwingi zaidi hapa.
[Afisa wa polisi alikutana na mwanamume akipapasa-papasa akipiga magoti] “Nilipoteza noti ya $2 kwenye barabara ya Atlantic,” kasema mwanamume huyo. "Nini kile?" aliuliza afisa aliyeshangaa. "Umepoteza notiya $2 kwenye barabara ya Atlantic? Kwa nini basi unaitafuta hapa Copley Square?" “Kwa sababu,” akasema akiendelea na utafutaji wake, “mwanga ni bora hapa."
1989, Classic Tales of Mulla Nasreddin, Retold by Houman Farzad, Translated from Persian by Diane L. Wilcox, Looking for the Missing Ring, Quote Page 26, Mazda Publishers, Costa Mesa, California. (Verified with scans by Quote Investigator; thanks to Stephen Goranson and Duke University library system)
1924 May 24, Boston Herald, Whiting’s Column: Tammany Has Learned That This Is No Time for Political Bosses, Quote Page
2, Column 1, Boston, Massachusetts.
na Rose Mwanri 🇹🇿 🏆 Shindano la Insha ya Methali 🥈 Mshindi wa Pili
Akiba kweli hazina, haijawahi saliti,
Kwetu ni muhimu sana, hutubeba kwa nyakati,
Kipindi kweli hatuna, inasimama kwa dhati,
Sote tuweke akiba, akiba ni mkombozi.
Creative Commons Attribution (CC BY 4.0) na Rose Mwanri Ilichapishwa na Maktaba.org Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
na Nankya Sauda 🇺🇬 Shindano la Insha ya Methali 🏆 Mshindi wa Kwanza 🥇
"Maisha tulivu ya upweke yasiobadilikaa huchochea akili na fikra bunifu."
"Maji hutulia pale ambapo mto una kina kirefu."
Creative Commons Attribution (CC BY 4.0) Inaruhusiwa kunakili, kutafsiri, kubadilisha na kuchapisha bila malipo ukitaja tu m/watunzi. Insha iliandikwa na Nankya Sauda Ilitafsiriwa na Brighid McCarthy Ilichapishwa na Maktaba.org Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org Created from "Weeping Willows by Akerselven" by Thorolf Holmboe, Public Domain 1907
na Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿 🏆 Shindano la Insha ya Methali 🥉 Mshindi wa Tatu
Siogopi jua wala mvua, nikiitengeneza kesho yangu
Siogopi maumivu Wala majeraha, maana yote ni ya muda
Jua kali na kazi ndiyo desturi yangu, ili kheri kuja maishani
Machinga,mkulima, makuli na mvuvi wao na jua, Ili kuitafuta kesho
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Ni mchana jua la utosi, kichwani nina mavuno, jasho linatiririka
Jua limezama Sasa kasia ufukweni, hoi kitandani, nyavu zi baharini
Nyumbani mtaa wa nne, nahodha wa familia surubu nivute kheri
Jua Sasa la chomoza, Kiguu na njia kulitafuta tonge
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Creative Commons Attribution (CC BY 4.0) na Magreth Lazaro Mafie Ilichapishwa na Maktaba.org Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Nilikuwa na Njaa sana; ilikuwa imechelewa sana; "Sufuria inayotazamwa huchemka pole pole," kama Poor Richard asemavyo.
Majambo ya binadamu yana kujaa na kupwa, Yakidakwa yamejaa huongoza ushindini; yakipuuzwa, safari yote ya maisha yao haiachi maji mafu, na hujaa madhilifu.
- BURUTO katika Juliasi Kaizari, na William Shakespeare (ilitafsiriwa na Mwalimu Nyerere)
KiChina: 趁熱打鐵
KiThai: ตีเหล็กเมื่อแดง
KiHindi: लोहा गरम हैं. मार दो हथौड़ा.
KiGaelic (Ireland): buail an t-iarann te
Kiingereza: Strike while the iron is hot.
Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
- Methali ya Kiswahili
"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
Unaweza kusafiri kwa meli peke yako,
kulala au kupumzika peke yako.
Unaweza kuingia kwenye deni peke yako.
Kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya peke yako.
Lakini ni lazima muwe wawili ili kucheza tango, muwe wawili ili kucheza tango...
ايد لوحدها ماتسقفش
Mkono mmoja hauwezi kupiga makofi
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Kidole kimoja hakiuwi chawa
Watu hutaka furaha mpya. Huwa tunaona kuwa watu wengine wana bahati zaidi kuliko sisi wenyewe. Mazao daima ni bora katika shamba la jirani yetu; ng'ombe wake hutoa maziwa zaidi.
दूर के ढोल सुहावने लगते हैं
Ngoma za mbali husikika vizuri
隔籬飯香
Wali wa jirani hunukia vizuri
隣の芝生は青く見える
Majani ya jirani huonekana kijana zaidi
соседняя очередь всегда движется быстрее
Foleni nyingine husogea kwa kasi zaidi
There's no such thing as a stupid question
Matone madogo ya maji,
Chembe kidogo za mchanga,
hutengeneza bahari kubwa
Na ardhi ya kupendeza
Vivyo hivyo zile dakika ndogo,
ingawa ni ndogo,
hutengeneza enzi za milele.
Bado tunayo hukumu hapa (duniani);
Tunafundisha tu umwagaji damu, ambayo, ukifundishwa, hurudi
ili lipiza kisasi na kumtesa mvumbuzi: mkono wa haki
huweka viungo vya kikombe chetu cha sumu
Kwa midomo yetu wenyewe. ( Makbeth Act I, Scene 7 )
Chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna ( Wagalatia 6:7 )
善有善報,惡有惡報
Wema hulipwa kwa wema, na ubaya kwa ubaya.
Wie man in den Wald hineinruft, so schallt es heraus
Unacholia msituni, kitasikika tena
"It may be that the politicians of the United States (a mistake in the print we presume for the state of New York) are not so fastidious as some gentlemen are, as to disclosing the principles on which they act. They boldly preach what they practice. When they are contending for victory, they avow the intention of enjoying the fruits of it. If they are defeated, they expect to retire from office -- IF THEY ARE SUCCESSFUL, THEY CLAIM, AS A MATTER OF RIGHT THE ADVANTAGES OF SUCCESS. THEY SEE NOTHING WRONG IN THE RULE, THAT TO THE VICTOR BELONGS THE SPOILS OF THE ENEMY.
A penny spar'd is twice got.
Senti iliyookolewa hupatikana mara mbili.
- Outlandish Proverbs by George Herbert (1640)
Matumizi ya pesa ndiyo faida zote zinayopatikana ukiwa na pesa.
Kwa pound [£] sita kwa mwaka [yaani riba] unaweza kutumia £ mia [yaani kupitia mkopo], kama unajulikana kama mwaminifu na mwenye busara.
Anayetumia groat [senti 4] kwa siku bure, hutumia pound £ zaidi ya sita kwa mwaka, ambazo ni bei ya kujipatia matumizi ya pound £ mia moja.
[Kwa hivyo] Anayepoteza muda wake wa thamani ya groat [senti 4] kwa siku, siku moja na nyingine, anapoteza fursa ya kutumia pound mia moja kila siku.
Anayepoteza muda wa shilingi tano kwa uvivu hupoteza shilingi tano, ni kama amezitupa tu baharini.
Anayepoteza shilingi tano sio tu kwamba anapoteza kiasi hicho, bali anapoteza pia faida yote ambayo ingeweza kupatikana kwa kuzitumia katika shughuli zake, ambayo, akiwa kijana, wakati wa uzee ingefikia kiasi kikubwa cha fedha.
Tena: anayeuza kwa mkopo huongeza bei ya kile anachokiuza kwa kiasi sawa riba angaliingiza na pesa hizo kwa kipindi ambacho atazikosa. Kwa hivyo, anayenunua kwa mkopo hulipa riba kwa kile anachonunua, na anayelipa pesa mara moja kwa kila anachonunua hukoa fursa ya kuzikopesha kwa wengine, kwa hivyo aliye na kitu alichonunua ameshalipa riba kwa matumizi yake.
Hata hivyo nasema kulipa mara moja unaponunua ni bora, kwa sababu anayeuza kwa mkopo anatarajia kupoteza asilimia tano ya mikopo; kwa hivyo anaongeza bei ya kile anachokiuza kwa asilimia ileile ili kuzuia hasara. Wanaolipa kwa mikopo hulipa kodi mara moja. Anayelipa kwa pesa mara moja anaweza kuzuia kodi hii
"Senti iliyohifadhiwa ni senti mbili hakika;
[haba] kwa siku ni [nne] kwa mwaka."
One man's meat is another man's poison
Nyama na mtu mmoja ni sumu ya mtu mwengine
Mwanangu, mguu wa kondoo katika mkono wako mwenyewe ni bora kuliko bega zima katika mkono wa mwengine; Afadhali kondoo mdogo aliye karibu na wee kuliko ng'ombe aliye mbali; Afadhali shomoro aliyeshikwa mkononi kuliko ndege elfu warukao angani; vazi ulilo nalo ni afadhali kuliko vazi la zambarau usiloliona.
- Hadithi ya Ahikar (ukurasa wa 110)
Un tiens vaut mieux que deux tu l'auras
'Shika-hii-hapa" moja ina thamana kuliko 'nitakuletea-baadaye' mbili
明日の百より今日の五十
Hamsini leo ni bora kuliko mia kesho
Meglio un uovo oggi che una gallina domani
Bora yai leo kuliko kuku kesho
Nikisikia nitasahau, nikiona nitakumbuka, nikifanya nitaelewa.
-Mwalimu Amos
Nyoka ana madhara.
-Mwalimu Shila