You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

New announcements
Discussions
Proverbs

Maji yaliyotulia ndiyo yenye kina kirefu

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 6mo ago
by
View this proverb in English
Still waters run deep
na Nankya Sauda 🇺🇬
Shindano la Insha ya Methali 🏆
Mshindi wa Kwanza 🥇

Maji yaliyotulia ndiyo yenye kina kirefu

Umewahi kuchukua muda na kujiuliza kwa nini wazee huwa wana busara zaidi kuliko vijana? Je, umewahi kuchukua muda wa kutafakari asili yako ulipochipuka? Ikiwa sivyo, [sasa] ni wakati mzuri wa kuanza kutafuta asili yako kwa sababu ni muhimu mtu ajue mizizi yake.
   Baada ya muda, unachukua mzigo wa kufunua asili ya watu mashuhuri wenye akili na haiba zao, utakuja kutambua kwamba wao ni introverts (yaani wakimya, wanaopenda kukaa peke yao/kujitenga) lakini ni mashuhuri. Ni muhimu uchukue muda wako, hata ukiwa bize, ujifunze kuhusu wasomi mashuhuri kama Albert Einstein, mwanasayansi mashuhuri ambaye alisema nukuu inayotuelimisha:
"Maisha tulivu ya upweke yasiobadilikaa huchochea akili na fikra bunifu."

Hii inamaanisha kwamba wakati ukiwa peke yako ni nafasi ya kujitafakari, lakini pia ni nafasi ya kutumia akili yako bunifu. Wanasema wazungumzaji wakubwa ni wanasheria wazuri, na tumeona hayo katika maisha yetu ya kila siku ambapo watu hutoa ahadi tupu, hutoa matamko ya uwongo ili kuwapendeza waliomzunguka bila kuchukua muda wa kufanya kitu kwa nia ya kutekeleza maneno yao. Kwa sababu hiyo, wengi wamepoteza imani na hawa wanaoitwa “wazungumzaji wakubwa.”
   Kwa upande mwingine, wakimya hutushangaza kwa matendo yao. Hatua zao hupangiliwa kila mara, matamanio yao ni wazi na vitendo vyao hufanyika kwa kusudi. Wapenzi wakimya hukuza mahusiano yao ya kimapenzi kwa ubunifu mpya ili kudumisha mahusiano. Waliowaajiri [wakimya] na waliokaa karibu na introverts husema kuwafahamu ni moja ya mafanikio makubwa katika maisha yao, ndo maana hawa wamefanya kazi nadhifu zaidi, wakawa na vipindi vyao vya kutafakari peke yao, na hatimaye walitoa kazi bora na kupata cheo kikubwa.
   Tunaweza kufafanua methali kama misemo inatumika katika nchi au utamaduni fulani. Ni maneno mafupi yenye busara na hutoa ushauri na vile vile kuongeza wazo kuhusiana na maisha ya kila siku. Kwa kweli, ili kufahamu kwa kina mila na desturi za kitamaduni, ni vizuri warejelee methali kwani zinaweza kuwa na maana pana ndani. 
Kihistoria, methali "Still waters run deep" (Maji yalotulia ndo yenye kina kirefu/Usicheze maji yanayosimama) inatoka Kilatini cha kale. Ilipata umaarufu baada ya Shakespeare kuitumia katika tamthilia yake ya Henry VI mwaka 1590. Alisema:
"Maji hutulia pale ambapo mto una kina kirefu."

Tunatambua kwamba, mara nyingi watu hatari zaidi walio na roho mbaya hupanga hatua zao na kuchukua hatua kwa wakati ambao wengine hatarajii. Ndio maana usaliti hutoka kwa watu ambao hatutarajii [kitu kama hicho] kutoka kwao. Kwa hiyo ni muhimu kwa mtu kuchukua si tu yale yanayokutana na macho bali pia kuchukua tahadhari hasa kutoka kwa watu ambao hawalipizi kisasi mara tu baada ya kukasirishwa au kukabiliwa.
   Albert Einstein licha ya tabia yake ya kujittenga, yeye anajulikana sana kwa kubuni nadharia yake ya relativity ambayo ilileta mapinduzi katika uelewa wetu wa nafasi ya nje, wakati, na kanimvutano (gravity).
   Kwa kumalizia, ni muhimu sana kutofikia hitimisho [haraka] kwa sababu sura hudanganya na kuna mengi ya kujua na kugundua kuliko macho yanavyoweza kuona.
Sources

Kuhusu Insha Hii

Insha hii ilishinda nafasi ya kwanza 🥇 katika Shindano la Insha ya Methali 🏆 July 2023
NANKYA SAUDA ni MWUGANDA  🇺🇬  anaye MIAKA 21 
Insha iliandikwa kwa Kiingereza juu ya methali "Still waters run deep."
Methali za Kiswahili ambazo ni karibu na hii ni:
Usicheze maji yanayosimama, na Kimya kingi kina mshindo mkuu.  

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
Inaruhusiwa kunakili, kutafsiri, kubadilisha na kuchapisha bila malipo ukitaja tu m/watunzi.
Insha iliandikwa na Nankya Sauda
Ilitafsiriwa na Brighid McCarthy
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Created from "Weeping Willows by Akerselven" by Thorolf Holmboe, Public Domain 1907 

Vitabu - Related Books on Maktaba.org 

Vitabu hivi vilivyotajwa kwenye insha vinapatikana bure:
Henry VI: Part II na William Shakespeare
Relativity: The Special and General Theory na Albert Einstein 
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Ustawi wa kiuchumi huenea na huwafikia raia wote wa nchi au eneo. Nchi haiwezi kufaidika bila raia wake wote kufaidika kwa namna moja au nyingine, kama vile baharini, maji yakijaa boti zote zitapanda, wimbi linalokuja litainua boti zote ziwe mitumbwi, jahazi, meli au mashua.

Msemo huo hutumiwa kumaanisha makundi yote yalinufaika kutokana na mabadiliko ya hali, hasa utitiri wa rasilimali, hata kama inaonekana kama zinawafikia matajiri wachache pekee. Nimesikia wafanyakazi wakiona wenzao wamepokea bonasi au kamisheni kubwa wanasema, "A rising tide lists all boats," ikimaanisha mauzo yakipanda, mapato ya kampuni yataongezeka na fursa kwa kampuni, na kwa hivyo, kwa wafanyikazi wote pia. Katika kesi hii, ni wazi wimbi halizinui boti zote kwa usawa au kiasi kilekile.

Wakosoaji wa methali hii wanaweza kulalamika kwamba methali hii inatumika pia ili kuhalalisha mpango au makubaliano yoyote hata kama yatawanufaisha wachache tu. Lakini kwa kawaida msemo huo husemwa  na viongozi kwa matumaini au kama pongezi.

Methali hiyo mara nyingi huhusishwa na John F. Kennedy rais wa Marekani, ambaye aliiitumia katika hotuba yake, mwaka wa 1963 akijitetea baada ya baada ya kukosolewa juu ya ujenzi wa bwawa ulitumia pesa nyingi sana (matumizi ya fujo). Mwandishi wa hotuba za Kennedy (aliyeitwa Ted Sorensen) alifichua kwamba Rais Kennedy alitumia methali hii baada ya kuisoma katika jarida la "New England Council."

Msemo karibu na huu ni "to grow the pie" yaani "kukuza keki" ambayo inamaanisha, kama keki ni kubwa zaidi, washiriki wote watapata keki zaidi hata kama uwiano/asilimia haibadiliki.

Je, unakubali kwamba ustawi mpana wa kiuchumi huwafikia wote?
...
Updated 6mo ago
by
Large tasks in life need to tackled in small steps, day by day. This proverb comes from Swahili:
Haba na haba hujaza kibaba
Little by little fills up the jar

Can you think of other similar proverbs that encourage the same way of thinking? 

This saying reminds be of a poem called "Little Things" by Julia Abigail Fletcher Carney:
Little drops of water,
Little grains of sand,
Make the mighty ocean
And the pleasant land.
     
Thus the little minutes,
Humble though they be,
Make the mighty ages
Of eternity. 
Julia Carney composed this poem in 1845 as a student in class -- and she was given only 10 minutes to write it!
...
Updated 6mo ago
by

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Updated 6mo ago
by

Do you have a big dream?

A dream too big for you to ever accomplish on your own? Maybe even too big to be accomplished in one generation?

Some gothic cathedrals in Europe took over 600 years -- more than 20 generations -- to complete! Although the Great Pyramid of Giza seems to have been built much faster (in a single generation), it also took tens of thousands of people.

In Tanzania, the Great Mosque of Kilwa was built in the 11th-14th centuries, rebuilt after earthquake damage, and continued to be remodeled up to the 18th century. It was described in the 1300s by Ibn Battuta. (You can take a 3D virtual tour of Kilwa! Check out the link in sources.)

The wonders of the world, modern and ancient, began as big dreams, dreams that took many generations to fulfill. Each generation continued the work of the past and also contributed to revising the blueprints for the future.

So if you are trying to do something great -- something that will really change the world -- don't expect to do it in one day. And don't try to do it alone. 

Related proverbs:


 Swahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako
If you want to go fast, go alone, if you want to go far, go together 

French:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
from Li Proverbe au Vilain, published around 1190
Modern French: Rome ne s'est pas faite en un jour
Rome wasn't built in a day

Chinese:
冰凍三尺,非一日之寒
Three feet of ice is not the result of one cold day

Scottish Gaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
It is not with the first strike that the tree will fall
...

Image credit: Screenshot from 3D virtual tour of Kilwa Kisiwani created by Zamani Project

Updated 6mo ago
by