You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Haraka haraka haina baraka

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 4mo ago
by
View this proverb in English
Haste makes waste (Haraka haraka haina baraka)
Methali ya leo ni "Haraka haraka haina baraka." Tafsiri yake kwa Kiingereza ni "Haste makes waste" au "Hurry hurry has no blessing" Mnaonaje - tafsiri ipi bora? Toeni maoni chini... 

Kwa upande wangu naona kwa mitazamo miwili. Methali hii inaweza kutufundisha:
  1. Subira: Haraka husababisha makosa, na makosa hutuzuia baraka. (Nenda taratibu)
  2. Mindfulness (yaani uwepo kiakili na utulivu): Tunapopoenda kwa haraka, hakuna muda wa kutambua, kutumia au kufurahia baraka tulizo nazo. 

Kuna misemo karibu na "haraka haraka haina baraka" katika nchi nyingi. Mifano: 
Kihispania: 
No por mucho madrugar amanece más temprano
(Kuamka mapema hakufanyi jua kuchomoza mapema)
Kifaransa: 
Tout vient a point a qui sait attendre
(Everything comes to those who wait)
Kiswahili:
 Pole pole ndio mwendo 
Kichina: 
欲速则不达
Methali hii ya Kichina ni karibu na "Haraka haraka haina baraka". Inatoka kitabu cha Misemo ya Konfusio (Analects, 13:17, ona ukurasa wa 92):
Tsz-hiá alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Kü-fu, aliomba ushauri wa Konfusio juu ya serikali,  Konfusio akajibu "Usitamani matokeo ya haraka. Usiangalie faida ndogo. Ukitaka matokeo ya haraka, hayatakuwa ya mbali; na ukizingatia faida ndogo huwezi kukabiliana vizuri na mambo muhimu."

Katika kitabu cha  "Methali za Kiswahili Zaidi kutoka Afrika Mashariki" waandishi Kalugila na Lodhi walitaja methali hii kama mfano mzuri wa mtindo wa ushauri katika methali:
Kwa mujibu wa tarehe/historia, yaelekea kuwa mithali zilitangulia tungo za ushairi, na watungaji wa Kiswahili walikuwa na fursa ya kutumia hazina kubwa ya mithali zilizohifadhiwa na wakuzaji wa masimulizi na mapokeo ambao wengi wao walikuwa wanawake. Mithali za hapo mwanzoni bila shaka zilitungwa kwa mitindo ya ushairi ambayo polepole ikatakata na kuweka imara miundo ya arudhi/prozodi zilizokubaliwa kuwa za kawaida. Mithali za Kiswahili za kawaida mno, na zilizo fupi pia, ni zenye mizani 6, 8, 12 au 16. Nyingi zao hutumika katika tunga kama mistari, vipande au mikarara/vipokeo. Kuna mifano ming i ya mashairi yanayoanzia na mithali fulani na pia ni maelezo marefu ya mithali yenyewe.Katika mifano ifuatayo kutoka mashairi mbalimbali kuna ikaa (mwendo wa ulinganiful ya 3 + 3, yaani mizani 6 parnoja na kituo cha kati na mkazo kwenye mizani ya mwisho ila moja: [Mifano:] Akili ni mali. Mahaba ni haba. Mapenzi majonzi.
Kituo katika mithali na fumbo kisababishacho vipande 2, 3 au 4 ni sawa na kituo chenye ikaa/mwendo katika mashairi ya vina yenye mizani kamiIi zinazolingana. Vina vyenyewe vinaweza kuelezwa kama ifuatavyo. [Mifano]:
Haraka haraka / haina baraka (aaba, 3+3/3+3)
(Kwa) haba na haba / hujaza kibaba. (aaba, 3+3/3+3)
 
Niliuliza Akili Bandia "Nifanye nini ili kutekeleza methali ya "haraka haraka haina baraka katika maisha yangu ya kila siku?" Hapa ni shauri zake: (Nilihariri nukuu)
Kuweka Mipango: Kabla ya kuanza kazi/mradi, chukua muda wa kuweka mipango. Gawanya kazi kubwa katika hatua ndogo zinazoweza kudhibitiwa, na ujipe muda wa kutosha kukamilisha kila hatua vizuri.
Kufanya Maamuzi: Usifanye maamuzi kwa haraka na ya haraka, hasa kuhusu mambo muhimu. Orodhesha chaguzi zako zote, pima faida na hasara, tafuta ushauri, kisha ufanye chaguo sahihi.
Kujifunza: Badala ya kujaribu kusoma kitabu, darasa au zoezi la nyumbani kwa haraka, nenda polepole, jiulize maswali, soma tena na tena hadi uelewe nyenzo kikamilifu. Kwa njia hii utajifunza kweli na kukumbuka habari, badala ya kuisahau haraka. Pia utafurahia kujifunza mengi zaidi!
Mahusiano: Kujenga mahusiano imara huchukua muda. Iwe na marafiki, familia, au mapenzi, usikimbilie. Wekeza muda katika kumfahamu mtu, kumwelewa, na kujenga msingi imara.
Kazi: Zingatia ubora kuliko kasi, na uchukue muda wako wa mapumziko ili kuepuka uchovu. Epuka kuharakisha kazi zako ili kuzimaliza haraka. Ukienda haraka hautafanya kazi yenye ubora wa juu, lakini pia kufanya kazi kwa makini hukusaidia kujifunza na kukua.
Afya: Usitafute suluhisho la haraka wala njia za mkato katika masuala ya afya yako. Mazoezi, chakula safi, na mapumziko ni muhimu, na yote yanahitaji muda.
Kujiboresha: Ukuaji na maendeleo ya kibinafsi ni mchakato wa muda mrefu. Usiharakishe. Weka malengo yanayoweza kufikiwa, yafanyie kazi hatua kwa hatua, na uthamini ushindi mdogo unaoendelea.
Mindfulness (uwepo wa kiakili): Kuwa makini na mahali ulipo na kile unachokifanya. Wakati wa kula, furahia ladha kile unapotafuna. Unapozungumza na mtu, mzikilize kwa makini. "Haraka haraka haina baraka" inatufundisha maisha ni safari. 
Naona Akili Bandia alinipa ushauri mzuri wa busara... Ningependa kujua maoni yenu :)

Vitabu Vinavyohusiana:
More Swahili Proverbs from East Africa: Methali zaidi za kiswahili toka Afrika Mashariki by Leonidas Kalugila and Abdulaziz Y. Lodhi, ukurasa wa 77
Methali za Kiswahili - Swahili Proverbs ukurasa wa 202
Misemo ya Konfusio - Analects, 13:17, ukurasa wa 92 (Kiingereza kutoka Kichina)
Interpersonal Communication - A Mindful Approach to Relationships 

Sources
Rasilimali:
Mindfulness (Jamii forums)
Wiktionary - "Haraka haraka haina baraka"
Swahili Proverbs about Hurry and Patience collected by Albert Scheven, Center for African Studies, University of Illinois, Urbana-Champaign
Google translate inaonyesha "Haste makes waste" tafsiri yake ni "Haraka haraka haina baraka" na inasema "reviewed by contributors." Lakini ukibadilisha nafasi (back translate) utaona "Haste has no blessing." Hm... Ipi bora?

Vyanzo vya methali za lugha nyingine:
Kichina: (Wiktionary)  (BBC)
Kihispania: (Wiktionary)
Kifaransa (le dictionnaire Orthodidacte)
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Siku moja, mfanyabiashara mashuhuri alitafuta msaidizi. Alipokea maombi na CV za watu wengi sana, lakini wawili tu walikidhi vigezo: Amina na Baraka. Ili kuamua kati yao, aliwaita wote wawili, na akawaalika waje kwaajili ya mahojiano ya ajira, kesho yake asubuhi. "Saa tatu kamili -- vaa mavazi ya kazi, na usichelewe!" Akawaonya.

Kesho yake Ali aliwahi kuamka, akavaa suti yake nzuri, na alipanda basi kijijini kwake saa 2. "Bora kinga kuliko tiba" alifikiria. Njiani kuelekea mjini, basi ilianza kutoa moshi. Abira wote walishuka na waliachwa porini. Hapo hapo mvua ilianza kunyesha. Kila basi lililompita, Ali akaomba nafasi, lakini, kutokana na hali ya hewa, mabasi yote yalikuwa yameshajaa. Kwa hivyo ikabidi atembee kwa miguu. Ilipotimia saa tatu, bado Ali alikuwa mbali na mji, na mvua ikawa kali zaidi na zaidi. "Lazima niendelee" akajiambia, "Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa."

Wakati huohuo mjini, Baraka aliamka ghorofani kwake, na akashtuka ghafla akiona jua lilikuwa limeshafika mbali angani. "Aisee! Niliweka alarm! Simu yangu ina shida gani sasa?" Alitazama saa ukutani: Saa tatu kamili. "Bora niache tu. Hata nikiondoka saivi, bado nitachelewa kufika. Si alisema usichelewe? Hatamwajiri aliyechelewa." Kwa hivyo Baraka, akiwa na huzuni, akalala tena.

Saa nne na nusu, hatimaye, Ali alifika ofisini kwa mfanyabiashara na kugonga mlango, suti yake ikichuruzika maji na matope sakafuni. Mfanyabiashara akajibu. "Si nilikwambia vaa mavazi yanayofaa na usichelewe? Sasa umechelewa zaidi ya saa limoja na mavazi yako yamechafuka. Niambie nitawezaje kukuajiri baada ya hapo?" Kisha Ali akaeleza yote yaliyomtokea. Mfanyabishara akamjibu "Nimejifunza mengi kuhusu wewe kutoka kwa hadithi yako Ali. Ukiwa na kusudi kichwani, utafanya kazi kwa bidii, na pale unapokutana na vikwazo hukati tamaa, hata kama umechelewa. Nakwambia, wewe ndiye wa kwanza kufika leo. Mwingine alikosa kabisa. Nitakuajiri wewe."

Mafanikio makubwa huanza na makosa mengi, lakini baada ya muda, uvumilivu na ustahilimilu huleta matunda. Kukosa ni uanadamu, lakini Mungu ni mvumilivu sana kwetu. Anatupa nafasi nyingi za kujifunza na kujaribu tena, ilimradi tusikate tamaa.

Wengine wanasema methali ya "Better late than never never" inatoka kwa kitabu cha The Canterbury Tales, kilichoandikwa na Chaucer miaka ya 1390.
Better than never is late
“Bora kuliko kamwe ni kuchelewa
-The Canterbury Tales, The Canon's Yeoman's Tale
Wengine wanasema chimbuko la kweli ni kitabu cha Historia ya Roma, kilichoandikwa na Livy takriban mwaka wa 20 KK.
Lilatini: potiusque sero quam numquam
Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa
- History of Rome, Book 4

Methali ya Kiingereza inayoendana ni:
It's never too late
Hakuna kuchelewa
 Methali ya Kiingereza inayopinga:
Don't close the gate after the horse has bolted.
Usifunge mlango baada ya farasi kukimbia

Methali ya Kihindi: 
जब जाति तब सवेरे
Wakati wowote unapoamka, ndo asubuhi yako

...

Fikiria kama umechelewa Mahojiano ya Ajira. Ungefanyaje? Next time unapofikiri "Nimeshachelewa" jiambie "Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa." Kwa mfano makala hii ya Methali ya Siku ilichelewa, lakini sasa unaisoma - Asante!

Updated 4mo ago
by
What one person throws away may be useful and valuable to someone else.

This saying is often used to describe either the diversity of human preferences or to express optimism that humans are quite creative when it comes to repurposing or recycling what other people throw away.

For example, entrepreneur Gibson Kiwago, founder of WAGA Tanzania, recycles old laptop batteries to power homes and businesses in Tanzanzia. Check out our E-Waste Reading List!

The notion that people subjectively assess quality has been around a long time. The saying derives from a 17th century proverb:
One man's meat is another man's poison.

Have you ever seen value in something that someone else threw away?
...
Updated 4mo ago
by
Large tasks in life need to tackled in small steps, day by day. This proverb comes from Swahili:
Haba na haba hujaza kibaba
Little by little fills up the jar

Can you think of other similar proverbs that encourage the same way of thinking? 

This saying reminds be of a poem called "Little Things" by Julia Abigail Fletcher Carney:
Little drops of water,
Little grains of sand,
Make the mighty ocean
And the pleasant land.
     
Thus the little minutes,
Humble though they be,
Make the mighty ages
Of eternity. 
Julia Carney composed this poem in 1845 as a student in class -- and she was given only 10 minutes to write it!
...
Updated 4mo ago
by
A penny that stays in your pocket can be used for another purpose. It could be used to buy something else, or you could lend or invest it to yield more money in the future. In economics, this principle is called "opportunity cost". When we spend money or time on one thing, we also lose the opportunity to use it for something else.

This proverb is usually attributed to Benjamin Franklin, but he did not originate it, nor did he use the exact phrase. Similar versions of the proverb appear in earlier sources. For example:
A penny spar'd is twice got.
- Outlandish Proverbs by George Herbert (1640) 

In Poor Richard's Almanac (1736), Benjamin Franklin quotes the proverb and explains it well:
Necessary Hints to Those That Would Be Rich
The use of money is all the advantage there is in having money. For six pounds a year [interest] you may have the use of one hundred pounds [a loan], provided you are a man of known prudence and honesty.
He that spends a groat [4 pence] a day idly spends idly above six pounds a year, which is the price for the use of one hundred pounds.
He that wastes idly a groat's [4  pence] worth of his time per day, one day with another, wastes the privilege of using one hundred pounds each day.
He that idly loses five shillings' worth of time loses five shillings, and might as prudently throw five shillings into the sea.
He that loses five shillings not only loses that sum, but all the advantage that might be made by turning it in dealing, which by the time that a young man becomes old will amount to a considerable sum of money.
Again, he that sells upon credit asks a price for what he sells equivalent to the principal and interest of his money for the time he is to be kept out of it, therefore, he that buys upon credit pays interest for what he buys, and he that pays ready money might let that money out to use, so that he that possesses anything he has bought pays interest for the use of it.
Yet in buying goods it is best to pay ready money, because he that sells upon credit expects to lose five per cent by bad debts; therefore he charges on all he sells upon credit an advance that shall make up that deficiency. Those who pay for what they buy upon credit pay their share of this advance. He that pays ready money escapes, or may escape, that charge.
"A penny saved is twopence clear;
A pin a day's a groat a year."

So, next time you think about spending money or time on something, ask yourself what the opportunity cost might be. If you didn't spend it, could you lend it to someone else? Could you pay off your existing debts? Could you invest in something that might bring a larger profit in the future?

...
Updated 4mo ago
by