You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Taarifa
Majadiliano
Methali

Haraka haraka haina baraka

Ili kupiga KURA kwa Methali ya Mwezi
Kura
0
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
View this proverb in English
Haste makes waste (Haraka haraka haina baraka)
Methali ya leo ni "Haraka haraka haina baraka." Tafsiri yake kwa Kiingereza ni "Haste makes waste" au "Hurry hurry has no blessing" Mnaonaje - tafsiri ipi bora? Toeni maoni chini... 

Kwa upande wangu naona kwa mitazamo miwili. Methali hii inaweza kutufundisha:
  1. Subira: Haraka husababisha makosa, na makosa hutuzuia baraka. (Nenda taratibu)
  2. Mindfulness (yaani uwepo kiakili na utulivu): Tunapopoenda kwa haraka, hakuna muda wa kutambua, kutumia au kufurahia baraka tulizo nazo. 

Kuna misemo karibu na "haraka haraka haina baraka" katika nchi nyingi. Mifano: 
Kihispania: 
No por mucho madrugar amanece más temprano
(Kuamka mapema hakufanyi jua kuchomoza mapema)
Kifaransa: 
Tout vient a point a qui sait attendre
(Everything comes to those who wait)
Kiswahili:
 Pole pole ndio mwendo 
Kichina: 
欲速则不达
Methali hii ya Kichina ni karibu na "Haraka haraka haina baraka". Inatoka kitabu cha Misemo ya Konfusio (Analects, 13:17, ona ukurasa wa 92):
Tsz-hiá alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Kü-fu, aliomba ushauri wa Konfusio juu ya serikali,  Konfusio akajibu "Usitamani matokeo ya haraka. Usiangalie faida ndogo. Ukitaka matokeo ya haraka, hayatakuwa ya mbali; na ukizingatia faida ndogo huwezi kukabiliana vizuri na mambo muhimu."

Katika kitabu cha  "Methali za Kiswahili Zaidi kutoka Afrika Mashariki" waandishi Kalugila na Lodhi walitaja methali hii kama mfano mzuri wa mtindo wa ushauri katika methali:
Kwa mujibu wa tarehe/historia, yaelekea kuwa mithali zilitangulia tungo za ushairi, na watungaji wa Kiswahili walikuwa na fursa ya kutumia hazina kubwa ya mithali zilizohifadhiwa na wakuzaji wa masimulizi na mapokeo ambao wengi wao walikuwa wanawake. Mithali za hapo mwanzoni bila shaka zilitungwa kwa mitindo ya ushairi ambayo polepole ikatakata na kuweka imara miundo ya arudhi/prozodi zilizokubaliwa kuwa za kawaida. Mithali za Kiswahili za kawaida mno, na zilizo fupi pia, ni zenye mizani 6, 8, 12 au 16. Nyingi zao hutumika katika tunga kama mistari, vipande au mikarara/vipokeo. Kuna mifano ming i ya mashairi yanayoanzia na mithali fulani na pia ni maelezo marefu ya mithali yenyewe.Katika mifano ifuatayo kutoka mashairi mbalimbali kuna ikaa (mwendo wa ulinganiful ya 3 + 3, yaani mizani 6 parnoja na kituo cha kati na mkazo kwenye mizani ya mwisho ila moja: [Mifano:] Akili ni mali. Mahaba ni haba. Mapenzi majonzi.
Kituo katika mithali na fumbo kisababishacho vipande 2, 3 au 4 ni sawa na kituo chenye ikaa/mwendo katika mashairi ya vina yenye mizani kamiIi zinazolingana. Vina vyenyewe vinaweza kuelezwa kama ifuatavyo. [Mifano]:
Haraka haraka / haina baraka (aaba, 3+3/3+3)
(Kwa) haba na haba / hujaza kibaba. (aaba, 3+3/3+3)
 
Niliuliza Akili Bandia "Nifanye nini ili kutekeleza methali ya "haraka haraka haina baraka katika maisha yangu ya kila siku?" Hapa ni shauri zake: (Nilihariri nukuu)
Kuweka Mipango: Kabla ya kuanza kazi/mradi, chukua muda wa kuweka mipango. Gawanya kazi kubwa katika hatua ndogo zinazoweza kudhibitiwa, na ujipe muda wa kutosha kukamilisha kila hatua vizuri.
Kufanya Maamuzi: Usifanye maamuzi kwa haraka na ya haraka, hasa kuhusu mambo muhimu. Orodhesha chaguzi zako zote, pima faida na hasara, tafuta ushauri, kisha ufanye chaguo sahihi.
Kujifunza: Badala ya kujaribu kusoma kitabu, darasa au zoezi la nyumbani kwa haraka, nenda polepole, jiulize maswali, soma tena na tena hadi uelewe nyenzo kikamilifu. Kwa njia hii utajifunza kweli na kukumbuka habari, badala ya kuisahau haraka. Pia utafurahia kujifunza mengi zaidi!
Mahusiano: Kujenga mahusiano imara huchukua muda. Iwe na marafiki, familia, au mapenzi, usikimbilie. Wekeza muda katika kumfahamu mtu, kumwelewa, na kujenga msingi imara.
Kazi: Zingatia ubora kuliko kasi, na uchukue muda wako wa mapumziko ili kuepuka uchovu. Epuka kuharakisha kazi zako ili kuzimaliza haraka. Ukienda haraka hautafanya kazi yenye ubora wa juu, lakini pia kufanya kazi kwa makini hukusaidia kujifunza na kukua.
Afya: Usitafute suluhisho la haraka wala njia za mkato katika masuala ya afya yako. Mazoezi, chakula safi, na mapumziko ni muhimu, na yote yanahitaji muda.
Kujiboresha: Ukuaji na maendeleo ya kibinafsi ni mchakato wa muda mrefu. Usiharakishe. Weka malengo yanayoweza kufikiwa, yafanyie kazi hatua kwa hatua, na uthamini ushindi mdogo unaoendelea.
Mindfulness (uwepo wa kiakili): Kuwa makini na mahali ulipo na kile unachokifanya. Wakati wa kula, furahia ladha kile unapotafuna. Unapozungumza na mtu, mzikilize kwa makini. "Haraka haraka haina baraka" inatufundisha maisha ni safari. 
Naona Akili Bandia alinipa ushauri mzuri wa busara... Ningependa kujua maoni yenu :)

Vitabu Vinavyohusiana:
More Swahili Proverbs from East Africa: Methali zaidi za kiswahili toka Afrika Mashariki by Leonidas Kalugila and Abdulaziz Y. Lodhi, ukurasa wa 77
Methali za Kiswahili - Swahili Proverbs ukurasa wa 202
Misemo ya Konfusio - Analects, 13:17, ukurasa wa 92 (Kiingereza kutoka Kichina)
Interpersonal Communication - A Mindful Approach to Relationships 

Marejeleo
Rasilimali:
Mindfulness (Jamii forums)
Wiktionary - "Haraka haraka haina baraka"
Swahili Proverbs about Hurry and Patience collected by Albert Scheven, Center for African Studies, University of Illinois, Urbana-Champaign
Google translate inaonyesha "Haste makes waste" tafsiri yake ni "Haraka haraka haina baraka" na inasema "reviewed by contributors." Lakini ukibadilisha nafasi (back translate) utaona "Haste has no blessing." Hm... Ipi bora?

Vyanzo vya methali za lugha nyingine:
Kichina: (Wiktionary)  (BBC)
Kihispania: (Wiktionary)
Kifaransa (le dictionnaire Orthodidacte)
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
This proverb means that there are some things you can't do alone. The tango is dance for two people, so you can't dance the tango alone.

The proverb comes from a 1952 song It Takes Two to Tango:
You can sail in a ship by yourself,
Take a nap or a nip by yourself.
You can get into debt on your own.
There are lots of things that you can do alone.
But it takes two to tango, two to tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning and Pearl Bailey) - Check out the sources to listen to the original recording!

This proverb has many different meanings that you can apply in your daily life and relationships.  There are lots of things in life that require more than one person: It takes two people to cooperate, to make a bargain or to engage in a fight. You may really want to dance with someone, but if they don't want to dance with you, it's better to move on.  Similarly, if you're in a fight, consider how your own behavior might be contributing to continuing the fight. A dance isn't about being perfect, it's about being in time with your partner and enjoying the experience. 

Similar proverbs from Africa:
Egyptian (Arabic):
ايد لوحدها ماتسقفش‎
One hand can't clap

Swahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Without a second person a quarrel cannot start

Kidole kimoja hakiuwi chawa
One finger doesn't kill a louse

...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Huwa tunatendewa kama tunavyowatendea wengine. Kwa kawaida methali hii hutumika kama onyo, au wakati mtu mbaya anapata alichostahili. Lakini pia inaweza kutumika kama tumaini la baraka kwa wale wanaofanya mema. Chimbuko halisi cha methali hiyo haijulikani, lakini ilianza Amerika miaka za 60 hivi. Inaendana na kanuni la Karma katika dini ya Kihindi.

Methali na nukuu zinazohusiana:
Shakespeare
Bado tunayo hukumu hapa (duniani);
Tunafundisha tu umwagaji damu, ambayo, ukifundishwa, hurudi
ili lipiza kisasi na kumtesa mvumbuzi: mkono wa haki
huweka viungo vya kikombe chetu cha sumu
Kwa midomo yetu wenyewe.  ( Makbeth Act I, Scene 7 )
Biblia:
Chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna ( Wagalatia 6:7 )
Kichina: 
善有善報,惡有惡報
Wema hulipwa kwa wema, na ubaya kwa ubaya. 
Kijerumani:
Wie man in den Wald hineinruft, so schallt es heraus
Unacholia msituni, kitasikika tena
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Je, umewahi kuona muda huenda pole pole wakati unasubiri? Lakini kwa upande mwingine, ukivutiwa na mambo mengine, m muda huenda haraka.

Kwa mfano, ukisubiri kumwona daktari, muda ni mfupi ukiangalia simu yako au kusoma gazeti, badala ya kungoja tu kusikia jina lako liitwe.

Chimbuko cha methali hii ni Benjamin Franklin kwa Poor Richard's Almanac, hata hivyo haionekani hapo. Badala yake, Franklin aliitumia katika insha juu ya 'sumaku ya wanyama' mwaka 1785. 
Nilikuwa na Njaa sana; ilikuwa imechelewa sana; "Sufuria inayotazamwa huchemka pole pole," kama Poor Richard asemavyo.
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Hapo zamani za kale, palikuwa na binti mrembo, mkarimu, mwenye akili aliyeitwa Poshia. Wanaume wengi walitaka kumuoa na walikuja ili kuomba uchumba. Baba Poshia alikuwa amefariki dunia. Alikuwa tajiri na aliacha wosia ulioelekeza kamba yeyote aliyetaka kumuoa Poshia, lazima achague kati ya masanduku tatu: sanduku la dhahabu, sanduku la fedha na sanduku la risasi. Atakayechagua sahihi ndiye atakayeruhusiwa kumuoa Poshiia na kurithi mali zote za Baba Poshia. Siku moja, Mfalme wa Moroko alikuja ili kuomba uchumba.

Mabepari wa Venisi

Tazama ▶️ YouTube


POSHIA: Kayavute mapazia masanduku yaonekane kwake mtukufu huyu mtoto wa mfalme. Haya sasa kachague.

MOROKO: La kwanza, ni la dhahabu, lenye maandiko haya:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
Na la pili, ni la fedha, linaloahidi hivi: 
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
La, tatu, risasi butu, na onyo lake ni butu:
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
Nitajuaje yakuwa nimechagua vizuri?

POSHIA: Moja lina picha yangu, mzawa wa mfalme: Ukilichagua hilo basi na mimi ni wako.

MOROKO: Muungu Fulani uniongoze. Hebu nione; nitayachagua tena maandiko toka mwisho. Nitaanzia la tatu: lasemaje, la risasi?
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
Itambidi atoe - atoleeni? Risasi? Na pia ahatarishe - kwa ajili ya risasi? Sanduku hili latisha: wahatarishao vyote hutumaini kupata faida iliyo nzuri: Wenye moyo wa dhahabu hawajali takataka; Kwa hiyo basi sitoi na wala sihatarishi chochote nilicho nacho kwa sababu ya risasi. La fedha lasema nini, lenye rangi ya baridi?
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
Apate astahilicho! Subiri hapa, Moroko. Upime thamani yako kwa mkono wa mwadilifu: Kama ukithaminiwa vile ujifanidivyo wastahili kutosha; walakini ya kutosha inaweza isitoshe kumpata siti huyu. Bali nikitia shaka kuwa simstahili,Basi hapo nitakuwa najiumbua mwenyewe. Stahili yangu ni nini? Bila shaka ni bibie. Namstahili, hakika, kwa nasaba na kwa mali, kwa madaha na kwa sifa zote za malezi mema na kuzidi yote hayo namstahili kwa pendo. Vipi, nisiendelee, nichague papa hapa?
Hebu tuyaone tena ya sanduku la dhahabu:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Naam, ni siti huyu; anotamaniwa kote. Toka pande zote nne za dunia wanakuja kubusu sanamu hii takatifu ilo hai: Majangwa ya Hirikani na nyika pana ajabu, za Uarabuni kote, sasa zimekuwa njia ziletazo watawala kumwona Poshia bora. Nayo dola ya bahari ambayo inapofura hutemea hata mbingu, haiwezi kuzuia nia ya wageni hao; ila wanazidi kuja, kama wavuka kijito, kumwona Poshia bora. Moja la matatu haya lina picha yake nzuri. Itawezekana kweli liwe lile la risasi? Wazo chafu kama hilo lingekuwa ni laana. Halifai japo kuwa sanda yake ya kaburini.
Au niwaze ya kuwa kawekwa ndani ya fedha? Moja ya kumi na moja ya thamani ya dhahabu? Hilo ni wazo la dhambi! Kito cha thamani hivi hakiwekeki po pote ila ndani ya dhahabu. Uingereza wanayo sarafu tu ya dhahabu, ambayo kwa juu yake imechapwa malaika. Bali hapa malaika mwenyewe hasa yu ndani ya sanduku hili hapa, na bahati nijaliwe!

POSHIA: Ni huu hapa, chukua, mzawa wa mfalme; kama sura yangu imo nimekuwa mali yako.

[Anafungua sanduku la dhahabu]
MOROKO: Mama yang! Nini hii? Ni fuu tupu la kichwa, ambalo katika jicho lina hati ma’ndiko. Nitasoma maandiko.
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.
Nimefarikiwa kweli. Bure nimejitanibu. Basi buriani, joto; nawe, makiwa, karibu. Basi kwa heri Poshia. Ninayo
huzuni sana siwezi kwa heri ndefu: Ndivyo wanavyoagana watu waliopoteza.
[Aondoka na Wafuasi wake. Tarumbeta]
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by