You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

New announcements
Discussions
Proverbs

Kalamu hushinda jambia

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 6mo ago
by
View this proverb in English
The pen is mightier than the sword

Ufafanuzi


Methali hii ya Kiingereza inatafsirika pia kama "Kalamu ina nguvu kuliko upanga au jambia" au " Kalamu ni kali kuliko upanga." Katika methali hii, jambia au upanga unaashiria nguvu na ukatili, na maana ya kalamu ni maneno. Ingawa upanga unaweza kushinda kwa nguvu, kalamu inaweza kuwashawishi, kuwahamasisha, na kuwaelimisha watu. Sio kila mtu ana silaha za kuwalazimisha watu wengine kufanya kile anachotaka, lakini kila mtu ana uwezo wa kubadilisha ulimwengu kupitia kile anachofikiria, kusema na kuandika kwa maneno. 

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
 - Methali ya Kiswahili

Methali hii ni kweli kwa sababu mara nyingi maneno huchochea na kudhibiti jinsi watu wanavyotumia nguvu na silaha zao. Kwa mfano, kupitia sheria, maneno ya viongozi, mahakimu na majaji yana uwezo wa kuwafunga watu gerezani au hata kuwaua. Kutoa hotuba ya moto kwa umati wa watu wenye hasira kunaweza kuleta ghasia kali na madhara mengine (ona Juliasi Kaizari).

"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)

Lakini pia, methali hiyo inatukumbusha nguvu ya upinzani usio na vurugu kwenye kuleta mabadiliko ya kudumu, kanuni iliyotetewa na kuonyeshwa na watu kama Mahatma Gandhi, Martin Luther King, na Nelson Mandela.  Angalia pia: Insha ya "Civil Disobedience"  na Henry David Thoreau, pamoja na Tamthilia mashuhuri ya "Antigone" na Sophocles.

Chimbuko


Nukuu hii ya "kalamu ina nguvu kuliko upanga" ilipata umaarufu kupitia tamthilia ya "Richelieu: au The Conspiracy"  na Edward Bulwer-Lytton (mwaka wa 1839, ukurasa wa 47). Lakini hakika wazo lilikuwepo kabla.

Wengine wanasema chimbuko halisi la methali hii ni Hadithi ya Ahikar. Kitabu hiki kiliandikwa takriban miaka 600 kabla ya kristu, na ni chimbuko la methali zingine kama "Ndege mkononi ana thamani ya wawili mtini"). Katika toleo letu, mfasiri hakuweza kusoma maandishi kutokana na hali ya karatasi, na maneno yalikatika. (Ukurasa 171/274
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na  ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa  ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Je, hili ndilo chimbuko halisi la methali hii, miaka zaidi ya 2,500 iliyopita? Muwe majaji...

Chanzo karibu na methali hii pia kinaonekana katika Agano la Kale:
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia

Na vilevile katika Shakespeare: 
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)

 Je, unakubali kalamu hushinda jambia? Toa maoni yako hapo chini!
Details CC BY Unaruhusiwa kunakili & kusambaza mchoro huu na makala hii bila idhini, ukitaja tu chanzo (www.maktaba.org)
Sources
The pen is mightier than the sword (Wikipedia)
Story of Ahikar (Page 171/274
Hebrews 4:12 (KJV)
William Shakespeare Hamlet Act 2, scene II (page 59)
Henry David Thoreau's Essay, "Civil Disobedience"
Sophocles' play, "Antigone"
Edward Bulwer-Lytton's 1839 play "Richelieu: Or the Conspiracy"
You furnish the pictures and I'll furnish the war. - William Randolph Hearst (Wikipedia: Yellow Journalism)
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Je, umewahi kuona muda huenda pole pole wakati unasubiri? Lakini kwa upande mwingine, ukivutiwa na mambo mengine, m muda huenda haraka.

Kwa mfano, ukisubiri kumwona daktari, muda ni mfupi ukiangalia simu yako au kusoma gazeti, badala ya kungoja tu kusikia jina lako liitwe.

Chimbuko cha methali hii ni Benjamin Franklin kwa Poor Richard's Almanac, hata hivyo haionekani hapo. Badala yake, Franklin aliitumia katika insha juu ya 'sumaku ya wanyama' mwaka 1785. 
Nilikuwa na Njaa sana; ilikuwa imechelewa sana; "Sufuria inayotazamwa huchemka pole pole," kama Poor Richard asemavyo.
...
Updated 6mo ago
by
Compare this simple, humble basket of fruit with a bag of lollipops. The fruit is ripe, juicy, packed full of vitamins -- it just sells itself. The lollipops, on the other hand, scream for our attention with explosive slogans and neon colors. But underneath the shiny packaging, it's really just plain sugar with some food coloring and artificial flavors.

Like other primates, humans find fruit attractive because it gives us energy and nutrition. Candy gives us energy, but it doesn't give us real nutrition. It just does a very clever job pretending to be fruit. Don't fall for it!

A good thing doesn't need to advertise, because quality speaks for itself. As the economists would say, demand exceeds supply.  Many advertisements seems to promise us happiness, beauty, love, wealth or respect. But ask yourself, does the ad promise more than the product can really deliver? Coca-Cola isn't a love potion.

This proverb reminds us of the enduring value of true quality and competence over flashy appearances. It's often used to express skepticism about a person who brags or praises themselves excessively.

We should all strive to be more like the basket of fruit: simple, authentic and good. These qualities will draw other people to you — at least the kind of people who understand that “chema chajiuza, kibaya chajitembeza

Related proverbs:
Don't judge a book by its cover.
Appearances are deceiving.
All that glitters is not gold 
 高嶺の花  Hana yori dango - Dumplings over flowers

...
Updated 6mo ago
by
Our proverb today comes from Swahili.
Ukitaka uvunguni sharti uiname
If you want something underneath [the bed] you must bend down
This proverb is usually used to encourage hard work and dedication. We can't expect to find the things we are searching for unless we are willing to looking in places that aren't easy to reach.

Here's a story that illustrates the proverb. The story is about Mulla Nasreddin, a humorous character often seen in Sufi folklore.
Mulla [Nasreddin] had lost his ring in the living room. He searched for it for a while, but since he could not find it, he went out into the yard and began to look there. His wife, who saw what he was doing, asked: “Mulla, you lost your ring in the room, why are you looking for it in the yard?” Mulla stroked his beard and said: “The room is too dark and I can’t see very well. I came out to the courtyard to look for my ring because there is much more light out here.”
-  Retold by Houman Farzad, Translated from Persian by Diane L. Wilcox (1989)

In English, a similar story is often told with a drunkard looking for money (or keys). Here is a version from the Boston Herald (1924):
[A police officer encountered a man groping about on his hands and knees]
“I lost a $2 bill down on Atlantic avenue,” said the man. “What’s that?” asked the puzzled officer. “You lost a $2 bill on Atlantic avenue? Then why are you hunting around here in Copley square?” “Because,” said the man as he turned away and continued his hunt on his hands and knees, “the light’s better up here.”

This story has come to be known as the streetlight effect in science.

Thank you to one of our members for suggesting this proverb! 🙏
Do you have a proverb to suggest? Share it here!


...

This picture was created using AI. What do you think?

Updated 6mo ago
by
Kuna vitu ambavyo huwezi kufanya peke yako. Tango ni mchezo (densi) ya watu wawili, kwa hivyo huwezi kucheza tango peke yako.

Methali hii inatoka wimbo ulioimbwa 1952, It Takes Two to Tango:
Unaweza kusafiri kwa meli peke yako,
kulala au kupumzika peke yako.
Unaweza kuingia kwenye deni peke yako.
Kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya peke yako.
Lakini ni lazima muwe wawili ili kucheza tango, muwe wawili ili kucheza tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning na Pearl Bailey) Ona vyanzo/sources ili kusikiliza wimbo huu!

Methali hii ina maana nyingi tofauti ambazo unaweza kutekeleza katika mahusiano na maisha yako ya kila siku. Mambo mengi huhitaji watu zaidi ya mmoja: Wawili wanatakiwa ili kushirikiana, kufanya biashara ama kupigana. Ukitaka kucheza na mtu ambaye hataki kucheza na wewe, bora kumtafuta mchezaji mwengine.. Vivyo hivyo, ukiwa kwenye mgogoro au magomvi, itabidi ufikirie jinsi tabia yako inavyoweza kuchangia katika kuendeleza shida. katika dance, lengo si kuwa mkamilifu, bali ni kuendana na mwenzako na kufurahia pamoja.
Methali zinazofanana kutoka Afrika: 
Kimisri (Kiarabu): 
ايد لوحدها ماتسقفش‎
Mkono mmoja hauwezi kupiga makofi
Kiswahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Kidole kimoja hakiuwi chawa
...
Updated 6mo ago
by