You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs
Akiba Haiozi
Join
or login
to VOTE
Votes
59
View this proverb in English
Savings don't rot
na Rose Mwanri 🇹🇿 
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥈 Mshindi wa Pili 

Akiba Haiozi

Methali ni usemi wa kimafumbo unaotumika katika jamii. Maneno katika methali huwa na maana ya ziada na methali huwa na pande mbili. Upande wa kwanza hutoa wazo na upande wa pili humalizia wazo. Akiba haiozi ni miongoni mwa methali za kiswahili inayotumika sana katika jamii za kiafrika na kwa watumiaji wa lugha ya kiswahili duniani, ikiwa na lengo la kuwaasa watu juu ya umuhimu wa kujiwekea akiba.

 Dhima ya methali hii ni kutusisitiza sisi wanajamii kujianda vema na maisha ya leo pamoja na kesho huku tukiwa tayari kuzikabili changamoto mbalimbali za maisha.

 Methali hii hutuonyesha ni kawaida mwanadamu kupatwa na dharura mbalimbali katika maisha ya kila siku. Mfano kupatwa na maradhi, ajali, au hata kifo. Pale unapokuwa na akiba uliyojiwekea itakusaidia wakati umepatwa na changamoto ya ghafla ambayo hukuitarajia.

 Faida nyingine ya kuweka akiba ni kuboresha maisha. Cha kwanza nashauri tuwe na utaratibu wa kuweka akiba mara kwa mara ili kuweza kuboresha maisha yetu kwa ujumla. Tunavyozidi kuweka akiba ndivyo ambavyo akiba hiyo inaweza kutusaidia kuboresha makazi yetu na miundombinu kwa ujumla ndani ya jamii zetu. Mfano mzuri ni wazazi ambao akiba wanazoziweka huwasaidia kulipa karo za shule pamoja na kununua vifa mbalimbali vya shulena hata gharama zingine zinazojitokeza kwa wakati huo.

 Methali hii pia inatukumbusha kuwa kadri tunavyozidi kuweka akiba ndivyo tunavyokuza hazina yetu. Swa na ile methali inayosema “ Haba na haba hujaza kibaba” ukichambua methali hizi zinaendana maana na utagundua ni ukumbusho mkubwa kwetu kuhusu ujenzi wa hatma njema ya jamii yetu ya sasa na baadae. Kwa kuwa zinatuhimiza kuwekeza kwa kila chumo tulipatalo. Tunakuza hazina kwa kuwa kile tunachoweka akiba kipo kwaajili yetu.

 Chukua nafasi kujiuliza, ni mara ngapi umepatwa na changamoto na akiba ndiyo ikaokoa jahazi, ni mambo mangapi yametokea bila taarifa na akiba ndiyo imetumika kuweka mambo sawa. Naamini sote tunapaswa kuweka akiba bila kujali kipato ni kikubwa au kidogo. Mfano unaweza kuanza kuweka akiba kidogo kidogo kutokana na kile unachokipata na kufikia muda Fulani utakuwa na akiba kubwa.

 Vilevile methali hii inasaidia kukuza maarifa kwa mtu mmoja mmoja na jamii hasa pale ambapo pamekuwepo na tofauti ya uhifadhi wa akiba kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Hapo zamani tunaambiwa watu walikuwa wanahifadhi akiba zao kwa kuchimba chini ya ardhi, kuweka chini ya kitanda au hata sehemu zingine ambazo wao waliamini ni salama. Leo hii watu hawatumii sana njia za kienyeji kuweka akiba zao. Ukija kwenye fedha zipo benki zenye mifumo thabiti na salama katika kuhifadhi fedha. Kwa upande wa akiba ya mazao pia zipo njia salama za kuhifadhi tena hata kwa muda mrefu bila kuharibika. Kwa hakika akiba haiozi.

 Waswahili tunasema “akiba haiozi”, “haba na haba hujaza kibaba” ikimaanisha kwamba akiba yaweza kuonekana ndogo ila kadri inavyoongezeka ndivyo inavyokuwa kubwa. Kinyume chake tunaambiwa “Chovya chovya humaliza buyu la asali”, “Bandu bandu humaliza gogo”. Tukikumbushwa kuwa vile tunavyochukua akiba zetu kidogo kidogo bila sababu ya msingi ndivyo ambavyo iko siku tutahamaki na kuona akiba imeisha bila kuona kitu cha maana kilichofanyika. Tukumbuke “mali bila daftari huisha bila habari”, tuangalie mfano wa shairi hili linalotusisitiza kuhusu kuweka akiba.

Akiba kweli hazina, haijawahi saliti,
Kwetu ni muhimu sana, hutubeba kwa nyakati,
Kipindi kweli hatuna, inasimama kwa dhati,
Sote tuweke akiba, akiba ni mkombozi.

 Kwa hakika ni dhahiri yatupasa kutunza vitu vyetu vizuri na rasilimali tulizonazo kwa kuweka akiba ili tuweze kujinusuru pale ambapo tunapokumbwa na changamoto za kushtukiza kwa ajili ya maisha yetu ya sasa na ya baadae.

Sources

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishinda nafasi ya pili 🥈 katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Rose Mwanri ni mwalimu Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Rose Mwanri
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org

Related on Maktaba.org 


Loading...
Loading...
Login to view and post comments

Do you have a big dream?

A dream too big for you to ever accomplish on your own? Maybe even too big to be accomplished in one generation?

Some gothic cathedrals in Europe took over 600 years -- more than 20 generations -- to complete! Although the Great Pyramid of Giza seems to have been built much faster (in a single generation), it also took tens of thousands of people.

In Tanzania, the Great Mosque of Kilwa was built in the 11th-14th centuries, rebuilt after earthquake damage, and continued to be remodeled up to the 18th century. It was described in the 1300s by Ibn Battuta. (You can take a 3D virtual tour of Kilwa! Check out the link in sources.)

The wonders of the world, modern and ancient, began as big dreams, dreams that took many generations to fulfill. Each generation continued the work of the past and also contributed to revising the blueprints for the future.

So if you are trying to do something great -- something that will really change the world -- don't expect to do it in one day. And don't try to do it alone. 

Related proverbs:


 Swahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako
If you want to go fast, go alone, if you want to go far, go together 

French:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
from Li Proverbe au Vilain, published around 1190
Modern French: Rome ne s'est pas faite en un jour
Rome wasn't built in a day

Chinese:
冰凍三尺,非一日之寒
Three feet of ice is not the result of one cold day

Scottish Gaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
It is not with the first strike that the tree will fall
...

Image credit: Screenshot from 3D virtual tour of Kilwa Kisiwani created by Zamani Project

Updated 4mo ago
by
What one person throws away may be useful and valuable to someone else.

This saying is often used to describe either the diversity of human preferences or to express optimism that humans are quite creative when it comes to repurposing or recycling what other people throw away.

For example, entrepreneur Gibson Kiwago, founder of WAGA Tanzania, recycles old laptop batteries to power homes and businesses in Tanzanzia. Check out our E-Waste Reading List!

The notion that people subjectively assess quality has been around a long time. The saying derives from a 17th century proverb:
One man's meat is another man's poison.

Have you ever seen value in something that someone else threw away?
...
Updated 4mo ago
by
Compare this simple, humble basket of fruit with a bag of lollipops. The fruit is ripe, juicy, packed full of vitamins -- it just sells itself. The lollipops, on the other hand, scream for our attention with explosive slogans and neon colors. But underneath the shiny packaging, it's really just plain sugar with some food coloring and artificial flavors.

Like other primates, humans find fruit attractive because it gives us energy and nutrition. Candy gives us energy, but it doesn't give us real nutrition. It just does a very clever job pretending to be fruit. Don't fall for it!

A good thing doesn't need to advertise, because quality speaks for itself. As the economists would say, demand exceeds supply.  Many advertisements seems to promise us happiness, beauty, love, wealth or respect. But ask yourself, does the ad promise more than the product can really deliver? Coca-Cola isn't a love potion.

This proverb reminds us of the enduring value of true quality and competence over flashy appearances. It's often used to express skepticism about a person who brags or praises themselves excessively.

We should all strive to be more like the basket of fruit: simple, authentic and good. These qualities will draw other people to you — at least the kind of people who understand that “chema chajiuza, kibaya chajitembeza

Related proverbs:
Don't judge a book by its cover.
Appearances are deceiving.
All that glitters is not gold 
 高嶺の花  Hana yori dango - Dumplings over flowers

...
Updated 4mo ago
by
Have you ever seen a blacksmith at work? Or maybe an artisan shaping hot glass? It's pretty incredible to watch, right? (If not, visit Shanga Foundation in Arusha or check out video links below)
In our everyday experience, glass is hard, brittle and breakable, but glass is actually made by melting sand and shaping it like liquid.

Some things in life seem unchangeable; they just will not bend. If we use all our strength, they only shatter in our hands and hurt us. But a skillful craftsman can make brittle things soft and malleable by preparing them appropriately, and taking decisive action at the right moment.

This proverb is often used to mean that you should take action quickly when an opportunity arises, so that you don't miss it. See also: There is a tide
 There is a tide in the affairs of men,
 Which, taken at the flood, leads on to fortune;
 Omitted, all the voyage of their life
 Is bound in shallows and in miseries.
- Brutus in Julius Caesar, Act 4, Scene 3 by William Shakespeare
However, it's worth noting that in the play, this advice has pretty bad consequences for Brutus, who didn't exactly sail on to fortune after this speech (read more...)

Many cultures and languages have a proverb that is very similar to "Strike while the iron is hot." It seems likely that the proverb has multiple independent origins.
Chinese: 趁熱打鐵
Thai: ตีเหล็กเมื่อแดง
Hindi: लोहा गरम हैं. मार दो हथौड़ा.
Irish: buail an t-iarann te
Swahili: Fua chuma wakati kingali moto

...

Image: Elimu Yetu teachers visit to Shanga Foundation, Arusha, Tanzania

Updated 4mo ago
by