You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs
Mchumia juani, hulia kivulini
Join
or login
to VOTE
Votes
59
View this proverb in English
Work in the sun, eat in the shade
na Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥉 Mshindi wa Tatu
Ni mara ngapi umesikia Mchumia juani hulia kivulini? Hii ni methali ya kiswahili (kibantu) yenye maana ya kuwatia moyo watu katika shughuli mbalimbali wanazozifanya Kila siku wawe na Imani kuwa ipo siku watayafurahia matunda ya kazi yao. 

Methali hii huwapa watu nguvu, bidii, moyo, ujasiri, tumaini na weledi katika kufanya kazi. Mfanyakazi huamini kuwa baada ya kazi ngumu zenye surubu basi huleta mavuno mazuri yenye kumfanya astareheke kivulini akila matunda ya kazi yake. Shairi lifuatalo linaonesha kwa namna gani mchumia juani huwa katika majukumu ya Kila siku.

Siogopi jua wala mvua, nikiitengeneza kesho yangu
Siogopi maumivu Wala majeraha, maana yote ni ya muda
Jua kali na kazi ndiyo desturi yangu, ili kheri kuja maishani
Machinga,mkulima, makuli na mvuvi wao na jua, Ili kuitafuta kesho
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Ni mchana jua la utosi, kichwani nina mavuno, jasho linatiririka
Jua limezama Sasa kasia ufukweni, hoi kitandani, nyavu zi baharini
Nyumbani mtaa wa nne, nahodha wa familia surubu nivute  kheri
Jua Sasa la chomoza, Kiguu na njia kulitafuta tonge
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.

Bwana mmoja alikuwa mkulima. Maisha yake yote alitumia katika kilimo. Hivyo kupendeza kwake kulikuwa mara chache. Watu kijijini kwake walimuita mkulima stadi. Alijenga nyumba kwa kuuza sehemu ya mazao yake, alisomesha wanae kwa kilimo.

Bwana huyu alikuwa mtu mwenye bidii alijifunza siku zote kanuni za mkulima bora, hivyo kadri muda unavyokwenda mashamba yake alivuna mazao mengi. Watu wengi walistaajabu sana kuona mabadiliko makubwa ndani ya familia yake. Aliwekeza vitu vingi kijijini kwake, mashamba, nyumba, maduka na mifugo mingi vilitoka shambani.

Watu wengi walikuja kujichukulia hekima kwa mkulima stadi. Siku zote aliwaambia "Mchumia juani, hulia kivulini. Jembe limeniheshimisha kijijini Mimi na familia yangu. Maisha yangu sasa yanakwenda barabara kwa hakika niko kivulini nafurahia matunda ya kazi yangu ya juani. Mimi leo kijana wa mkulima huyo stadi najivunia malezi, uwajibikaji wake kwa sababu kazi za juani leo zimetufanya tupumzike na kula kivulini. Kwa hakika maana ya mchumia juani inaonekana kwa vitendo. Bidii yako ndilo jua lako na kivuli ndiyo matunda ya bidii yako.

Hadithi hii inashibishwa na hadithi ilee ya "Mabala the Farmer" yaani Mabala Mkulima iliyoandikwa na Richard S. Mabala(1989). 

Mabala alikuwa mfanyakazi bandarini Kisha akapunguzwa hivyo akachagua kurudi kijijini Morogoro. Mabala alikuwa mzembe,mlevi na mbishi. Mabala alikwenda shambani na galoni ya pombe alikunywa na kulala, alipoamka alimwongelesha mkewe lakni hakujibiwa zaidi ya  sauti ya jembe tik-tok, tik-tok .

Mabala alikuwa mbishi, alimwagilia sukari shambani alifikiri ni mbolea, lakni mwisho alibadilika na kuwa mkulima stadi akawa mchumia juani ili familia yake ije kulia kivulini. Je wewe unahisi Mabala ni mchumia juani? Ndani ya familia au kwenye jamii mkulima stadi anakupa picha gani?

Mwisho hadithi hii kutoka katika methali ya mchumia juani hulia kivulini hutuonyesha dira njema katika kila tunachokifanya katika maisha ya kila siku. Huku methali kama Subira yavuta kheri, Mgaa na Upwa hali wali mkavu zote hufanana kimaudhui, zipo katika kuipa jamii nguvu na matumaini kwa kila jambo lifanyikalo katika malengo.
Sources

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishinda nafasi ya tatu 🥉 katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Magreth Lazaro Mafie ni mwanafunzi Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Magreth Lazaro Mafie
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org

The original essay included the following image, which is not included in the Creative Commons license.
Mchoro huu na / This image from: Honey Bee Arts - YouTube


Loading...
Loading...
Login to view and post comments

Ufafanuzi


Methali hii ya Kiingereza inatafsirika pia kama "Kalamu ina nguvu kuliko upanga au jambia" au " Kalamu ni kali kuliko upanga." Katika methali hii, jambia au upanga unaashiria nguvu na ukatili, na maana ya kalamu ni maneno. Ingawa upanga unaweza kushinda kwa nguvu, kalamu inaweza kuwashawishi, kuwahamasisha, na kuwaelimisha watu. Sio kila mtu ana silaha za kuwalazimisha watu wengine kufanya kile anachotaka, lakini kila mtu ana uwezo wa kubadilisha ulimwengu kupitia kile anachofikiria, kusema na kuandika kwa maneno. 

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
 - Methali ya Kiswahili

Methali hii ni kweli kwa sababu mara nyingi maneno huchochea na kudhibiti jinsi watu wanavyotumia nguvu na silaha zao. Kwa mfano, kupitia sheria, maneno ya viongozi, mahakimu na majaji yana uwezo wa kuwafunga watu gerezani au hata kuwaua. Kutoa hotuba ya moto kwa umati wa watu wenye hasira kunaweza kuleta ghasia kali na madhara mengine (ona Juliasi Kaizari).

"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)

Lakini pia, methali hiyo inatukumbusha nguvu ya upinzani usio na vurugu kwenye kuleta mabadiliko ya kudumu, kanuni iliyotetewa na kuonyeshwa na watu kama Mahatma Gandhi, Martin Luther King, na Nelson Mandela.  Angalia pia: Insha ya "Civil Disobedience"  na Henry David Thoreau, pamoja na Tamthilia mashuhuri ya "Antigone" na Sophocles.

Chimbuko


Nukuu hii ya "kalamu ina nguvu kuliko upanga" ilipata umaarufu kupitia tamthilia ya "Richelieu: au The Conspiracy"  na Edward Bulwer-Lytton (mwaka wa 1839, ukurasa wa 47). Lakini hakika wazo lilikuwepo kabla.

Wengine wanasema chimbuko halisi la methali hii ni Hadithi ya Ahikar. Kitabu hiki kiliandikwa takriban miaka 600 kabla ya kristu, na ni chimbuko la methali zingine kama "Ndege mkononi ana thamani ya wawili mtini"). Katika toleo letu, mfasiri hakuweza kusoma maandishi kutokana na hali ya karatasi, na maneno yalikatika. (Ukurasa 171/274
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na  ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa  ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Je, hili ndilo chimbuko halisi la methali hii, miaka zaidi ya 2,500 iliyopita? Muwe majaji...

Chanzo karibu na methali hii pia kinaonekana katika Agano la Kale:
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia

Na vilevile katika Shakespeare: 
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)

 Je, unakubali kalamu hushinda jambia? Toa maoni yako hapo chini!
...

CC BY Unaruhusiwa kunakili & kusambaza mchoro huu na makala hii bila idhini, ukitaja tu chanzo (www.maktaba.org)

Updated 4mo ago
by
Meaning it's better to be satisfied with what you have, rather than risking it for a chance at a larger reward.

This proverb turns out to be very old indeed. It comes from an ancient book called "The Story of Ahikar" also known as the "Proverbs of Ahiqar." 
My son, a sheep's foot in thine own hand is better than the whole shoulder in the hand of a stranger; better is a lambkin near thee than an ox far away; better is a sparrow held tight in the hand than a thousand birds flying about in the air; better is a hempen robe, that thou hast, than a robe of purple, that thou hast not.
The Story of Ahikar (page 110)
The book tells the story of an advisor to the ancient Assyrian and Egyptian rulers. It was probably written about 600 BCE, with the earliest surviving fragments dating to about 500 CE. 

Similar proverbs from around the world...
French:
Un tiens vaut mieux que deux tu l'auras
A here-you-go is worth more than two you-can-have-it-laters
Japanese
明日の百より今日の五十
Today's 50 over tomorrow's 100
Italian
Meglio un uovo oggi che una gallina domani
Better an egg today than a hen tomorrow

And one more for fun...
"A monkey on the back is worth two in the bush."
-ChatGPT

Do you think this proverb is good advice? When is it better to go with a sure thing now or take a chance and search for something better?
...
Updated 4mo ago
by
That which draws our attention, gets more attention. 

A wheel that makes noise is more likely to receive oil than other wheels (that also might need oil). We have limited attention, and thus we give our attention to people, projects and problems that stand out. This proverb asserts that there is not necessarily a correlation between the things we give our attention to and the things that actually need our attention.

Another version of the proverb is "the squeaky wheel gets the grease," and though the origin is unknown, American humorist Josh Billings is commonly attributed through his poem "The Kicker" in 1870
I hate to be a kicker,

I always long for peace,

But the wheel that squeaks the loudest,

Is the one that gets the grease.
 
...
Updated 4mo ago
by
This proverb means that we often get treated the same way we treat others. It is usually negatively, as a warning, or when a person who acted immorally gets their comeuppance. It could also be used as a promise of blessings to those who do good.  A third possible meaning is that Often compared to the Hindu doctrine of karma, the exact origin of the proverb is uncertain, but it seems to have emerged in the US in middle of the last century.

Related proverbs and quotes:
Shakespeare 
We still have judgment here; that we but teach
Bloody instructions, which, being taught, return
To plague the inventor: this even-handed justice
Commends the ingredients of our poison'd chalice
To our own lips.  (Macbeth Act I, Scene 7
Bible:
As you sow, so shall you reap (Galatians 6:7)
Chinese:
善有善報,惡有惡報
Good is rewarded with good, and evil with evil.
German
Wie man in den Wald hineinruft, so schallt es heraus
What you shout into the forest, will echo out again

...
Updated 4mo ago
by