You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Mshindi hufaidi yote

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 6mo ago
by
View this proverb in English
To the victor go the spoils
Methali hii ya Kiingereza "To the victor go the spoils" inatafsirika pia kama "Mshindi ndiye anayechukua vyote" au "Mshindi hupokea nyara zote."

Mshindi wa shindano ndiye anayepokea tuzo. Huwa anachukua asilimia kubwa ya faida ama faida zote, na hata manufaa zaidi ya yale yaliyokuwa yakipiganiwa.

Katika vita, nyara zinaweza kuwa ardhi, mamlaka au rasilimali nyingine zinazotafutwa. Katika shughuli zingine nyara zinaweza kuwa sifa, pesa au fursa. Methali hii hutumika ili kueleza matokeo yasiyo sawa au kutukumbusha kwamba katika migogoro mingi ni mshindi ndiye atakayechukua yote, asilimia kubwa, au angalau, kupendelewa. Angalia sehemu ya vyanzo kwa maelezo ya muktadha kuhusu chimbuko la methali hii, mwanasiasa wa Marekani katika miaka ya 1830 (Kiingereza).
Sources
https://en.wiktionary.org/wiki/to_the_victor_go_the_spoils

Tafsiri kutoka: https://twitter.com/mariastsehai/status/840801851352199170

William Marcy, a US senator in the 1830s said "To the victor belong the spoils of the enemy," during a speech defending Secretary of State Martin Van Buren from an attack by Senator Henry Clay.
During debate on Van Buren’s nomination as Minister to England
His statement contributed to him being known as an advocate of the "spoils system," which refers to appointing friends and political supporters to positions of power.

Marcy later became governor of New York (1833–39), Secretary of War (under President James K. Polk, 1845-1849) and Secretary of State under President Franklin Pierce (1853–57).

As Secretary of State Marcy helped purchase southern Arizona and southern New Mexico from Mexico in exchange for $10 million. Occurring on December 30, 1853, the deal is known in US history as the Gadsen purchase, or in Mexican history as the sale of the Mesilla Valley (or the Treaty of La Mesilla), which was a negotiated by US minister to Mexico James Gadsen following the conquest of northern Mexico by the United States in 1848. The dispute was encouraged by US advocates of a southern transcontinental railroad. Residents of the territory were to receive the same protections detailed in the Treaty of Guadalupe Hidalgo (1848) which offered US citizenship and civil rights to those living in the newly acquired territory.

18 February 1832, Frederick (MD) Town Herald, pg. 2: (source)
Mr. Marcy, a senator from New York, in the discussion on Mr. Van Buren's appointment as Ministor to England (by Andrew Jackson), plainly avowed the creed of his party.
"It may be that the politicians of the United States (a mistake in the print we presume for the state of New York) are not so fastidious as some gentlemen are, as to disclosing the principles on which they act. They boldly preach what they practice. When they are contending for victory, they avow the intention of enjoying the fruits of it. If they are defeated, they expect to retire from office -- IF THEY ARE SUCCESSFUL, THEY CLAIM, AS A MATTER OF RIGHT THE ADVANTAGES OF SUCCESS. THEY SEE NOTHING WRONG IN THE RULE, THAT TO THE VICTOR BELONGS THE SPOILS OF THE ENEMY.

Brown University has additional history of William Marcy who graduated from Brown in 1808.

Loading...
Loading...
Login to view and post comments
It’s a simple and profound truth about human relationships: Making a promise means creating an expectation in others. When we fail to keep our promises, we damage our relationships and our reputation. Next time you make a promise, ask yourself, "Would I sign a contract that said this?"

French
Chose promise, chose due 
A thing promised is a thing owed. 
Russian:
Долг платежом красен, а займы отдачею. 
The beauty of a debt is its payment 
Alternative translation: A debt is beautiful when it is paid off, and loans when repaid.
Latin:
Pacta sunt servanda
Agreements must be kept (an important principle of international law)
Chinese
口說無憑
Spoken words are no guarantee.
English
Your word is your bond

What do you think? Is a promise as strong as a contract?
...
Updated 6mo ago
by
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
...
Habari zenu wapenzi wa lugha na hekima! Karibuni tena katika kipindi chetu cha leo cha Methali! Methali ya leo ni “Mtoto akilia wembe, mpe.” Je, unaijua? Kwa walezi wengi, inaweza kuonewa… kali sana, au sivyo? Ina maana gani kwako? Je, unakubaliana nayo? Tushirikiane mawazo. 

Nikisikia nitasahau, nikiona nitakumbuka, nikifanya nitaelewa.
-Mwalimu Amos 

Mtoto akitaka wembe, basi mpe ili aelewe kwanini alionywa dhidi ya kucheza nao. Methali hii inaonyesha umuhimu wa kuwapa watu nafasi za kujifunza kutokana na uzoefu wao wenyewe, hata kama wanaweza kuumiwa (kidogo). Vilevile, hata ukikataa kumpa, labda hatatiii na atacheza nao ukiwa nje. Methali hii inaweza kutumika pia kama onyo kwa mtu anayepuuza ushauri au kusisitiza njia yake. Ingawa ni muhimu kusikiliza ushauri na maonyo kutoka kwa wengine, wakati mwingine tunahitaji kuona matokeo ya vitendo vyetu wenyewe ili kuelewa madhara yake. 

Adhabu ya Asili  (Natural Consequences)

Katika eneo la malezi, methali hii inafundisha kanuni ya Natural Consequences (Adhabu Halisi au Adhabu ya Asili). Adhabu ya asili ni matokeo yatakayokuja kwa sababu ya tabia ya mtoto mwenyewe. Tofauti na adhabu ya kutolewa au adhabu ya viboko, adhabu ya asili hujitokeza bila mlezi kujiingilia. Kwa mfano, fikiria kama mwanako amesahau daftari yake nyumbani. Ungefanyaje? Wazazi wengine wanajibu “Singefanya chochote, maana atahitaji kueleza kwa mwalimu wake.” Wengine wanasema “Ningekimbia shuleni ili kumletea daftari, halafu jioni ningempa adhabu.” Ipi bora?  Jibuni hapo chini… 

Swali: Je, mtoto akilia nyoka utampa?

Sawa tumekubaliana mtoto akilia wembe, mpe. Lakini… fikiria kama mtoto analia kitu cha hatari zaidi— je utakubali? Yesu aliwauliza wazazi: “Mtoto akiomba samaki, je, atampa nyoka?” Akilia nyoka, utampa? Wembe unaweza kusababisha jeraha ndogo, lakini si hatari sana kama nyoka mwenye sumu. 
Wewe kama mzazi, utakubali kiasi gani cha hatari ili ajifunze mwenyewe? Kama anaomba kuacha masomo ili kucheza michezo za simu sikuzote? Kama anaomba kumwoa/kumwolewa na mtu ambaye haumwamini katika umri mdogo? Yaani pia kuna maamuzi muhimu ambayo watoto hawako tayari kujifanyia. 
Je wewe kama mzazi unawezaje kuamua au kutambua kama unapaswa kumwokoa / kumlinda mwanako, ama kama unapaswa kumwachia afunzwe na ulimwengu? Wazazi na walezi wote tunaomba maoni yenu!

Nyoka ana madhara.
-Mwalimu Shila  

Utekelezaji wa methali hii katika maisha ya kila siku

Elimu: Watu hukumbuka walichojifunza kwa vitendo kuliko walichoambiwa kwa maneno. Utafute nafasi za kutekeleza kile unachojifunza.
Malezi: Mpe mtoto uhuru na nafasi za kujifunza kupitia uzoefu. Usimtatulie kila jambo, na usiogope anapofeli, kama hakuna hatari wala madhara ya muda mrefu, maana kufeli ni nafasi ya kujifunza kwake.
Kusikiliza: Ukipuuza maonyo na shauri, usishangaye kuona madhara yaliyotabiriwa.
...

Picha hii imetengenezwa na akili bandia (AI)

Updated 6mo ago
by
na Nankya Sauda 🇺🇬
Shindano la Insha ya Methali 🏆
Mshindi wa Kwanza 🥇

Maji yaliyotulia ndiyo yenye kina kirefu

Umewahi kuchukua muda na kujiuliza kwa nini wazee huwa wana busara zaidi kuliko vijana? Je, umewahi kuchukua muda wa kutafakari asili yako ulipochipuka? Ikiwa sivyo, [sasa] ni wakati mzuri wa kuanza kutafuta asili yako kwa sababu ni muhimu mtu ajue mizizi yake.
   Baada ya muda, unachukua mzigo wa kufunua asili ya watu mashuhuri wenye akili na haiba zao, utakuja kutambua kwamba wao ni introverts (yaani wakimya, wanaopenda kukaa peke yao/kujitenga) lakini ni mashuhuri. Ni muhimu uchukue muda wako, hata ukiwa bize, ujifunze kuhusu wasomi mashuhuri kama Albert Einstein, mwanasayansi mashuhuri ambaye alisema nukuu inayotuelimisha:
"Maisha tulivu ya upweke yasiobadilikaa huchochea akili na fikra bunifu."

Hii inamaanisha kwamba wakati ukiwa peke yako ni nafasi ya kujitafakari, lakini pia ni nafasi ya kutumia akili yako bunifu. Wanasema wazungumzaji wakubwa ni wanasheria wazuri, na tumeona hayo katika maisha yetu ya kila siku ambapo watu hutoa ahadi tupu, hutoa matamko ya uwongo ili kuwapendeza waliomzunguka bila kuchukua muda wa kufanya kitu kwa nia ya kutekeleza maneno yao. Kwa sababu hiyo, wengi wamepoteza imani na hawa wanaoitwa “wazungumzaji wakubwa.”
   Kwa upande mwingine, wakimya hutushangaza kwa matendo yao. Hatua zao hupangiliwa kila mara, matamanio yao ni wazi na vitendo vyao hufanyika kwa kusudi. Wapenzi wakimya hukuza mahusiano yao ya kimapenzi kwa ubunifu mpya ili kudumisha mahusiano. Waliowaajiri [wakimya] na waliokaa karibu na introverts husema kuwafahamu ni moja ya mafanikio makubwa katika maisha yao, ndo maana hawa wamefanya kazi nadhifu zaidi, wakawa na vipindi vyao vya kutafakari peke yao, na hatimaye walitoa kazi bora na kupata cheo kikubwa.
   Tunaweza kufafanua methali kama misemo inatumika katika nchi au utamaduni fulani. Ni maneno mafupi yenye busara na hutoa ushauri na vile vile kuongeza wazo kuhusiana na maisha ya kila siku. Kwa kweli, ili kufahamu kwa kina mila na desturi za kitamaduni, ni vizuri warejelee methali kwani zinaweza kuwa na maana pana ndani. 
Kihistoria, methali "Still waters run deep" (Maji yalotulia ndo yenye kina kirefu/Usicheze maji yanayosimama) inatoka Kilatini cha kale. Ilipata umaarufu baada ya Shakespeare kuitumia katika tamthilia yake ya Henry VI mwaka 1590. Alisema:
"Maji hutulia pale ambapo mto una kina kirefu."

Tunatambua kwamba, mara nyingi watu hatari zaidi walio na roho mbaya hupanga hatua zao na kuchukua hatua kwa wakati ambao wengine hatarajii. Ndio maana usaliti hutoka kwa watu ambao hatutarajii [kitu kama hicho] kutoka kwao. Kwa hiyo ni muhimu kwa mtu kuchukua si tu yale yanayokutana na macho bali pia kuchukua tahadhari hasa kutoka kwa watu ambao hawalipizi kisasi mara tu baada ya kukasirishwa au kukabiliwa.
   Albert Einstein licha ya tabia yake ya kujittenga, yeye anajulikana sana kwa kubuni nadharia yake ya relativity ambayo ilileta mapinduzi katika uelewa wetu wa nafasi ya nje, wakati, na kanimvutano (gravity).
   Kwa kumalizia, ni muhimu sana kutofikia hitimisho [haraka] kwa sababu sura hudanganya na kuna mengi ya kujua na kugundua kuliko macho yanavyoweza kuona.
...
Updated 6mo ago
by