We support the Pickleball community in Arusha, Tanzania
Play pickleball Learn more
Book a court Learn pickleball for FREE Hire a Pickleball coach
Posts / Proverbs Proverb of the day
SW

Usilolijua ni kama usiku wa giza

"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 

Related Posts

Don't count your chickens before they hatch means that you shouldn't depend on a favorable outcome until it is certain. You shouldn't assume that all your eggs will hatch into healthy chicks and grow into chickens. Do you have a story about this proverb? Share below!

The first written record of this common English proverb is a sonnet written in 1570 by Thomas Howell:
“Count not thy Chickens that unhatched be,
Weigh words as wind, till thou find certainty ”

Many languages have proverbs that convey a similar principle.

Swahili:
“Tujivune hatimaye. ”

Let's praise ourselves at the end.

French:
“Il ne faut pas vendre la peau de l’ours avant de l’avoir tué.”

Don't sell the skin of the bear before killing it.

Arabic:
“لا تشتري السمك وهو في البحر بل انتظر حتى يصطاد”

Do not buy a fish while it is in the sea; wait until it is caught.

German:
“Man soll den Tag nicht vor dem Abend loben.”

Don't praise the day before the evening.

Latin: 
“Ante victoriam ne canas triumphum”

Don't...

Read more...

This picture was created using AI. What do you think? What picture do you think would best illustrate this proverb?

Updated >1y ago
by

Methali hii ina maanisha hupaswi kutegemea matokeo mazuri kabla hayajatokea. Hupaswi kutegemea mayai yako yote yatakuwa vifaranga wenye afya nzuri. Je, una hadithi kuhusu methali hii? Toeni maoni!

Rekodi ya kwanza iliyoandikwa ya methali hii ya Kiingereza ni shairi iliyoandikwa mwaka wa 1570 na Thomas Howell:
“Usiwahesabu kuku wako ambao hawajaanguliwa,
Pima maneno kama upepo, hadi upate uhakika”

Lugha nyingi zina methali zinazofundisha kanuni karibu na hii. Mifano:

Kiswahili:
“Tujivune hatimaye.”

Kifaransa:
“Il ne faut pas vendre la peau de l'ours avant de l'avoir tué.”

Usiuze ngozi ya dubu kabla ya kumuua.

Kiarabu: 
“لا تشتري السمك وهو في البحر بل انتظر حتى يصطاد”

Usinunue samaki yumo baharini; subiri hadi itakapokamatwa.

Kijerumani:
“Man soll den Tag nicht vor dem Abend loben.”

Usisifu siku moja kabla ya jioni.

Kilatini:
“Ante victoram ne canas triumphum”

Usiimbe shangwe kabla ya ushindi.

Kireno:
“Não conte com o ovo dentro da galinha.”

Usihesabu yai ndani ya kuku.

Picha hii ilichorwa kwa kutumia Akili Bandia (AI). Mnafikiriaje? Toeni maoni!

Updated >1y ago
by

This Russian Proverb was quoted by Pushkin in the novel "The Daughter of the Commandant":
“My parents gave me their blessing, and my father said to me—
  "Good-bye, Petr'; serve faithfully he to whom you have sworn fidelity; obey your superiors; do not seek for favours; do not struggle after active service, but do not refuse it either, and remember the
proverb, 'Take care of your coat while it is new, and of your honour while it is young.'"
  My mother tearfully begged me not to neglect my health.”

Updated >1y ago
by

“When life gives you lemons, make lemonade” means that we should try to make the best out of difficult situations. Lemons are sour and bitter on their own, but by adding sugar and water turns sour lemons into a sweet refreshing drink. When life presents difficulties and challenges (lemons), we can be creative, resilient and flexible to transform these challenges into opportunities (lemonade).

Do you have a story about a time you turned a challenge into an opportunity? Do you know any other sayings that relate to the same principle? Comment below!
Here are some similar sayings from other cultures: 
“The impediment to action advances action. What stands in the way becomes the way.”

- Meditations by Marcus Aurelius

“ اِصْنَعْ شَرَابًا حَلُّوا مِنْ حَامِض لَيْمُون الْحَيَاةِ.”

“Make a sweet drink from the acid of the lemon of life. ”

-Arabic Proverb
“जब भी जीवन में मुश्किलें आएँ तो उनका भी लाभ उठाएँ”

“When difficulties come into life, take advantage of them too. ”

-Hindi...

Read more...

This picture was created using AI. What do you think? What picture do you think would best illustrate this proverb?

Updated >1y ago
by

"Maisha yakikupa limao, tengeneza juis" inamaanisha pale tunapokutana na changamoto, tunapaswa kujaribu kuzifanyia kazi  ili zibadilike kuwa fursa. Limao pekee ni chungu, lakini sukara na maji safi hugeuza limao chungu kuwa kinywaji kitamu cha kuburudisha. Maisha yanapoleta chungu na changamoto (limao), tunaweza kuwa wabunifu na wastahimilivu ili kubadilisha changamoto hizi kuwa fursa (juis).

Je, umewahi kubadilisha changamoto kuwa fursa?
Je! unajua misemo au mithani inayohusiana na kanuni hiyo hiyo?
Toeni maoni hapa chini!

Misemo inayohusiana kutoka kwa tamaduni mbalimbali:
Kizuizi cha hatua huendeleza hatua. Kinachosimama njiani kinakuwa njia.
- Tafakari za Marcus Aurelius (Roma ya Kale)
“اِصْنَعْ شَرَابًا حَلُّوا مِنْ حَامِض لَيْمُون الْحَيَاةِ”

“Tengeneza kinywaji kitamu kutoka kwa asidi ya limau ya maisha.”

-Methali ya Kiarabu 
“जब भी जीवन में मुश्किलें आएँ तो उनका भी लाभ उठाएँ
Matatizo yanapotokea, tumia fursa hiyo pia. ”

-Methali ya Kihindi

(Chanzo: Shukrani kwa...

Read more...

Picha hii iliundwa kwa kutumia Akili Bandia. Unafikiriaje? Je, picha gani ingefafanua methali hii vyema?

Updated >1y ago
by

Today's proverb "Haraka haraka haina baraka" literally translates to "Hurry hurry has no blessing"... but that doesn't rhyme, so we decided to go with "Haste makes waste." Which translation do you like better?  Have you ever rushed through something and regretted it later? Comment below... 

I see two possible interpretations of this proverb (in Swahili):
1. Patience: Hurry causes us to make mistakes, and those mistakes cause us to miss out on potential blessings.
2. Mindfulness: When we're in a hurry, we don't have time to notice or enjoy the blessings we have.  

What do you think? What's your interpretation?

Similar saying are common around the world:
Spanish: 
“No por mucho madrugar amanece más temprano
(Waking up early doesn't make the sun rise any sooner)”

Chinese: 
“欲速则不达
(Haste makes waste)”

From the Sayings of Confucius (Analects, 13:17, page 92)
“When Tsz-hiá became governor of Kü-fu, and consulted him about government, he answered, "Do not wish for speedy results. Do...

Read more...
Updated >1y ago
by

Methali ya leo ni "Haraka haraka haina baraka." Tafsiri yake kwa Kiingereza ni "Haste makes waste" au "Hurry hurry has no blessing" Mnaonaje - tafsiri ipi bora? Toeni maoni chini... 

Kwa upande wangu naona kwa mitazamo miwili. Methali hii inaweza kutufundisha:
1. Subira: Haraka husababisha makosa, na makosa hutuzuia baraka. (Nenda taratibu)
2. Mindfulness (yaani uwepo kiakili na utulivu): Tunapopoenda kwa haraka, hakuna muda wa kutambua, kutumia au kufurahia baraka tulizo nazo. 

Kuna misemo karibu na "haraka haraka haina baraka" katika nchi nyingi. Mifano: 
Kihispania: 
“No por mucho madrugar amanece más temprano
(Kuamka mapema hakufanyi jua kuchomoza mapema)”

Kifaransa: 
“Tout vient a point a qui sait attendre
(Everything comes to those who wait)”

Kiswahili:
“ Pole pole ndio mwendo ”

Kichina: 
“欲速则不达”

Methali hii ya Kichina ni karibu na "Haraka haraka haina baraka". Inatoka kitabu cha Misemo ya Konfusio (Analects, 13:17, ona ukurasa wa 92):
“Tsz-hiá alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa...

Read more...
Updated >1y ago
by

Today's proverb comes from the Ancient Greek myth of Icarus... and we wrote a short picture book about the story!

Download now:
Don't Fly Too Close to the Sun

"Don't fly too close to the sun" is a warning against hubris (excessive pride). The proverb teaches us that pride and ambition should be balanced with caution, humility and good advice.

For example, imagine a young entrepreneur. She launches her first product and has immediate success. Encouraged, she starts making more and more ambitious plans. She decides to take out a large loan from the bank in order to launch more products and buy property. But the sales growth she was expecting does not materialize, and she finds herself falling behind on the loan payments. In the end, the business sinks deeper and deeper into debt and can't recover. If she had steered a "middle path," building on her success with small, moderate steps, and listening to her mentors, things might have ended differently.

We can apply this proverb in...

Read more...
Updated >1y ago
by

Methali ya leo inatoka katika hadithi ya Ugiriki ya Kale ya Ikarus ... na tuliwaandikia kitabu kifupi cha picha kuhusu hadithi ya Ikarus...

Soma sasa: 
Usiruke Karibu Sana na Jua

"Usiruke karibu sana na jua" ni onyo dhidi ya kiburi. Methali hii inatufundisha kwamba kiburi na tamaa vinaweza kuleta madhara mabaya ukipuuza  tahadhari, unyenyekevu na ushauri mzuri.

Kwa mfano, fikiria mjasiriamali mdogo. Anazindua bidhaa yake ya kwanza na anapata mafanikio ya haraka. Akiwa ametiwa moyo, anaanza kuweka mipango kabambe zaidi na zaidi. Anaamua kuomba mkopo mkubwa wa benki ili kuzindua bidhaa zaidi na kununua vifaa, mali na ardhi. Lakini ukuaji wa mauzo aliokuwa akitarajia haujitokezi, na anajikuta akichelewa na malipo ya mkopo. Hatimaye, biashara inazidi kuzama kwenye deni. Angeenda "njia ya kati," yaani kujenga mafanikio yake kwa hatua nyingi ndogo, na kusikiliza maonyo ya washauri wake, mambo yangeenda vizuri zaidi.

Tunaweza kutumia methali hii katika maisha yetu ya kila siku kwa...

Read more...
Updated >1y ago
by

Today's proverb means that people who are excessively proud are likely to fail. Success can make us overconfident, causing mistakes. Pride and ego can also blind us to our limitations and prevent us from seeing reality clearly.

On the other hand, in the modern world, many people see confidence and self-esteem as positive virtues. What is the difference between healthy and unhealthy pride? Share your thoughts below!

This proverb is often associated with the story of Icarus, from Greek mythology. (Spoiler alert for those who haven't check out our new picture book, "Don't Fly Too Close to the Sun"). Icarus was given wings made of feathers and wax by his father, Daedalus. He was warned not to fly too close to the sun, but Icarus ignored his father’s advice, proudly flying higher and higher. The sun melted the wax, and Icarus fell into the sea and drowned.

Just before the Titanic's maiden voyage the company's leader, Phillip Franklin, wrote:
“There is no danger that Titanic will...

Read more...

Image from the painting by Caspar David Friedrich, 1817, "Wanderer above the Sea of Fog / Der Wanderer über dem Nebelmeer"

Updated >1y ago
by
Play Tennis or Pickleball in Arusha, Tanzania

Your reservations contribute to supporting:

for kids, teens and adults in Arusha, Tanzania

and the maintenance and upkeep of the courts.

We recently built 3 new lighted pickleball courts in Arusha, Tanzania!

Are you traveling to Tanzania?

Learn Useful Phrases in English & Swahili

Master essential everyday phrases in both languages