You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Taarifa
Majadiliano
Methali

Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu

Ili kupiga KURA kwa Methali ya Mwezi
Kura
0
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by

Swali: Je, umejifunza zaidi kutoka kwa wazazi wako ama kupitia uzoefu wako ulimwenguni?


Methali hii hutumika wakati mtu amekosa na kupata madhara, haswa kama ameonywa... kama vile dereva wa lori katika picha hii (kutoka Oxfordshire, Uingereza). Bila kujali kama ulifunzwa na wazazi, hatimaye lazima ukabiliane na ukweli wa maisha halisi. Ona pia: Mtoto akilia wembe, mpe

Kuna shairi lililotungwa na Akilimali Snow-White juu ya methali hii:

ASOFUNZWA NA WAZAZI, HUFUNZWA NA ULIMWENGU
na Akilimali Snow-White

Zama walinipumbaza, wazee kwa kunilea,
Nikashindwa kujifunza, myendo mipya ya dunia,
Leo najipendekeza, kwa walimwengu sikia,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Kazi zote singeweza, bila kuwanyenyekea,
Kutii kuwembeleza, kisha kuwatumikia,
Hata nikawapendeza, wakanifunza kwa nia,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Sasa kusema naweza, Kizungu bila udhia,
Kama vile Kingereza, na lugha zingine pia,
Kwa juhudi najifunza, hata zimenielea,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Naweza kuzungumza, pasipo kutia doa,
Na paovu kuongoza, doa nikaliondoa,
Mwishowe pakapendeza, lingano moja hatua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Sina nilipopasaza, pasina kupachungua,
Pande zote hachunguza, marifa nikachukuwa,
Hata najua kuuza, bidhaa na kununua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Kiasi nilo jifunza, si haba kwa kubabia,
Nitokapo napendeza, kazi njema natumia,
Ni vigumu kuibeza, jinsi inanielea,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Haifai kupuuza, kwa kitu usicho jua,
Jaribu kupeleleza, na kisha ukichungua,
Nia unap,o ikaza, hushindwi kitu kujua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Kazi nilizojifunza, babangu hakuzijua,
Hakujua Kingereza, kuuza na kununua,
Bali kujipendekeza, ndipo mwana nikajua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Nawatilia nyongeza, mlio nisaidia,
Nyote mlionifunza, Rabi awape afia,
Mungu heri tawajaza, mema kuwarudishia,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

- Diwani ya Akilimali

Fikeni E. M. K. Senkoro (1988) aliandika juu ya shairi hili:
[M]tu hawezi kupata uzoefu wa mambo yote yahusuyo maisha kutoka kwa wazazi wake: lazima awe tayari kufunzwa na ulimwengu, yaani kujifunza kutoka kwa wengine zaidi ya baba na mama yake. 

Nimejitahidi kutafsiri shairi hili kwa Kiingereza, na nitashukuru sana sana kupata feedback zenu, ndugu wajuaji wa Kiswahili na Kiingereza. (Someni hapa.)

Mnafikiriaje? Shairi hili lina maana gani kwako? 
Marejeleo
Picha ni kweli, inaonyesha ajali iliyotokea Uingereza, mkoa wa Oxfordshire, (Pich kutoka mitandao ya kijamii) - Soma pia Makala hii ya BBC

Shairi lilitoka Diwani ya Akilimali

Nukuu ya mwisho inatoka kitabu cha "Ushairi - Nadharia na Tahakiki" na F.E.M.K. Senkoro, Sura ya 7 (Dar Es Salaam University Press, 1988, ISBN 9976 60 0224)  
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Kuna vitu ambavyo huwezi kufanya peke yako. Tango ni mchezo (densi) ya watu wawili, kwa hivyo huwezi kucheza tango peke yako.

Methali hii inatoka wimbo ulioimbwa 1952, It Takes Two to Tango:
Unaweza kusafiri kwa meli peke yako,
kulala au kupumzika peke yako.
Unaweza kuingia kwenye deni peke yako.
Kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya peke yako.
Lakini ni lazima muwe wawili ili kucheza tango, muwe wawili ili kucheza tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning na Pearl Bailey) Ona vyanzo/sources ili kusikiliza wimbo huu!

Methali hii ina maana nyingi tofauti ambazo unaweza kutekeleza katika mahusiano na maisha yako ya kila siku. Mambo mengi huhitaji watu zaidi ya mmoja: Wawili wanatakiwa ili kushirikiana, kufanya biashara ama kupigana. Ukitaka kucheza na mtu ambaye hataki kucheza na wewe, bora kumtafuta mchezaji mwengine.. Vivyo hivyo, ukiwa kwenye mgogoro au magomvi, itabidi ufikirie jinsi tabia yako inavyoweza kuchangia katika kuendeleza shida. katika dance, lengo si kuwa mkamilifu, bali ni kuendana na mwenzako na kufurahia pamoja.
Methali zinazofanana kutoka Afrika: 
Kimisri (Kiarabu): 
ايد لوحدها ماتسقفش‎
Mkono mmoja hauwezi kupiga makofi
Kiswahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Kidole kimoja hakiuwi chawa
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
na Nankya Sauda 🇺🇬
Shindano la Insha ya Methali 🏆
Mshindi wa Kwanza 🥇

Maji yaliyotulia ndiyo yenye kina kirefu

Umewahi kuchukua muda na kujiuliza kwa nini wazee huwa wana busara zaidi kuliko vijana? Je, umewahi kuchukua muda wa kutafakari asili yako ulipochipuka? Ikiwa sivyo, [sasa] ni wakati mzuri wa kuanza kutafuta asili yako kwa sababu ni muhimu mtu ajue mizizi yake.
   Baada ya muda, unachukua mzigo wa kufunua asili ya watu mashuhuri wenye akili na haiba zao, utakuja kutambua kwamba wao ni introverts (yaani wakimya, wanaopenda kukaa peke yao/kujitenga) lakini ni mashuhuri. Ni muhimu uchukue muda wako, hata ukiwa bize, ujifunze kuhusu wasomi mashuhuri kama Albert Einstein, mwanasayansi mashuhuri ambaye alisema nukuu inayotuelimisha:
"Maisha tulivu ya upweke yasiobadilikaa huchochea akili na fikra bunifu."

Hii inamaanisha kwamba wakati ukiwa peke yako ni nafasi ya kujitafakari, lakini pia ni nafasi ya kutumia akili yako bunifu. Wanasema wazungumzaji wakubwa ni wanasheria wazuri, na tumeona hayo katika maisha yetu ya kila siku ambapo watu hutoa ahadi tupu, hutoa matamko ya uwongo ili kuwapendeza waliomzunguka bila kuchukua muda wa kufanya kitu kwa nia ya kutekeleza maneno yao. Kwa sababu hiyo, wengi wamepoteza imani na hawa wanaoitwa “wazungumzaji wakubwa.”
   Kwa upande mwingine, wakimya hutushangaza kwa matendo yao. Hatua zao hupangiliwa kila mara, matamanio yao ni wazi na vitendo vyao hufanyika kwa kusudi. Wapenzi wakimya hukuza mahusiano yao ya kimapenzi kwa ubunifu mpya ili kudumisha mahusiano. Waliowaajiri [wakimya] na waliokaa karibu na introverts husema kuwafahamu ni moja ya mafanikio makubwa katika maisha yao, ndo maana hawa wamefanya kazi nadhifu zaidi, wakawa na vipindi vyao vya kutafakari peke yao, na hatimaye walitoa kazi bora na kupata cheo kikubwa.
   Tunaweza kufafanua methali kama misemo inatumika katika nchi au utamaduni fulani. Ni maneno mafupi yenye busara na hutoa ushauri na vile vile kuongeza wazo kuhusiana na maisha ya kila siku. Kwa kweli, ili kufahamu kwa kina mila na desturi za kitamaduni, ni vizuri warejelee methali kwani zinaweza kuwa na maana pana ndani. 
Kihistoria, methali "Still waters run deep" (Maji yalotulia ndo yenye kina kirefu/Usicheze maji yanayosimama) inatoka Kilatini cha kale. Ilipata umaarufu baada ya Shakespeare kuitumia katika tamthilia yake ya Henry VI mwaka 1590. Alisema:
"Maji hutulia pale ambapo mto una kina kirefu."

Tunatambua kwamba, mara nyingi watu hatari zaidi walio na roho mbaya hupanga hatua zao na kuchukua hatua kwa wakati ambao wengine hatarajii. Ndio maana usaliti hutoka kwa watu ambao hatutarajii [kitu kama hicho] kutoka kwao. Kwa hiyo ni muhimu kwa mtu kuchukua si tu yale yanayokutana na macho bali pia kuchukua tahadhari hasa kutoka kwa watu ambao hawalipizi kisasi mara tu baada ya kukasirishwa au kukabiliwa.
   Albert Einstein licha ya tabia yake ya kujittenga, yeye anajulikana sana kwa kubuni nadharia yake ya relativity ambayo ilileta mapinduzi katika uelewa wetu wa nafasi ya nje, wakati, na kanimvutano (gravity).
   Kwa kumalizia, ni muhimu sana kutofikia hitimisho [haraka] kwa sababu sura hudanganya na kuna mengi ya kujua na kugundua kuliko macho yanavyoweza kuona.
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
by Rose Mwanri 🇹🇿 
🏆 Proverb Essay Contest 
🥈 Second Place Winner
A proverb is a metaphorical expression used in a community. Words in proverbs have additional meanings and proverbs have two sides. The first side gives an idea and the second side completes the idea. Akiba haiozi (Savings do not decay) is one of the Swahili proverbs that is widely used in African communities and by Kiswahili speakers globally, with the aim of reminding people about the importance of saving.

The purpose of this proverb is to encourage us as members of the community to prepare well for today's life as well as tomorrow so we are ready to face the various challenges of life.

This proverb shows us that it is normal for a human being to experience various emergencies in everyday life. For example, an illness, accident, or even death. When you have the savings that you have set aside, it will help you when you are faced with a sudden challenge that you did not expect.

Another benefit of saving is improving life. First of all, I advise we all have a regular savings plan to be able to improve our lives in general. The more we save, the more that savings can help us improve our housing and infrastructure within our communities. A good example is parents whose savings enable them to pay for school fees, supplies and even other expenses that may arise at the same time.

This proverb also reminds us that the more we save, the more we grow our treasury. As with the proverb that says "Haba and haba hujaza kibaba" (little by little fills up the measure). If you analyze these proverbs, they have the same meaning, and you will find that it is a great reminder about building a good fate for our community, now and later. [These proverbs] encourage us to invest every penny we get. We grow our treasury, because what we save is there for us.

Take the opportunity to ask yourself, how many times have you faced challenges and your savings kept the ship afloat? How many issues have arisen without notice that you used your savings to put things right? I believe we should all save regardless of whether our income is big or small. For example, you can start saving little by little from what you earn and in time your savings will add up to be big.

Also, this proverb helps to develop knowledge for individuals and communities, especially where there has been a difference in savings from one generation to another. In the past we are told that people used to store their savings by digging underground, putting under the bed or even other places that they believed were safe. Today, people do not use traditional methods to save their savings. When it comes to money, there are banks with stable and safe systems for storing money. In terms of crop saving, there are also safe ways to store crops, even for a long time, without spoiling. In fact, savings do not decay.

In Swahili, we say “Akiba haizoi” ("Savings don't rot"), “Haba na haba hujaza kibaba” (“Little by little fills up the measure") meaning that the savings may seem small but the more they increase, the bigger they become. On the contrary, we are told “Chovya chovya humaliza buyu la asali” (“Dip [by] dip finishes the jar of honey”), “Bandu bandu humaliza gogo” (“Chop [by] chop finishes the log.”) If we take from our savings little by little without a good reason, the day will come when we’re infuriated to see all the savings are gone without anything meaningful getting done. Let's remember “mali bila daftari huisha bila habari” ("Wealth without a notebook disappears without notice"). Let's look at an example of this poem that stresses us about saving.

  Savings are truly a treasure, they never betray,
  For us it’s very important, they carries us through times
  When we really have nothing, they stand sincerely,
  Let's all save, savings is a savior.

Truly, it’s clear that we should take care of the good things and the resources we have by saving, so that we can save ourselves when we are faced with surprising challenges in our present and future lives.
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Have you ever noticed that time seems to pass more slowly when you are waiting for something? On the other hand, if you distract yourself with other engaging activities, time goes by quickly.

For example, if you're in a waiting room for a doctor, the wait will seem shorter if you check your phone or read a magazine, rather than just waiting for your name being called.

This proverb was attributed by Benjamin Franklin to Poor Richard's Almanac, however it doesn't actually appear there. Instead, Franklin used it in an essay on animal magnetism in 1785.

I was very Hungry; it was so late; “a watched pot is slow to boil,” as Poor Richard says.

...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by