You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Taarifa
Majadiliano
Methali

Kama hujui kufunga kamba, funga vingi

Ili kupiga KURA kwa Methali ya Mwezi
Kura
1
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
View this proverb in English
If you don't know how to tie a rope, tie a lot
Hapo zamani za kale kulikuwa na kijana aliyetafuta kipaji chake. Siku moja, alishauriwa na babu yake “Kila mtu ana kipaji, utafute chako.” Kwa hivyo, alianza safari ya kukitafuta.

Barabarani aliwakuta vijana wenzake wakicheza mpira wa miguu. Walimkaribisha na akaanza kucheza nao. “Labda hiki ndicho kipaji changu!” alijisemea moyoni.  Hata hivyo, mpira ulipomkaribia, aliogopa. "Sijui kupiga mpira!" akaasema. Wengine wakamkimbiza wakimchekea.

Mtaani, alikutana na mmachinga. “Labda hiki ndicho kipaji changu.” alifikiria. Mmachinga alimkubali, akamwagiza “Msalimie huyu mteja.” Lakini mteja alipomkaribia, kijana aliogopa, “Sijui jinsi ya kumsalimia mteja!” alisema kijana. Mmachinga alikasirika, na kijana akafukuzwa tena.

Akiendelea kutemebea alifikiria “Najuta kutoka leo, sina kipaji chochote.” Alipofika ufukweni, alikutana na mvuvi. Mvuvi alimkaribisha na akaingia mashuani. Mvuvi akampa kamba na kusema “Funga hii.” “Sijui kufunga kamba!” kijana alimjibu mara moja. Mvuvi akamjibu “Kama hujui kufunga kamba, funga nyingi.”

Baada ya siku hiyo, kijana alijifunza mengi kutoka kwa mvuvi, na alifunga maelfu ya kamba. Hatimaye, alikuwa mvuvi stadi aliyeheshimiwa na jamii.

Kipaji chako hakipo tu katika asili yako, bali kinaundwa na juhudi unazozitoa. Ukubali kufundishwa na wengine, na usiogope kujaribu vipya. Fundo la kwanza utakalofunga, hulifungwi vizuri sana. Lakini kadri unavyoendelea kufunga kamba nyingi, ndivyo utakavyojifunza mbinu na mikakati bora.

Yule anayesema "siwezi" hujizuia nafasi za kujifunza. Kama hujui jinsi ya kufanya kitu fulani, ujifunze kwa vitendo na mazoezi. Kama hujui kupiga mpira, piga mipira mingi. Kama hujui kusalimia wateja, wasalimie wengi. Kama hujui kufunga kamba, funga nyingi.
Marejeleo
Shukrani kwa Jan M anayetoka jimbo la Connecticut, Marekani, kwa kupendekeza methali hii kwetu!
Hadithi ni ya kwangu; inaruhusiwa kunakili / kuchapisha bila idhini ukitaja tu chanzo. CC BY
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Kadiri hamu ya kula inavyoongezeka, chakula kina ladha bora.

Methali hiyo ilionekana kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Miguel de Cervantes Don Quixote, kilichochapishwa mwaka wa 1615 (katika Sehemu ya II, Sura ya V)

Mara nyingi wazazi husema hivi kwa watoto wao wanapokuwa walaji kwa fujo.
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
by Nankya Sauda 🇺🇬
🏆 Proverb Essay Contest 
🥇 First Place Winner

Still waters run deep

Ever taken time to wonder why the elderly will always live to be wiser than the young? Have you ever taken time to meditate on where your origin sprouts from? If not, it is high time you started looking for your origin because it is important for one to know their roots. 
 Over time, you take the burden to unveil the nature of famous geniuses and their personalities, you will come to realize that they are celebrated introverts.  It is important that one takes off some time their busy schedule and read about some of the top celebrated geniuses like Albert Einstein , the famous scientist from whom we derive one of the most educative quotes;
The monotony and solitude of a quiet life stimulates the creative mind.”

This highlights that time spent alone does not only provide one with space for self-reflection but also gives space to someone to use their mind creatively. Great talkers are great are great lawyers they say, and we have seen this happening during our daily routine where people make empty promises, make false declarations to please those around them but may never take time off to do something in a bid to realize their words. Because of that, many have ended up losing trust in these so called great talkers.
     On the other hand however, silent people have always blown our minds with their actions. Their moves are always calculated, their ambitions clear and their actions intentional. Romantic lovers in a relationship are always spicing up their relationships with new inventions to keep their love blooming. Those that have employed or stayed around introverts can justify that staying around these people has been one of the greatest achievements in their lives, for these have always worked  smarter, had critical thinking sessions in their alone time and eventually produced the best results and the biggest promotions.
     Literally, we can loosely define proverbs as traditional sayings that are particular to a particular country. They are short and wise sayings that usually offer advice as well as boost an idea in relation to the day to day life.  In fact, for one to have a clear and elaborate understanding of cultural norms and practices, it is wise that they always make a reference to proverbs since they can have an elaborate meaning beneath them.
     Historically, the proverb “STILL WATER RUNS DEEP” draws its origin from the ancient times in Latin. It became popular after Shakespeare used it in his play Henry vi in 1590. He said;
“Smooth runs the water where the brook is deep”

We realize that, in some instances the most dangerous people with the wickedest hearts have always calculated their moves and taken action at a time everyone least expects them to. That is why betrayals come from people we least expect them from. It is therefore crucial for someone to not only take what the eyes meet but also take caution especially from people who do not retaliate immediately after they have been provoked or confronted.
     Albert Einstein despite his introverted character, he his famously known for devising his theory of relativity which revolutionized our understanding of space, time, gravity and the universe.
     Conclusively, it is very important  not to draw conclusions just because looks are deceptive and there is always more to know and discover than the eyes can see.
...
That which draws our attention, gets more attention. 

A wheel that makes noise is more likely to receive oil than other wheels (that also might need oil). We have limited attention, and thus we give our attention to people, projects and problems that stand out. This proverb asserts that there is not necessarily a correlation between the things we give our attention to and the things that actually need our attention.

Another version of the proverb is "the squeaky wheel gets the grease," and though the origin is unknown, American humorist Josh Billings is commonly attributed through his poem "The Kicker" in 1870
I hate to be a kicker,

I always long for peace,

But the wheel that squeaks the loudest,

Is the one that gets the grease.
 
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Siku moja, mfanyabiashara mashuhuri alitafuta msaidizi. Alipokea maombi na CV za watu wengi sana, lakini wawili tu walikidhi vigezo: Amina na Baraka. Ili kuamua kati yao, aliwaita wote wawili, na akawaalika waje kwaajili ya mahojiano ya ajira, kesho yake asubuhi. "Saa tatu kamili -- vaa mavazi ya kazi, na usichelewe!" Akawaonya.

Kesho yake Ali aliwahi kuamka, akavaa suti yake nzuri, na alipanda basi kijijini kwake saa 2. "Bora kinga kuliko tiba" alifikiria. Njiani kuelekea mjini, basi ilianza kutoa moshi. Abira wote walishuka na waliachwa porini. Hapo hapo mvua ilianza kunyesha. Kila basi lililompita, Ali akaomba nafasi, lakini, kutokana na hali ya hewa, mabasi yote yalikuwa yameshajaa. Kwa hivyo ikabidi atembee kwa miguu. Ilipotimia saa tatu, bado Ali alikuwa mbali na mji, na mvua ikawa kali zaidi na zaidi. "Lazima niendelee" akajiambia, "Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa."

Wakati huohuo mjini, Baraka aliamka ghorofani kwake, na akashtuka ghafla akiona jua lilikuwa limeshafika mbali angani. "Aisee! Niliweka alarm! Simu yangu ina shida gani sasa?" Alitazama saa ukutani: Saa tatu kamili. "Bora niache tu. Hata nikiondoka saivi, bado nitachelewa kufika. Si alisema usichelewe? Hatamwajiri aliyechelewa." Kwa hivyo Baraka, akiwa na huzuni, akalala tena.

Saa nne na nusu, hatimaye, Ali alifika ofisini kwa mfanyabiashara na kugonga mlango, suti yake ikichuruzika maji na matope sakafuni. Mfanyabiashara akajibu. "Si nilikwambia vaa mavazi yanayofaa na usichelewe? Sasa umechelewa zaidi ya saa limoja na mavazi yako yamechafuka. Niambie nitawezaje kukuajiri baada ya hapo?" Kisha Ali akaeleza yote yaliyomtokea. Mfanyabishara akamjibu "Nimejifunza mengi kuhusu wewe kutoka kwa hadithi yako Ali. Ukiwa na kusudi kichwani, utafanya kazi kwa bidii, na pale unapokutana na vikwazo hukati tamaa, hata kama umechelewa. Nakwambia, wewe ndiye wa kwanza kufika leo. Mwingine alikosa kabisa. Nitakuajiri wewe."

Mafanikio makubwa huanza na makosa mengi, lakini baada ya muda, uvumilivu na ustahilimilu huleta matunda. Kukosa ni uanadamu, lakini Mungu ni mvumilivu sana kwetu. Anatupa nafasi nyingi za kujifunza na kujaribu tena, ilimradi tusikate tamaa.

Wengine wanasema methali ya "Better late than never never" inatoka kwa kitabu cha The Canterbury Tales, kilichoandikwa na Chaucer miaka ya 1390.
Better than never is late
“Bora kuliko kamwe ni kuchelewa
-The Canterbury Tales, The Canon's Yeoman's Tale
Wengine wanasema chimbuko la kweli ni kitabu cha Historia ya Roma, kilichoandikwa na Livy takriban mwaka wa 20 KK.
Lilatini: potiusque sero quam numquam
Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa
- History of Rome, Book 4

Methali ya Kiingereza inayoendana ni:
It's never too late
Hakuna kuchelewa
 Methali ya Kiingereza inayopinga:
Don't close the gate after the horse has bolted.
Usifunge mlango baada ya farasi kukimbia

Methali ya Kihindi: 
जब जाति तब सवेरे
Wakati wowote unapoamka, ndo asubuhi yako

...

Fikiria kama umechelewa Mahojiano ya Ajira. Ungefanyaje? Next time unapofikiri "Nimeshachelewa" jiambie "Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa." Kwa mfano makala hii ya Methali ya Siku ilichelewa, lakini sasa unaisoma - Asante!

Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by