You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Kama hujui kufunga kamba, funga vingi

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
1
Updated 4mo ago
by
View this proverb in English
If you don't know how to tie a rope, tie a lot
Hapo zamani za kale kulikuwa na kijana aliyetafuta kipaji chake. Siku moja, alishauriwa na babu yake “Kila mtu ana kipaji, utafute chako.” Kwa hivyo, alianza safari ya kukitafuta.

Barabarani aliwakuta vijana wenzake wakicheza mpira wa miguu. Walimkaribisha na akaanza kucheza nao. “Labda hiki ndicho kipaji changu!” alijisemea moyoni.  Hata hivyo, mpira ulipomkaribia, aliogopa. "Sijui kupiga mpira!" akaasema. Wengine wakamkimbiza wakimchekea.

Mtaani, alikutana na mmachinga. “Labda hiki ndicho kipaji changu.” alifikiria. Mmachinga alimkubali, akamwagiza “Msalimie huyu mteja.” Lakini mteja alipomkaribia, kijana aliogopa, “Sijui jinsi ya kumsalimia mteja!” alisema kijana. Mmachinga alikasirika, na kijana akafukuzwa tena.

Akiendelea kutemebea alifikiria “Najuta kutoka leo, sina kipaji chochote.” Alipofika ufukweni, alikutana na mvuvi. Mvuvi alimkaribisha na akaingia mashuani. Mvuvi akampa kamba na kusema “Funga hii.” “Sijui kufunga kamba!” kijana alimjibu mara moja. Mvuvi akamjibu “Kama hujui kufunga kamba, funga nyingi.”

Baada ya siku hiyo, kijana alijifunza mengi kutoka kwa mvuvi, na alifunga maelfu ya kamba. Hatimaye, alikuwa mvuvi stadi aliyeheshimiwa na jamii.

Kipaji chako hakipo tu katika asili yako, bali kinaundwa na juhudi unazozitoa. Ukubali kufundishwa na wengine, na usiogope kujaribu vipya. Fundo la kwanza utakalofunga, hulifungwi vizuri sana. Lakini kadri unavyoendelea kufunga kamba nyingi, ndivyo utakavyojifunza mbinu na mikakati bora.

Yule anayesema "siwezi" hujizuia nafasi za kujifunza. Kama hujui jinsi ya kufanya kitu fulani, ujifunze kwa vitendo na mazoezi. Kama hujui kupiga mpira, piga mipira mingi. Kama hujui kusalimia wateja, wasalimie wengi. Kama hujui kufunga kamba, funga nyingi.
Sources
Shukrani kwa Jan M anayetoka jimbo la Connecticut, Marekani, kwa kupendekeza methali hii kwetu!
Hadithi ni ya kwangu; inaruhusiwa kunakili / kuchapisha bila idhini ukitaja tu chanzo. CC BY
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Kila kazi kubwa katika maisha huhitaji kufanyika kwa hatua ndogo, siku baada ya siku. 

Je, unajua methali zingine zinazofanana na hii au zinazotoa dhana hiyohiyo? 

Msemo huu unakumbusha shairi liitwalo "Vitu Vidogo" na Julia Abigail Fletcher Carney: 
Matone madogo ya maji,
Chembe kidogo za mchanga, 
hutengeneza bahari kubwa
Na ardhi ya kupendeza

Vivyo hivyo zile dakika ndogo,
ingawa ni ndogo,
hutengeneza enzi za milele. 
Julia Carney alitunga shairi hili mwaka wa 1845 darasani akiwa mwanafunzi darasani -- na alipewa dakika 10 tu kuliandika!
...
Updated 4mo ago
by
na Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥉 Mshindi wa Tatu
Ni mara ngapi umesikia Mchumia juani hulia kivulini? Hii ni methali ya kiswahili (kibantu) yenye maana ya kuwatia moyo watu katika shughuli mbalimbali wanazozifanya Kila siku wawe na Imani kuwa ipo siku watayafurahia matunda ya kazi yao. 

Methali hii huwapa watu nguvu, bidii, moyo, ujasiri, tumaini na weledi katika kufanya kazi. Mfanyakazi huamini kuwa baada ya kazi ngumu zenye surubu basi huleta mavuno mazuri yenye kumfanya astareheke kivulini akila matunda ya kazi yake. Shairi lifuatalo linaonesha kwa namna gani mchumia juani huwa katika majukumu ya Kila siku.

Siogopi jua wala mvua, nikiitengeneza kesho yangu
Siogopi maumivu Wala majeraha, maana yote ni ya muda
Jua kali na kazi ndiyo desturi yangu, ili kheri kuja maishani
Machinga,mkulima, makuli na mvuvi wao na jua, Ili kuitafuta kesho
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Ni mchana jua la utosi, kichwani nina mavuno, jasho linatiririka
Jua limezama Sasa kasia ufukweni, hoi kitandani, nyavu zi baharini
Nyumbani mtaa wa nne, nahodha wa familia surubu nivute  kheri
Jua Sasa la chomoza, Kiguu na njia kulitafuta tonge
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.

Bwana mmoja alikuwa mkulima. Maisha yake yote alitumia katika kilimo. Hivyo kupendeza kwake kulikuwa mara chache. Watu kijijini kwake walimuita mkulima stadi. Alijenga nyumba kwa kuuza sehemu ya mazao yake, alisomesha wanae kwa kilimo.

Bwana huyu alikuwa mtu mwenye bidii alijifunza siku zote kanuni za mkulima bora, hivyo kadri muda unavyokwenda mashamba yake alivuna mazao mengi. Watu wengi walistaajabu sana kuona mabadiliko makubwa ndani ya familia yake. Aliwekeza vitu vingi kijijini kwake, mashamba, nyumba, maduka na mifugo mingi vilitoka shambani.

Watu wengi walikuja kujichukulia hekima kwa mkulima stadi. Siku zote aliwaambia "Mchumia juani, hulia kivulini. Jembe limeniheshimisha kijijini Mimi na familia yangu. Maisha yangu sasa yanakwenda barabara kwa hakika niko kivulini nafurahia matunda ya kazi yangu ya juani. Mimi leo kijana wa mkulima huyo stadi najivunia malezi, uwajibikaji wake kwa sababu kazi za juani leo zimetufanya tupumzike na kula kivulini. Kwa hakika maana ya mchumia juani inaonekana kwa vitendo. Bidii yako ndilo jua lako na kivuli ndiyo matunda ya bidii yako.

Hadithi hii inashibishwa na hadithi ilee ya "Mabala the Farmer" yaani Mabala Mkulima iliyoandikwa na Richard S. Mabala(1989). 

Mabala alikuwa mfanyakazi bandarini Kisha akapunguzwa hivyo akachagua kurudi kijijini Morogoro. Mabala alikuwa mzembe,mlevi na mbishi. Mabala alikwenda shambani na galoni ya pombe alikunywa na kulala, alipoamka alimwongelesha mkewe lakni hakujibiwa zaidi ya  sauti ya jembe tik-tok, tik-tok .

Mabala alikuwa mbishi, alimwagilia sukari shambani alifikiri ni mbolea, lakni mwisho alibadilika na kuwa mkulima stadi akawa mchumia juani ili familia yake ije kulia kivulini. Je wewe unahisi Mabala ni mchumia juani? Ndani ya familia au kwenye jamii mkulima stadi anakupa picha gani?

Mwisho hadithi hii kutoka katika methali ya mchumia juani hulia kivulini hutuonyesha dira njema katika kila tunachokifanya katika maisha ya kila siku. Huku methali kama Subira yavuta kheri, Mgaa na Upwa hali wali mkavu zote hufanana kimaudhui, zipo katika kuipa jamii nguvu na matumaini kwa kila jambo lifanyikalo katika malengo.
...
Kwa kiingereza tunasema "One man's trash is another man's treasure," maana yake, kilichotupwa na mtu mmoja, kinaweza kutumikia mwingine na kuwa na thamani kwake.

Msemo huu hutumika ili kueleza jinsi mapendeleo ya watu hutofautiana, ama kuonyesha matumaini kwamba wanadamu ni wabunifu katika masuala ya kupanga upya au kuchakata vitu vilivyotupwa na wengine.

Kwa mfano, mjasiriamali Gibson Kiwago, mwanzilishi wa WAGA Tanzania, anachakata betri za laptop ili kuleta umeme kwa nyumba na maduka. Jifunze zaidi kuhusu E-Waste (Orodha ya Kusoma)!

Dhana kwamba thamani ya kitu hutegemea mtazamo wako ipo tangu zamani. Chimbuko cha msemo huu ni methali ya Kiingereza iliyotumika karne ya 17:
One man's meat is another man's poison
Nyama na mtu mmoja ni sumu ya mtu mwengine

Je umewahi kuona thamani katika kitu kilichotupwa na mwengine?
...
Updated 4mo ago
by
Kadiri hamu ya kula inavyoongezeka, chakula kina ladha bora.

Methali hiyo ilionekana kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Miguel de Cervantes Don Quixote, kilichochapishwa mwaka wa 1615 (katika Sehemu ya II, Sura ya V)

Mara nyingi wazazi husema hivi kwa watoto wao wanapokuwa walaji kwa fujo.
...
Updated 4mo ago
by