You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Taarifa
Majadiliano
Methali
Akiba Haiozi
ili kupiga kura
Kura
59
View this proverb in English
Savings don't rot
na Rose Mwanri 🇹🇿 
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥈 Mshindi wa Pili 

Akiba Haiozi

Methali ni usemi wa kimafumbo unaotumika katika jamii. Maneno katika methali huwa na maana ya ziada na methali huwa na pande mbili. Upande wa kwanza hutoa wazo na upande wa pili humalizia wazo. Akiba haiozi ni miongoni mwa methali za kiswahili inayotumika sana katika jamii za kiafrika na kwa watumiaji wa lugha ya kiswahili duniani, ikiwa na lengo la kuwaasa watu juu ya umuhimu wa kujiwekea akiba.

 Dhima ya methali hii ni kutusisitiza sisi wanajamii kujianda vema na maisha ya leo pamoja na kesho huku tukiwa tayari kuzikabili changamoto mbalimbali za maisha.

 Methali hii hutuonyesha ni kawaida mwanadamu kupatwa na dharura mbalimbali katika maisha ya kila siku. Mfano kupatwa na maradhi, ajali, au hata kifo. Pale unapokuwa na akiba uliyojiwekea itakusaidia wakati umepatwa na changamoto ya ghafla ambayo hukuitarajia.

 Faida nyingine ya kuweka akiba ni kuboresha maisha. Cha kwanza nashauri tuwe na utaratibu wa kuweka akiba mara kwa mara ili kuweza kuboresha maisha yetu kwa ujumla. Tunavyozidi kuweka akiba ndivyo ambavyo akiba hiyo inaweza kutusaidia kuboresha makazi yetu na miundombinu kwa ujumla ndani ya jamii zetu. Mfano mzuri ni wazazi ambao akiba wanazoziweka huwasaidia kulipa karo za shule pamoja na kununua vifa mbalimbali vya shulena hata gharama zingine zinazojitokeza kwa wakati huo.

 Methali hii pia inatukumbusha kuwa kadri tunavyozidi kuweka akiba ndivyo tunavyokuza hazina yetu. Swa na ile methali inayosema “ Haba na haba hujaza kibaba” ukichambua methali hizi zinaendana maana na utagundua ni ukumbusho mkubwa kwetu kuhusu ujenzi wa hatma njema ya jamii yetu ya sasa na baadae. Kwa kuwa zinatuhimiza kuwekeza kwa kila chumo tulipatalo. Tunakuza hazina kwa kuwa kile tunachoweka akiba kipo kwaajili yetu.

 Chukua nafasi kujiuliza, ni mara ngapi umepatwa na changamoto na akiba ndiyo ikaokoa jahazi, ni mambo mangapi yametokea bila taarifa na akiba ndiyo imetumika kuweka mambo sawa. Naamini sote tunapaswa kuweka akiba bila kujali kipato ni kikubwa au kidogo. Mfano unaweza kuanza kuweka akiba kidogo kidogo kutokana na kile unachokipata na kufikia muda Fulani utakuwa na akiba kubwa.

 Vilevile methali hii inasaidia kukuza maarifa kwa mtu mmoja mmoja na jamii hasa pale ambapo pamekuwepo na tofauti ya uhifadhi wa akiba kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Hapo zamani tunaambiwa watu walikuwa wanahifadhi akiba zao kwa kuchimba chini ya ardhi, kuweka chini ya kitanda au hata sehemu zingine ambazo wao waliamini ni salama. Leo hii watu hawatumii sana njia za kienyeji kuweka akiba zao. Ukija kwenye fedha zipo benki zenye mifumo thabiti na salama katika kuhifadhi fedha. Kwa upande wa akiba ya mazao pia zipo njia salama za kuhifadhi tena hata kwa muda mrefu bila kuharibika. Kwa hakika akiba haiozi.

 Waswahili tunasema “akiba haiozi”, “haba na haba hujaza kibaba” ikimaanisha kwamba akiba yaweza kuonekana ndogo ila kadri inavyoongezeka ndivyo inavyokuwa kubwa. Kinyume chake tunaambiwa “Chovya chovya humaliza buyu la asali”, “Bandu bandu humaliza gogo”. Tukikumbushwa kuwa vile tunavyochukua akiba zetu kidogo kidogo bila sababu ya msingi ndivyo ambavyo iko siku tutahamaki na kuona akiba imeisha bila kuona kitu cha maana kilichofanyika. Tukumbuke “mali bila daftari huisha bila habari”, tuangalie mfano wa shairi hili linalotusisitiza kuhusu kuweka akiba.

Akiba kweli hazina, haijawahi saliti,
Kwetu ni muhimu sana, hutubeba kwa nyakati,
Kipindi kweli hatuna, inasimama kwa dhati,
Sote tuweke akiba, akiba ni mkombozi.

 Kwa hakika ni dhahiri yatupasa kutunza vitu vyetu vizuri na rasilimali tulizonazo kwa kuweka akiba ili tuweze kujinusuru pale ambapo tunapokumbwa na changamoto za kushtukiza kwa ajili ya maisha yetu ya sasa na ya baadae.

Marejeleo

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishinda nafasi ya pili 🥈 katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Rose Mwanri ni mwalimu Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Rose Mwanri
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org

Related on Maktaba.org 


Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Methali hii inahusiana na tabia ya kufikiria kwamba watu wengine wana vitu vizuri zaidi, hali nzuri zaidi nk... Kwa mfano kufikiri jirani yako ana majani mazuri kuliko wewe.

Chanzo cha methali hii ni "Sanaa ya Upendo" na Ovid, kitabu cha mashairi yaliyotungwa ili kutoa shauri kwa wanaume na wanawake kuhusu kutafuta na kudumisha mahusiano ya kimapenzi. Kitabu hiki kiliandikwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita, takribani 2 KK:
Watu hutaka furaha mpya. Huwa tunaona kuwa watu wengine wana bahati zaidi kuliko sisi wenyewe. Mazao daima ni bora katika shamba la jirani yetu; ng'ombe wake hutoa maziwa zaidi. 
 - Ovid Ars Amatoria (Sanaa ya Upendo), Ukurasa wa 24

Kwa upande mmoja, methali hii inamaanisha, bora kushika kile ulicho nacho, na kupuuza kile ambacho wengine wanacho, hata kama inaonekana ni bora zaidi. Lakini pia kwa mtazamo mwengine, inamaanisha bora kutumia akili yako katika kuboresha hali yako mwenyewe (kama kumwagilia shamba lako) badala ya kufikiria sana ukweli kwamba shamba lako, au hali kwa ujumla, ni duni. Methali nyingine ni "Majani huonekana ya kijani zaidi pale ambapo yalipomwagiliwa maji." 

Methali zinazofanana kikanuni:
Kihindi: 
दूर के ढोल सुहावने लगते हैं
Ngoma za mbali husikika vizuri
Kichina: 
隔籬飯香 
Wali wa jirani hunukia vizuri
Kijapani:
隣の芝生は青く見える
Majani ya jirani huonekana kijana zaidi
Kurusi:
соседняя очередь всегда движется быстрее
Foleni nyingine husogea kwa kasi zaidi
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Ustawi wa kiuchumi huenea na huwafikia raia wote wa nchi au eneo. Nchi haiwezi kufaidika bila raia wake wote kufaidika kwa namna moja au nyingine, kama vile baharini, maji yakijaa boti zote zitapanda, wimbi linalokuja litainua boti zote ziwe mitumbwi, jahazi, meli au mashua.

Msemo huo hutumiwa kumaanisha makundi yote yalinufaika kutokana na mabadiliko ya hali, hasa utitiri wa rasilimali, hata kama inaonekana kama zinawafikia matajiri wachache pekee. Nimesikia wafanyakazi wakiona wenzao wamepokea bonasi au kamisheni kubwa wanasema, "A rising tide lists all boats," ikimaanisha mauzo yakipanda, mapato ya kampuni yataongezeka na fursa kwa kampuni, na kwa hivyo, kwa wafanyikazi wote pia. Katika kesi hii, ni wazi wimbi halizinui boti zote kwa usawa au kiasi kilekile.

Wakosoaji wa methali hii wanaweza kulalamika kwamba methali hii inatumika pia ili kuhalalisha mpango au makubaliano yoyote hata kama yatawanufaisha wachache tu. Lakini kwa kawaida msemo huo husemwa  na viongozi kwa matumaini au kama pongezi.

Methali hiyo mara nyingi huhusishwa na John F. Kennedy rais wa Marekani, ambaye aliiitumia katika hotuba yake, mwaka wa 1963 akijitetea baada ya baada ya kukosolewa juu ya ujenzi wa bwawa ulitumia pesa nyingi sana (matumizi ya fujo). Mwandishi wa hotuba za Kennedy (aliyeitwa Ted Sorensen) alifichua kwamba Rais Kennedy alitumia methali hii baada ya kuisoma katika jarida la "New England Council."

Msemo karibu na huu ni "to grow the pie" yaani "kukuza keki" ambayo inamaanisha, kama keki ni kubwa zaidi, washiriki wote watapata keki zaidi hata kama uwiano/asilimia haibadiliki.

Je, unakubali kwamba ustawi mpana wa kiuchumi huwafikia wote?
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Hapo zamani za kale, palikuwa na binti mrembo, mkarimu, mwenye akili aliyeitwa Poshia. Wanaume wengi walitaka kumuoa na walikuja ili kuomba uchumba. Baba Poshia alikuwa amefariki dunia. Alikuwa tajiri na aliacha wosia ulioelekeza kamba yeyote aliyetaka kumuoa Poshia, lazima achague kati ya masanduku tatu: sanduku la dhahabu, sanduku la fedha na sanduku la risasi. Atakayechagua sahihi ndiye atakayeruhusiwa kumuoa Poshiia na kurithi mali zote za Baba Poshia. Siku moja, Mfalme wa Moroko alikuja ili kuomba uchumba.

Mabepari wa Venisi

Tazama ▶️ YouTube


POSHIA: Kayavute mapazia masanduku yaonekane kwake mtukufu huyu mtoto wa mfalme. Haya sasa kachague.

MOROKO: La kwanza, ni la dhahabu, lenye maandiko haya:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
Na la pili, ni la fedha, linaloahidi hivi: 
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
La, tatu, risasi butu, na onyo lake ni butu:
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
Nitajuaje yakuwa nimechagua vizuri?

POSHIA: Moja lina picha yangu, mzawa wa mfalme: Ukilichagua hilo basi na mimi ni wako.

MOROKO: Muungu Fulani uniongoze. Hebu nione; nitayachagua tena maandiko toka mwisho. Nitaanzia la tatu: lasemaje, la risasi?
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
Itambidi atoe - atoleeni? Risasi? Na pia ahatarishe - kwa ajili ya risasi? Sanduku hili latisha: wahatarishao vyote hutumaini kupata faida iliyo nzuri: Wenye moyo wa dhahabu hawajali takataka; Kwa hiyo basi sitoi na wala sihatarishi chochote nilicho nacho kwa sababu ya risasi. La fedha lasema nini, lenye rangi ya baridi?
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
Apate astahilicho! Subiri hapa, Moroko. Upime thamani yako kwa mkono wa mwadilifu: Kama ukithaminiwa vile ujifanidivyo wastahili kutosha; walakini ya kutosha inaweza isitoshe kumpata siti huyu. Bali nikitia shaka kuwa simstahili,Basi hapo nitakuwa najiumbua mwenyewe. Stahili yangu ni nini? Bila shaka ni bibie. Namstahili, hakika, kwa nasaba na kwa mali, kwa madaha na kwa sifa zote za malezi mema na kuzidi yote hayo namstahili kwa pendo. Vipi, nisiendelee, nichague papa hapa?
Hebu tuyaone tena ya sanduku la dhahabu:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Naam, ni siti huyu; anotamaniwa kote. Toka pande zote nne za dunia wanakuja kubusu sanamu hii takatifu ilo hai: Majangwa ya Hirikani na nyika pana ajabu, za Uarabuni kote, sasa zimekuwa njia ziletazo watawala kumwona Poshia bora. Nayo dola ya bahari ambayo inapofura hutemea hata mbingu, haiwezi kuzuia nia ya wageni hao; ila wanazidi kuja, kama wavuka kijito, kumwona Poshia bora. Moja la matatu haya lina picha yake nzuri. Itawezekana kweli liwe lile la risasi? Wazo chafu kama hilo lingekuwa ni laana. Halifai japo kuwa sanda yake ya kaburini.
Au niwaze ya kuwa kawekwa ndani ya fedha? Moja ya kumi na moja ya thamani ya dhahabu? Hilo ni wazo la dhambi! Kito cha thamani hivi hakiwekeki po pote ila ndani ya dhahabu. Uingereza wanayo sarafu tu ya dhahabu, ambayo kwa juu yake imechapwa malaika. Bali hapa malaika mwenyewe hasa yu ndani ya sanduku hili hapa, na bahati nijaliwe!

POSHIA: Ni huu hapa, chukua, mzawa wa mfalme; kama sura yangu imo nimekuwa mali yako.

[Anafungua sanduku la dhahabu]
MOROKO: Mama yang! Nini hii? Ni fuu tupu la kichwa, ambalo katika jicho lina hati ma’ndiko. Nitasoma maandiko.
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.
Nimefarikiwa kweli. Bure nimejitanibu. Basi buriani, joto; nawe, makiwa, karibu. Basi kwa heri Poshia. Ninayo
huzuni sana siwezi kwa heri ndefu: Ndivyo wanavyoagana watu waliopoteza.
[Aondoka na Wafuasi wake. Tarumbeta]
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Je, umewahi kuona muda huenda pole pole wakati unasubiri? Lakini kwa upande mwingine, ukivutiwa na mambo mengine, m muda huenda haraka.

Kwa mfano, ukisubiri kumwona daktari, muda ni mfupi ukiangalia simu yako au kusoma gazeti, badala ya kungoja tu kusikia jina lako liitwe.

Chimbuko cha methali hii ni Benjamin Franklin kwa Poor Richard's Almanac, hata hivyo haionekani hapo. Badala yake, Franklin aliitumia katika insha juu ya 'sumaku ya wanyama' mwaka 1785. 
Nilikuwa na Njaa sana; ilikuwa imechelewa sana; "Sufuria inayotazamwa huchemka pole pole," kama Poor Richard asemavyo.
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by