You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Taarifa
Majadiliano
Methali

Siku ya kufa nyani miti yote huteleza

Ili kupiga KURA kwa Methali ya Mwezi
Kura
0
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by

Maana

Mtu hawezi kuepuka hatima yake.

Matumizi

Methali hii hutumiwa nyakati za vita, au juu ya kiongozi pale ambapo wakati wa kuanguka umefika (mf. Macbeth). Tazama pia: Kile kinachozunguka huja karibu (What goes around comes around)

Utekelezaji

Hata ukijitahidi sana kufikiria, kuhangaika na kuepuka matatizo, bado yanaweza kujitokeza. Wakati mwingine, kujaribu kuzuia tatizo kunaweza kusababisha tatizo lilelile kutokea au kuifanya kuwa mbaya zaidi (mf. Oedipus). Nyani anaweza kuchagua tawi lingine ili kuepuka kuteleza, lakini tawi hilo pia linaweza kuteleza vile vile.

Katika hekaya za Kigiriki, hatima zilitajwa kama dada watatu: Clotho anayesuka uzi wa maisha (kuzaliwa), Lachesis anayechota uzi (akimpa kila mtu baraka na changamoto alizojaliwa maishani), na Atropos anayekata uzi (kifo).

Methali hii inatuhimiza kukubali ukomo wa nguvu yetu na kukiri kwamba mambo mengi muhimu yako nje ya udhibiti wetu.

Misemo inayohusiana


Kiswahili:
Ulichojaliwa hakipunguzi wala haiwezi kukuongezea
Siku za mwizi ni arobaini Siku za mwizi ni arobaini 

Kilatini (Stoic
Amor fati
Penda hatma 
 
Kichina (kutoka kwa Analects)
生死有命,富貴在天
Maisha na kifo vimepangwa, utajiri na heshima [hutoka] mbinguni.
Marejeleo
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Methali hii ya Kiingereza "To the victor go the spoils" inatafsirika pia kama "Mshindi ndiye anayechukua vyote" au "Mshindi hupokea nyara zote."

Mshindi wa shindano ndiye anayepokea tuzo. Huwa anachukua asilimia kubwa ya faida ama faida zote, na hata manufaa zaidi ya yale yaliyokuwa yakipiganiwa.

Katika vita, nyara zinaweza kuwa ardhi, mamlaka au rasilimali nyingine zinazotafutwa. Katika shughuli zingine nyara zinaweza kuwa sifa, pesa au fursa. Methali hii hutumika ili kueleza matokeo yasiyo sawa au kutukumbusha kwamba katika migogoro mingi ni mshindi ndiye atakayechukua yote, asilimia kubwa, au angalau, kupendelewa. Angalia sehemu ya vyanzo kwa maelezo ya muktadha kuhusu chimbuko la methali hii, mwanasiasa wa Marekani katika miaka ya 1830 (Kiingereza).
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
by Ibrahim Nyanda
🏆 Proverb Essay Contest
"Why is it that our village is not developed compared to other villages around us? Many young people our age from other villages have studied, and some have found their meaningful jobs in the city. Although there's a school in our village, we young people aren't doing well in school. When teachers are hired, they don’t stay long, they leave. What is there here in Bombambili?” These were the questions that the young man Akilimali asked his friend Manase while they were grazing the cattle. 

After this question, Manese seemed immersed in a great wave of thoughts ,and after considering for a while, he turned to his friend, looked at him deeply and asked him, “Do you believe in witchcraft?” Akilimali answered by nodding his head in agreement and said, “I believe, because I’ve often seen people going to witch doctors, and when they go through difficulties, they believe they've been bewitched. Don’t you remember the other day when we were told that Granny Andunje was found on the roof of old man Masanja stark naked, practicing witchcraft at night. So after that, how can I not believe, my friend?”

Manase looked at Akilimali carefully and then said to him “I want to tell you a secret that you won’t believe... Do you know your mother and your sister are witches?” Akilimali remained dumbfounded like a lizard caught in a door, and then, swelling with anger, he told Manase “Woah, hey kid, don’t start bringing me this nonsense, you stop calling my mom a witch or I’ll show you something you won’t believe with your eyes, ohoooo!!” 

Manase calmed his friend Akilimali, then told him “Wait for me to return the cows to the neighbor, then I’ll tell you the whole story. I know you’ll understand, you just chill out. “

As soon as he has returned the livestock, Manase began telling Akilimali, “My friend, I want to tell you a secret that I’ve kept for a long time. Everything you see here -- even the lack of development in the village -- it’s because of witchcraft. Every day I see your mom and your sister riding a hyaena. They pass by my mom's house, going to bewitch people...”  Manase paused a little, then continued

"You can’t believe it-- even I didn’t believe it until I was anointed with a special potion and saw them. I’ll give you this potion tonight. Apply it in your eyes and you’ll give me an answer tomorrow.”


After dinner, Akilimali was warming himself by the fire with his dad, outside their mud house thatched with grass, while his mom and sister were inside. He applied the potion as directed... and after ten minutes he saw his sister and his mom riding the hyena like a motorcycle, ready to embark on their voyage to bewitch people!


“Forgive me my friend, it was just anger.” Akilimali spoke these words choking back tears. 

“I knew it. Now you see our village is not developing and even your own mom and sister are involved. Every villager who wants to bring development ends up dead. One day they'll end up like Granny Andunje."

“I’m sure even your dad doesn’t know that your mom and sister are witches, and every day they go out to bewitch people and leave you two a magic trick to make you think they’re around. Go put that potion in your dad's eyes, then you’ll give me an answer” explained Manase. 


That evening, secretly, Akilimali explained to his dad that his sister and his mom were witches, a thing which his dad vehemently denied. 

“Mom, today Dad is watching us; look how he is staring at us,” Akilimali’s sister told their mom, riding the hyena as before, as their dad and brother were outside warming themselves as they usually did.

“I don’t think he sees us; turn the hyena so it looks like we’re heading towards them,” Akilimali’s mom said.

Akilimali says that was the last day he saw his father, because after seeing the hyena carrying his wife and daughter, he bolted like he was running the hundred-meter dash. Indeed, what you don’t know is like the darkness of the night, Akilimali was left in disbelief that all this time he lived with his mom and sister not knowing they were witches.
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Methali hii inatoka Kiingereza "A penny saved is a penny earned." Maana yake, mia inayobaki mfukoni inaweza kutumiwa kwajali ya madhumuni mengine. Mifano: Inaweza kutumika kwaajili ya kununua kitu kingine, unaweza kukopesha au kuwekeza ili kuingiza riba au pesa zaidi katika siku zijazo. Katika uchumi, kanuni hii inaitwa Opportunity Costs (gharama za kukosa fursa). Tunapotumia pesa au muda kwa jambo limoja, tunapoteza pia fursa ya kuzitumia kwajili ya jambo lingine.

Methali hii huhusishwa na Benjamin Franklin, lakini si chimbuko halisi, wala hakuandika msemo huu kamili. Misemo karibu na huu ilichapishwa kabla yake. Kwa mfano: 

A penny spar'd is twice got.
Senti iliyookolewa hupatikana mara mbili.
- Outlandish Proverbs by George Herbert (1640)  
 
Katika Poor Richard's Almanac (1736), Benjamin Franklin alinukuu methali hii na alifafanua vizuri kanuni ya Opportuinty Cost hivi:

Vidokezo kwa Wale Wanaotaka kuwa Matajiri

Matumizi ya pesa ndiyo faida zote zinayopatikana ukiwa na pesa.
Kwa pound [£] sita kwa mwaka [yaani riba] unaweza kutumia  £ mia [yaani kupitia mkopo], kama unajulikana kama mwaminifu na mwenye busara.
Anayetumia groat [senti 4] kwa siku bure, hutumia pound £ zaidi ya sita kwa mwaka, ambazo ni bei ya kujipatia matumizi ya pound £ mia moja.
[Kwa hivyo] Anayepoteza muda wake wa thamani ya groat [senti 4] kwa siku, siku moja na nyingine, anapoteza fursa ya kutumia pound mia moja kila siku.
Anayepoteza muda wa shilingi tano kwa uvivu hupoteza shilingi tano, ni kama amezitupa tu baharini.
Anayepoteza shilingi tano sio tu kwamba anapoteza kiasi hicho, bali anapoteza pia faida yote ambayo ingeweza kupatikana kwa kuzitumia katika shughuli zake, ambayo, akiwa kijana, wakati wa uzee ingefikia kiasi kikubwa cha fedha.
Tena: anayeuza kwa mkopo huongeza bei ya kile anachokiuza kwa kiasi sawa riba angaliingiza na pesa hizo kwa kipindi ambacho atazikosa. Kwa hivyo, anayenunua kwa mkopo hulipa riba kwa kile anachonunua, na anayelipa pesa mara moja kwa kila anachonunua hukoa fursa ya kuzikopesha kwa wengine, kwa hivyo aliye na kitu alichonunua ameshalipa riba kwa matumizi yake.
Hata hivyo nasema kulipa mara moja unaponunua ni bora, kwa sababu anayeuza kwa mkopo anatarajia kupoteza asilimia tano ya mikopo; kwa hivyo anaongeza bei ya kile anachokiuza kwa asilimia ileile ili kuzuia hasara. Wanaolipa kwa mikopo hulipa kodi mara moja. Anayelipa kwa pesa mara moja anaweza kuzuia kodi hii
"Senti iliyohifadhiwa ni senti mbili hakika;
[haba] kwa siku ni [nne] kwa mwaka."
 
Basi, unapofikiria kutumia muda au pesa zako katika jamblo fulani, jiulize, ningekosa, ningepata fursa zipi? Pesa hizi zingeweza kutumikia vipi? Mifano: kumkopesha mwingine, kurudisha madeni uliyonayo, kubuni kitu kipya au kuwekeza katika kitu ambacho kinaweza kuleta faida kubwa mbeleni.
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by