You are now browsing in English. Switch to Swahili
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiingereza. Rudi kwa Kiswahili"
You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

If a child cries for a razor, give it to him (Mtoto akilia wembe, mpe)

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 5mo ago
by
View this proverb in Swahili
Mtoto akilia wembe, mpe
Hello, lovers of language and wisdom!  Welcome back to your daily dose of proverbs. Today's proverb is "Mtoto akilia wembe, mpe" -- literally, "If a child cries for a razor blade, give it to them." To many parents that might sound, well… pretty harsh, right? But if you speak Swahili, you’ve probably heard this proverb. Do you agree with it? What does it mean to you? Share your thoughts.

If I hear I will forget, if I see I will remember, if I do I will understand.
-Teacher Amos

If a child wants a razor, then give it to him so that he understands why he was warned against playing with it.  This proverb illustrated the importance of giving people opportunities to learn from their own experience, even if they might get (slightly) hurt. Also, even if you refuse to give it to him, he might disobey you and play with it while you are away. This proverb can also be used as a warning to someone who ignores advice and insists on his own way.  While it is important to listen to advice and warnings from others, sometimes we need to see the consequences of our own actions to understand.

Natural Consequences

In the area of ​​parenting, this proverb teaches the principle of Natural Consequences.  A natural consequence is the result that naturally follows because of a person's behavior.  Unlike corporal punishment, penalties or demerits, natural consequences occur without the intervention of the parent or guardian.  For example, imagine if your son forgot his notebook at home.  What would you do? Some parents answer "I wouldn't do anything; he’ll have to explain to his teacher."  Others say "I would run to school to bring him the notebook, and then in the evening I would discipline him."  Which one is better?  Answer below...

Question for parents: If a child cries for a snake, will you give it to him?

 
OK, so we’ve agreed, if a child cries for a razor, we should give it to him.  But… imagine if the child is begging for something more dangerous– Would you agree? Jesus asked parents: "If your child asks for a fish, will you give him a snake?" What if the child asks for a  poisonous snake? Will you give it to them? 

A snake has real risks.
-Teacher Shila   

A razor can give them a small wound, but it is not as dangerous as a poisonous snake. What if they ask to quit their studies to play mobile games all day?  What if they ask to marry someone you don't trust at a young age? There are also important decisions that children are not ready to make for themselves. How do you, as a parent, decide or recognize when you should save and protect your child from regret, and when you should let the world teach them? Parents, tell us your opinion!

Apply this proverb in your life

Education: People remember what they experience and do, rather than what they are told.  Find opportunities to apply what you learn.
Parenting: Give the child freedom and opportunities to learn through experience.  Don't solve everything for him, and don't be afraid when he fails, if there is no danger or long-term effects, because failure is an opportunity for them to learn.
Listening: If you ignore warnings and advice, don't be surprised to see the predicted consequences occur.
Details Image created using AI.
Sources
Velten, C. (1903). Sitten und Gebräuche der Suaheli, nebst einem Anhang über Rechtsgewohnheiten der Suaheli. Vandenhoeck & Ruprecht. - Page 349
Bible: Mathew 7:10, Luke 11:11

Loading...
Loading...
Login to view and post comments
na Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥉 Mshindi wa Tatu
Ni mara ngapi umesikia Mchumia juani hulia kivulini? Hii ni methali ya kiswahili (kibantu) yenye maana ya kuwatia moyo watu katika shughuli mbalimbali wanazozifanya Kila siku wawe na Imani kuwa ipo siku watayafurahia matunda ya kazi yao. 

Methali hii huwapa watu nguvu, bidii, moyo, ujasiri, tumaini na weledi katika kufanya kazi. Mfanyakazi huamini kuwa baada ya kazi ngumu zenye surubu basi huleta mavuno mazuri yenye kumfanya astareheke kivulini akila matunda ya kazi yake. Shairi lifuatalo linaonesha kwa namna gani mchumia juani huwa katika majukumu ya Kila siku.

Siogopi jua wala mvua, nikiitengeneza kesho yangu
Siogopi maumivu Wala majeraha, maana yote ni ya muda
Jua kali na kazi ndiyo desturi yangu, ili kheri kuja maishani
Machinga,mkulima, makuli na mvuvi wao na jua, Ili kuitafuta kesho
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Ni mchana jua la utosi, kichwani nina mavuno, jasho linatiririka
Jua limezama Sasa kasia ufukweni, hoi kitandani, nyavu zi baharini
Nyumbani mtaa wa nne, nahodha wa familia surubu nivute  kheri
Jua Sasa la chomoza, Kiguu na njia kulitafuta tonge
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.

Bwana mmoja alikuwa mkulima. Maisha yake yote alitumia katika kilimo. Hivyo kupendeza kwake kulikuwa mara chache. Watu kijijini kwake walimuita mkulima stadi. Alijenga nyumba kwa kuuza sehemu ya mazao yake, alisomesha wanae kwa kilimo.

Bwana huyu alikuwa mtu mwenye bidii alijifunza siku zote kanuni za mkulima bora, hivyo kadri muda unavyokwenda mashamba yake alivuna mazao mengi. Watu wengi walistaajabu sana kuona mabadiliko makubwa ndani ya familia yake. Aliwekeza vitu vingi kijijini kwake, mashamba, nyumba, maduka na mifugo mingi vilitoka shambani.

Watu wengi walikuja kujichukulia hekima kwa mkulima stadi. Siku zote aliwaambia "Mchumia juani, hulia kivulini. Jembe limeniheshimisha kijijini Mimi na familia yangu. Maisha yangu sasa yanakwenda barabara kwa hakika niko kivulini nafurahia matunda ya kazi yangu ya juani. Mimi leo kijana wa mkulima huyo stadi najivunia malezi, uwajibikaji wake kwa sababu kazi za juani leo zimetufanya tupumzike na kula kivulini. Kwa hakika maana ya mchumia juani inaonekana kwa vitendo. Bidii yako ndilo jua lako na kivuli ndiyo matunda ya bidii yako.

Hadithi hii inashibishwa na hadithi ilee ya "Mabala the Farmer" yaani Mabala Mkulima iliyoandikwa na Richard S. Mabala(1989). 

Mabala alikuwa mfanyakazi bandarini Kisha akapunguzwa hivyo akachagua kurudi kijijini Morogoro. Mabala alikuwa mzembe,mlevi na mbishi. Mabala alikwenda shambani na galoni ya pombe alikunywa na kulala, alipoamka alimwongelesha mkewe lakni hakujibiwa zaidi ya  sauti ya jembe tik-tok, tik-tok .

Mabala alikuwa mbishi, alimwagilia sukari shambani alifikiri ni mbolea, lakni mwisho alibadilika na kuwa mkulima stadi akawa mchumia juani ili familia yake ije kulia kivulini. Je wewe unahisi Mabala ni mchumia juani? Ndani ya familia au kwenye jamii mkulima stadi anakupa picha gani?

Mwisho hadithi hii kutoka katika methali ya mchumia juani hulia kivulini hutuonyesha dira njema katika kila tunachokifanya katika maisha ya kila siku. Huku methali kama Subira yavuta kheri, Mgaa na Upwa hali wali mkavu zote hufanana kimaudhui, zipo katika kuipa jamii nguvu na matumaini kwa kila jambo lifanyikalo katika malengo.
...
Kwa kiingereza tunasema "One man's trash is another man's treasure," maana yake, kilichotupwa na mtu mmoja, kinaweza kutumikia mwingine na kuwa na thamani kwake.

Msemo huu hutumika ili kueleza jinsi mapendeleo ya watu hutofautiana, ama kuonyesha matumaini kwamba wanadamu ni wabunifu katika masuala ya kupanga upya au kuchakata vitu vilivyotupwa na wengine.

Kwa mfano, mjasiriamali Gibson Kiwago, mwanzilishi wa WAGA Tanzania, anachakata betri za laptop ili kuleta umeme kwa nyumba na maduka. Jifunze zaidi kuhusu E-Waste (Orodha ya Kusoma)!

Dhana kwamba thamani ya kitu hutegemea mtazamo wako ipo tangu zamani. Chimbuko cha msemo huu ni methali ya Kiingereza iliyotumika karne ya 17:
One man's meat is another man's poison
Nyama na mtu mmoja ni sumu ya mtu mwengine

Je umewahi kuona thamani katika kitu kilichotupwa na mwengine?
...
Updated 5mo ago
by
As the appetite increases, food tastes better.

The proverb first appeared in Miguel de Cervantes' Don Quixote, published in 1615 (in Part II, Chapter V)

Parents often say this to their children when they are fussy eaters.
...
Updated 5mo ago
by
na Nankya Sauda 🇺🇬
Shindano la Insha ya Methali 🏆
Mshindi wa Kwanza 🥇

Maji yaliyotulia ndiyo yenye kina kirefu

Umewahi kuchukua muda na kujiuliza kwa nini wazee huwa wana busara zaidi kuliko vijana? Je, umewahi kuchukua muda wa kutafakari asili yako ulipochipuka? Ikiwa sivyo, [sasa] ni wakati mzuri wa kuanza kutafuta asili yako kwa sababu ni muhimu mtu ajue mizizi yake.
   Baada ya muda, unachukua mzigo wa kufunua asili ya watu mashuhuri wenye akili na haiba zao, utakuja kutambua kwamba wao ni introverts (yaani wakimya, wanaopenda kukaa peke yao/kujitenga) lakini ni mashuhuri. Ni muhimu uchukue muda wako, hata ukiwa bize, ujifunze kuhusu wasomi mashuhuri kama Albert Einstein, mwanasayansi mashuhuri ambaye alisema nukuu inayotuelimisha:
"Maisha tulivu ya upweke yasiobadilikaa huchochea akili na fikra bunifu."

Hii inamaanisha kwamba wakati ukiwa peke yako ni nafasi ya kujitafakari, lakini pia ni nafasi ya kutumia akili yako bunifu. Wanasema wazungumzaji wakubwa ni wanasheria wazuri, na tumeona hayo katika maisha yetu ya kila siku ambapo watu hutoa ahadi tupu, hutoa matamko ya uwongo ili kuwapendeza waliomzunguka bila kuchukua muda wa kufanya kitu kwa nia ya kutekeleza maneno yao. Kwa sababu hiyo, wengi wamepoteza imani na hawa wanaoitwa “wazungumzaji wakubwa.”
   Kwa upande mwingine, wakimya hutushangaza kwa matendo yao. Hatua zao hupangiliwa kila mara, matamanio yao ni wazi na vitendo vyao hufanyika kwa kusudi. Wapenzi wakimya hukuza mahusiano yao ya kimapenzi kwa ubunifu mpya ili kudumisha mahusiano. Waliowaajiri [wakimya] na waliokaa karibu na introverts husema kuwafahamu ni moja ya mafanikio makubwa katika maisha yao, ndo maana hawa wamefanya kazi nadhifu zaidi, wakawa na vipindi vyao vya kutafakari peke yao, na hatimaye walitoa kazi bora na kupata cheo kikubwa.
   Tunaweza kufafanua methali kama misemo inatumika katika nchi au utamaduni fulani. Ni maneno mafupi yenye busara na hutoa ushauri na vile vile kuongeza wazo kuhusiana na maisha ya kila siku. Kwa kweli, ili kufahamu kwa kina mila na desturi za kitamaduni, ni vizuri warejelee methali kwani zinaweza kuwa na maana pana ndani. 
Kihistoria, methali "Still waters run deep" (Maji yalotulia ndo yenye kina kirefu/Usicheze maji yanayosimama) inatoka Kilatini cha kale. Ilipata umaarufu baada ya Shakespeare kuitumia katika tamthilia yake ya Henry VI mwaka 1590. Alisema:
"Maji hutulia pale ambapo mto una kina kirefu."

Tunatambua kwamba, mara nyingi watu hatari zaidi walio na roho mbaya hupanga hatua zao na kuchukua hatua kwa wakati ambao wengine hatarajii. Ndio maana usaliti hutoka kwa watu ambao hatutarajii [kitu kama hicho] kutoka kwao. Kwa hiyo ni muhimu kwa mtu kuchukua si tu yale yanayokutana na macho bali pia kuchukua tahadhari hasa kutoka kwa watu ambao hawalipizi kisasi mara tu baada ya kukasirishwa au kukabiliwa.
   Albert Einstein licha ya tabia yake ya kujittenga, yeye anajulikana sana kwa kubuni nadharia yake ya relativity ambayo ilileta mapinduzi katika uelewa wetu wa nafasi ya nje, wakati, na kanimvutano (gravity).
   Kwa kumalizia, ni muhimu sana kutofikia hitimisho [haraka] kwa sababu sura hudanganya na kuna mengi ya kujua na kugundua kuliko macho yanavyoweza kuona.
...
Updated 5mo ago
by