You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Taarifa
Majadiliano
Methali
Usilolijua ni kama usiku wa giza
ili kupiga kura
Kura
13
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
Marejeleo

Chimbuko:

Methali ya kiswahili kutoka kitabu cha “METHALI ZETU” cha Oxford inayosema “USILOLIJUA NI KAMA USIKU WA GIZA.”  

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishika nafasi ya nne katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Ibrahim Methusela Nyanda ni Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Ibrahim Nyanda
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Meaning it's better to be satisfied with what you have, rather than risking it for a chance at a larger reward.

This proverb turns out to be very old indeed. It comes from an ancient book called "The Story of Ahikar" also known as the "Proverbs of Ahiqar." 
My son, a sheep's foot in thine own hand is better than the whole shoulder in the hand of a stranger; better is a lambkin near thee than an ox far away; better is a sparrow held tight in the hand than a thousand birds flying about in the air; better is a hempen robe, that thou hast, than a robe of purple, that thou hast not.
The Story of Ahikar (page 110)
The book tells the story of an advisor to the ancient Assyrian and Egyptian rulers. It was probably written about 600 BCE, with the earliest surviving fragments dating to about 500 CE. 

Similar proverbs from around the world...
French:
Un tiens vaut mieux que deux tu l'auras
A here-you-go is worth more than two you-can-have-it-laters
Japanese
明日の百より今日の五十
Today's 50 over tomorrow's 100
Italian
Meglio un uovo oggi che una gallina domani
Better an egg today than a hen tomorrow

And one more for fun...
"A monkey on the back is worth two in the bush."
-ChatGPT

Do you think this proverb is good advice? When is it better to go with a sure thing now or take a chance and search for something better?
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Huwa tunatendewa kama tunavyowatendea wengine. Kwa kawaida methali hii hutumika kama onyo, au wakati mtu mbaya anapata alichostahili. Lakini pia inaweza kutumika kama tumaini la baraka kwa wale wanaofanya mema. Chimbuko halisi cha methali hiyo haijulikani, lakini ilianza Amerika miaka za 60 hivi. Inaendana na kanuni la Karma katika dini ya Kihindi.

Methali na nukuu zinazohusiana:
Shakespeare
Bado tunayo hukumu hapa (duniani);
Tunafundisha tu umwagaji damu, ambayo, ukifundishwa, hurudi
ili lipiza kisasi na kumtesa mvumbuzi: mkono wa haki
huweka viungo vya kikombe chetu cha sumu
Kwa midomo yetu wenyewe.  ( Makbeth Act I, Scene 7 )
Biblia:
Chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna ( Wagalatia 6:7 )
Kichina: 
善有善報,惡有惡報
Wema hulipwa kwa wema, na ubaya kwa ubaya. 
Kijerumani:
Wie man in den Wald hineinruft, so schallt es heraus
Unacholia msituni, kitasikika tena
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Kuna vitu ambavyo huwezi kufanya peke yako. Tango ni mchezo (densi) ya watu wawili, kwa hivyo huwezi kucheza tango peke yako.

Methali hii inatoka wimbo ulioimbwa 1952, It Takes Two to Tango:
Unaweza kusafiri kwa meli peke yako,
kulala au kupumzika peke yako.
Unaweza kuingia kwenye deni peke yako.
Kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya peke yako.
Lakini ni lazima muwe wawili ili kucheza tango, muwe wawili ili kucheza tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning na Pearl Bailey) Ona vyanzo/sources ili kusikiliza wimbo huu!

Methali hii ina maana nyingi tofauti ambazo unaweza kutekeleza katika mahusiano na maisha yako ya kila siku. Mambo mengi huhitaji watu zaidi ya mmoja: Wawili wanatakiwa ili kushirikiana, kufanya biashara ama kupigana. Ukitaka kucheza na mtu ambaye hataki kucheza na wewe, bora kumtafuta mchezaji mwengine.. Vivyo hivyo, ukiwa kwenye mgogoro au magomvi, itabidi ufikirie jinsi tabia yako inavyoweza kuchangia katika kuendeleza shida. katika dance, lengo si kuwa mkamilifu, bali ni kuendana na mwenzako na kufurahia pamoja.
Methali zinazofanana kutoka Afrika: 
Kimisri (Kiarabu): 
ايد لوحدها ماتسقفش‎
Mkono mmoja hauwezi kupiga makofi
Kiswahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Kidole kimoja hakiuwi chawa
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Methali hii inahusiana na tabia ya kufikiria kwamba watu wengine wana vitu vizuri zaidi, hali nzuri zaidi nk... Kwa mfano kufikiri jirani yako ana majani mazuri kuliko wewe.

Chanzo cha methali hii ni "Sanaa ya Upendo" na Ovid, kitabu cha mashairi yaliyotungwa ili kutoa shauri kwa wanaume na wanawake kuhusu kutafuta na kudumisha mahusiano ya kimapenzi. Kitabu hiki kiliandikwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita, takribani 2 KK:
Watu hutaka furaha mpya. Huwa tunaona kuwa watu wengine wana bahati zaidi kuliko sisi wenyewe. Mazao daima ni bora katika shamba la jirani yetu; ng'ombe wake hutoa maziwa zaidi. 
 - Ovid Ars Amatoria (Sanaa ya Upendo), Ukurasa wa 24

Kwa upande mmoja, methali hii inamaanisha, bora kushika kile ulicho nacho, na kupuuza kile ambacho wengine wanacho, hata kama inaonekana ni bora zaidi. Lakini pia kwa mtazamo mwengine, inamaanisha bora kutumia akili yako katika kuboresha hali yako mwenyewe (kama kumwagilia shamba lako) badala ya kufikiria sana ukweli kwamba shamba lako, au hali kwa ujumla, ni duni. Methali nyingine ni "Majani huonekana ya kijani zaidi pale ambapo yalipomwagiliwa maji." 

Methali zinazofanana kikanuni:
Kihindi: 
दूर के ढोल सुहावने लगते हैं
Ngoma za mbali husikika vizuri
Kichina: 
隔籬飯香 
Wali wa jirani hunukia vizuri
Kijapani:
隣の芝生は青く見える
Majani ya jirani huonekana kijana zaidi
Kurusi:
соседняя очередь всегда движется быстрее
Foleni nyingine husogea kwa kasi zaidi
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by