You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

New announcements
Discussions
Proverbs
Mchumia juani, hulia kivulini
Join
or login
to VOTE
Votes
59
View this proverb in English
Work in the sun, eat in the shade
na Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥉 Mshindi wa Tatu
Ni mara ngapi umesikia Mchumia juani hulia kivulini? Hii ni methali ya kiswahili (kibantu) yenye maana ya kuwatia moyo watu katika shughuli mbalimbali wanazozifanya Kila siku wawe na Imani kuwa ipo siku watayafurahia matunda ya kazi yao. 

Methali hii huwapa watu nguvu, bidii, moyo, ujasiri, tumaini na weledi katika kufanya kazi. Mfanyakazi huamini kuwa baada ya kazi ngumu zenye surubu basi huleta mavuno mazuri yenye kumfanya astareheke kivulini akila matunda ya kazi yake. Shairi lifuatalo linaonesha kwa namna gani mchumia juani huwa katika majukumu ya Kila siku.

Siogopi jua wala mvua, nikiitengeneza kesho yangu
Siogopi maumivu Wala majeraha, maana yote ni ya muda
Jua kali na kazi ndiyo desturi yangu, ili kheri kuja maishani
Machinga,mkulima, makuli na mvuvi wao na jua, Ili kuitafuta kesho
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Ni mchana jua la utosi, kichwani nina mavuno, jasho linatiririka
Jua limezama Sasa kasia ufukweni, hoi kitandani, nyavu zi baharini
Nyumbani mtaa wa nne, nahodha wa familia surubu nivute  kheri
Jua Sasa la chomoza, Kiguu na njia kulitafuta tonge
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.

Bwana mmoja alikuwa mkulima. Maisha yake yote alitumia katika kilimo. Hivyo kupendeza kwake kulikuwa mara chache. Watu kijijini kwake walimuita mkulima stadi. Alijenga nyumba kwa kuuza sehemu ya mazao yake, alisomesha wanae kwa kilimo.

Bwana huyu alikuwa mtu mwenye bidii alijifunza siku zote kanuni za mkulima bora, hivyo kadri muda unavyokwenda mashamba yake alivuna mazao mengi. Watu wengi walistaajabu sana kuona mabadiliko makubwa ndani ya familia yake. Aliwekeza vitu vingi kijijini kwake, mashamba, nyumba, maduka na mifugo mingi vilitoka shambani.

Watu wengi walikuja kujichukulia hekima kwa mkulima stadi. Siku zote aliwaambia "Mchumia juani, hulia kivulini. Jembe limeniheshimisha kijijini Mimi na familia yangu. Maisha yangu sasa yanakwenda barabara kwa hakika niko kivulini nafurahia matunda ya kazi yangu ya juani. Mimi leo kijana wa mkulima huyo stadi najivunia malezi, uwajibikaji wake kwa sababu kazi za juani leo zimetufanya tupumzike na kula kivulini. Kwa hakika maana ya mchumia juani inaonekana kwa vitendo. Bidii yako ndilo jua lako na kivuli ndiyo matunda ya bidii yako.

Hadithi hii inashibishwa na hadithi ilee ya "Mabala the Farmer" yaani Mabala Mkulima iliyoandikwa na Richard S. Mabala(1989). 

Mabala alikuwa mfanyakazi bandarini Kisha akapunguzwa hivyo akachagua kurudi kijijini Morogoro. Mabala alikuwa mzembe,mlevi na mbishi. Mabala alikwenda shambani na galoni ya pombe alikunywa na kulala, alipoamka alimwongelesha mkewe lakni hakujibiwa zaidi ya  sauti ya jembe tik-tok, tik-tok .

Mabala alikuwa mbishi, alimwagilia sukari shambani alifikiri ni mbolea, lakni mwisho alibadilika na kuwa mkulima stadi akawa mchumia juani ili familia yake ije kulia kivulini. Je wewe unahisi Mabala ni mchumia juani? Ndani ya familia au kwenye jamii mkulima stadi anakupa picha gani?

Mwisho hadithi hii kutoka katika methali ya mchumia juani hulia kivulini hutuonyesha dira njema katika kila tunachokifanya katika maisha ya kila siku. Huku methali kama Subira yavuta kheri, Mgaa na Upwa hali wali mkavu zote hufanana kimaudhui, zipo katika kuipa jamii nguvu na matumaini kwa kila jambo lifanyikalo katika malengo.
Sources

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishinda nafasi ya tatu 🥉 katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Magreth Lazaro Mafie ni mwanafunzi Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Magreth Lazaro Mafie
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org

The original essay included the following image, which is not included in the Creative Commons license.
Mchoro huu na / This image from: Honey Bee Arts - YouTube


Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Hapo zamani za kale, palikuwa na binti mrembo, mkarimu, mwenye akili aliyeitwa Poshia. Wanaume wengi walitaka kumuoa na walikuja ili kuomba uchumba. Baba Poshia alikuwa amefariki dunia. Alikuwa tajiri na aliacha wosia ulioelekeza kamba yeyote aliyetaka kumuoa Poshia, lazima achague kati ya masanduku tatu: sanduku la dhahabu, sanduku la fedha na sanduku la risasi. Atakayechagua sahihi ndiye atakayeruhusiwa kumuoa Poshiia na kurithi mali zote za Baba Poshia. Siku moja, Mfalme wa Moroko alikuja ili kuomba uchumba.

Mabepari wa Venisi

Tazama ▶️ YouTube


POSHIA: Kayavute mapazia masanduku yaonekane kwake mtukufu huyu mtoto wa mfalme. Haya sasa kachague.

MOROKO: La kwanza, ni la dhahabu, lenye maandiko haya:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
Na la pili, ni la fedha, linaloahidi hivi: 
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
La, tatu, risasi butu, na onyo lake ni butu:
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
Nitajuaje yakuwa nimechagua vizuri?

POSHIA: Moja lina picha yangu, mzawa wa mfalme: Ukilichagua hilo basi na mimi ni wako.

MOROKO: Muungu Fulani uniongoze. Hebu nione; nitayachagua tena maandiko toka mwisho. Nitaanzia la tatu: lasemaje, la risasi?
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
Itambidi atoe - atoleeni? Risasi? Na pia ahatarishe - kwa ajili ya risasi? Sanduku hili latisha: wahatarishao vyote hutumaini kupata faida iliyo nzuri: Wenye moyo wa dhahabu hawajali takataka; Kwa hiyo basi sitoi na wala sihatarishi chochote nilicho nacho kwa sababu ya risasi. La fedha lasema nini, lenye rangi ya baridi?
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
Apate astahilicho! Subiri hapa, Moroko. Upime thamani yako kwa mkono wa mwadilifu: Kama ukithaminiwa vile ujifanidivyo wastahili kutosha; walakini ya kutosha inaweza isitoshe kumpata siti huyu. Bali nikitia shaka kuwa simstahili,Basi hapo nitakuwa najiumbua mwenyewe. Stahili yangu ni nini? Bila shaka ni bibie. Namstahili, hakika, kwa nasaba na kwa mali, kwa madaha na kwa sifa zote za malezi mema na kuzidi yote hayo namstahili kwa pendo. Vipi, nisiendelee, nichague papa hapa?
Hebu tuyaone tena ya sanduku la dhahabu:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Naam, ni siti huyu; anotamaniwa kote. Toka pande zote nne za dunia wanakuja kubusu sanamu hii takatifu ilo hai: Majangwa ya Hirikani na nyika pana ajabu, za Uarabuni kote, sasa zimekuwa njia ziletazo watawala kumwona Poshia bora. Nayo dola ya bahari ambayo inapofura hutemea hata mbingu, haiwezi kuzuia nia ya wageni hao; ila wanazidi kuja, kama wavuka kijito, kumwona Poshia bora. Moja la matatu haya lina picha yake nzuri. Itawezekana kweli liwe lile la risasi? Wazo chafu kama hilo lingekuwa ni laana. Halifai japo kuwa sanda yake ya kaburini.
Au niwaze ya kuwa kawekwa ndani ya fedha? Moja ya kumi na moja ya thamani ya dhahabu? Hilo ni wazo la dhambi! Kito cha thamani hivi hakiwekeki po pote ila ndani ya dhahabu. Uingereza wanayo sarafu tu ya dhahabu, ambayo kwa juu yake imechapwa malaika. Bali hapa malaika mwenyewe hasa yu ndani ya sanduku hili hapa, na bahati nijaliwe!

POSHIA: Ni huu hapa, chukua, mzawa wa mfalme; kama sura yangu imo nimekuwa mali yako.

[Anafungua sanduku la dhahabu]
MOROKO: Mama yang! Nini hii? Ni fuu tupu la kichwa, ambalo katika jicho lina hati ma’ndiko. Nitasoma maandiko.
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.
Nimefarikiwa kweli. Bure nimejitanibu. Basi buriani, joto; nawe, makiwa, karibu. Basi kwa heri Poshia. Ninayo
huzuni sana siwezi kwa heri ndefu: Ndivyo wanavyoagana watu waliopoteza.
[Aondoka na Wafuasi wake. Tarumbeta]
...
Updated 4mo ago
by
It’s a simple and profound truth about human relationships: Making a promise means creating an expectation in others. When we fail to keep our promises, we damage our relationships and our reputation. Next time you make a promise, ask yourself, "Would I sign a contract that said this?"

French
Chose promise, chose due 
A thing promised is a thing owed. 
Russian:
Долг платежом красен, а займы отдачею. 
The beauty of a debt is its payment 
Alternative translation: A debt is beautiful when it is paid off, and loans when repaid.
Latin:
Pacta sunt servanda
Agreements must be kept (an important principle of international law)
Chinese
口說無憑
Spoken words are no guarantee.
English
Your word is your bond

What do you think? Is a promise as strong as a contract?
...
Updated 4mo ago
by
Kwa kiingereza tunasema "One man's trash is another man's treasure," maana yake, kilichotupwa na mtu mmoja, kinaweza kutumikia mwingine na kuwa na thamani kwake.

Msemo huu hutumika ili kueleza jinsi mapendeleo ya watu hutofautiana, ama kuonyesha matumaini kwamba wanadamu ni wabunifu katika masuala ya kupanga upya au kuchakata vitu vilivyotupwa na wengine.

Kwa mfano, mjasiriamali Gibson Kiwago, mwanzilishi wa WAGA Tanzania, anachakata betri za laptop ili kuleta umeme kwa nyumba na maduka. Jifunze zaidi kuhusu E-Waste (Orodha ya Kusoma)!

Dhana kwamba thamani ya kitu hutegemea mtazamo wako ipo tangu zamani. Chimbuko cha msemo huu ni methali ya Kiingereza iliyotumika karne ya 17:
One man's meat is another man's poison
Nyama na mtu mmoja ni sumu ya mtu mwengine

Je umewahi kuona thamani katika kitu kilichotupwa na mwengine?
...
Updated 4mo ago
by

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Updated 4mo ago
by