You are now browsing in English. Switch to Swahili
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiingereza. Rudi kwa Kiswahili"
You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 5mo ago
by

Swali: Je, umejifunza zaidi kutoka kwa wazazi wako ama kupitia uzoefu wako ulimwenguni?


Methali hii hutumika wakati mtu amekosa na kupata madhara, haswa kama ameonywa... kama vile dereva wa lori katika picha hii (kutoka Oxfordshire, Uingereza). Bila kujali kama ulifunzwa na wazazi, hatimaye lazima ukabiliane na ukweli wa maisha halisi. Ona pia: Mtoto akilia wembe, mpe

Kuna shairi lililotungwa na Akilimali Snow-White juu ya methali hii:

ASOFUNZWA NA WAZAZI, HUFUNZWA NA ULIMWENGU
na Akilimali Snow-White

Zama walinipumbaza, wazee kwa kunilea,
Nikashindwa kujifunza, myendo mipya ya dunia,
Leo najipendekeza, kwa walimwengu sikia,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Kazi zote singeweza, bila kuwanyenyekea,
Kutii kuwembeleza, kisha kuwatumikia,
Hata nikawapendeza, wakanifunza kwa nia,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Sasa kusema naweza, Kizungu bila udhia,
Kama vile Kingereza, na lugha zingine pia,
Kwa juhudi najifunza, hata zimenielea,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Naweza kuzungumza, pasipo kutia doa,
Na paovu kuongoza, doa nikaliondoa,
Mwishowe pakapendeza, lingano moja hatua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Sina nilipopasaza, pasina kupachungua,
Pande zote hachunguza, marifa nikachukuwa,
Hata najua kuuza, bidhaa na kununua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Kiasi nilo jifunza, si haba kwa kubabia,
Nitokapo napendeza, kazi njema natumia,
Ni vigumu kuibeza, jinsi inanielea,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Haifai kupuuza, kwa kitu usicho jua,
Jaribu kupeleleza, na kisha ukichungua,
Nia unap,o ikaza, hushindwi kitu kujua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Kazi nilizojifunza, babangu hakuzijua,
Hakujua Kingereza, kuuza na kununua,
Bali kujipendekeza, ndipo mwana nikajua,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

Nawatilia nyongeza, mlio nisaidia,
Nyote mlionifunza, Rabi awape afia,
Mungu heri tawajaza, mema kuwarudishia,
Asofunzwa na wazazi, hufunzwa na walimwengu.

- Diwani ya Akilimali

Fikeni E. M. K. Senkoro (1988) aliandika juu ya shairi hili:
[M]tu hawezi kupata uzoefu wa mambo yote yahusuyo maisha kutoka kwa wazazi wake: lazima awe tayari kufunzwa na ulimwengu, yaani kujifunza kutoka kwa wengine zaidi ya baba na mama yake. 

Nimejitahidi kutafsiri shairi hili kwa Kiingereza, na nitashukuru sana sana kupata feedback zenu, ndugu wajuaji wa Kiswahili na Kiingereza. (Someni hapa.)

Mnafikiriaje? Shairi hili lina maana gani kwako? 
Sources
Picha ni kweli, inaonyesha ajali iliyotokea Uingereza, mkoa wa Oxfordshire, (Pich kutoka mitandao ya kijamii) - Soma pia Makala hii ya BBC

Shairi lilitoka Diwani ya Akilimali

Nukuu ya mwisho inatoka kitabu cha "Ushairi - Nadharia na Tahakiki" na F.E.M.K. Senkoro, Sura ya 7 (Dar Es Salaam University Press, 1988, ISBN 9976 60 0224)  
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
This proverb refers to the tendency to imagine or dwell on the notion that other people have nicer things...like your neighbor having a nicer lawn. 

The original source of this proverb is Ovid's "Art of Love", a book of advice for men and women about finding and keeping romantic relationships, written over 2000 years ago, about 2 AD:
People don't resist the temptation of new delights. We always deem that other people are more fortunate than ourselves. The crop is always better in our neighbour's field; his cows more rich in milk.
- Ovid The Art of Love, Page 24

One lesson from this proverb is to focus more on what you have, ignoring what others may have that is better. Another lesson might be to put your attention on improving your own situation (like watering your lawn) rather than dwelling on the fact that your lawn (or situation in general) is inferior.

An interesting variation on this proverb is: "The grass is always greener where you water."

Similar proverbs from other cultures:

Hindi:
दूर के ढोल सुहावने लगते हैं
From far away the drums sound better
Chinese:
隔籬飯香
Next door's rice smells good 
Japanese:
隣の芝生は青く見える
The neighbor's grass seems green 
Russian:
соседняя очередь всегда движется быстрее
The other queue always moves faster 



...
Updated 5mo ago
by
Have you ever noticed that time seems to pass more slowly when you are waiting for something? On the other hand, if you distract yourself with other engaging activities, time goes by quickly.

For example, if you're in a waiting room for a doctor, the wait will seem shorter if you check your phone or read a magazine, rather than just waiting for your name being called.

This proverb was attributed by Benjamin Franklin to Poor Richard's Almanac, however it doesn't actually appear there. Instead, Franklin used it in an essay on animal magnetism in 1785.

I was very Hungry; it was so late; “a watched pot is slow to boil,” as Poor Richard says.

...
Updated 5mo ago
by
Umewahi kuona mhunzi akifanya kazi? Au labda ulimwoma fundi akitengeza glass (kioo)? Si ni ajabu sana? (Ukitaka kuona kwa macho yako, tembelea Shanga Foundation Arusha, au tazama videos kwenye links hapo chini - ona Rasilimali).

Katika uzoefu wetu, glasi ni ngumu, yaani haikunji kabisa. Ukitumia nguvu zako zote, kio kitavunjika mkononi mwako na kukuumiza. Lakini hakika kioo hutengenezwa kwa kuyeyusha mchanga, mabichi na laini kama udongo.

Maishani kuna mambo ambayo yanaonekana kuwa magumu, yaani hayabadiliki kabisa, hayapindi. Tukitumia nguvu zetu zote, yataharibika tu na kutuumiza. Lakini fundi mwenye ujuzi anaweza kuyafanya kuwa mepesi na laini, kwa kuyatayarisha ipasavyo, na kuchukua hatua sahihi kwa wakati ufaao.

Methali hii hutumika sana kwa maana "chukua hatua haraka fursa inapotokea, ili usiikose." Kama WaSwahili wanavyosema "Samaki mkunje angali mbichi." Ona pia There is a tide:
Majambo ya binadamu yana kujaa na kupwa, Yakidakwa yamejaa huongoza ushindini; yakipuuzwa, safari yote ya maisha yao haiachi maji mafu, na hujaa madhilifu.
- BURUTO katika Juliasi Kaizari, na William Shakespeare (ilitafsiriwa na Mwalimu Nyerere)
Hata hivyo, ikumbukwe kwenye tamthilia hii, ushauri huu ulikuwa na madhara mabaya kwake, maana Buruto hakushinda baada ya hotuba hii (soma zaidi...)

Lugha na tamaduni nyingi zina methali zinazofanana sana na hii. Labda methali hizo zina chimbuko nyingi tofauti zisizotegemeana. 

KiChina: 趁熱打鐵
KiThai: ตีเหล็กเมื่อแดง
KiHindi: लोहा गरम हैं. मार दो हथौड़ा.
KiGaelic (Ireland): buail an t-iarann te
Kiingereza: Strike while the iron is hot.

...

Picha: Walimu wa Elimu Yetu wakijifunza ufundi wa kioo wakitemeblea Shanga, Arusha, Tanzania

Updated 5mo ago
by
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
...