We built 3 pickleball courts in Arusha, Tanzania
Book a court Learn pickleball for FREE Hire a Pickleball coach
You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

New announcements
Discussions
Proverbs
Usilolijua ni kama usiku wa giza
Join
or login
to VOTE
Votes
16
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
Sources

Chimbuko:

Methali ya kiswahili kutoka kitabu cha “METHALI ZETU” cha Oxford inayosema “USILOLIJUA NI KAMA USIKU WA GIZA.”  

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishika nafasi ya nne katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Ibrahim Methusela Nyanda ni Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Ibrahim Nyanda
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Methali hii inatoka Kiingereza "A penny saved is a penny earned." Maana yake, mia inayobaki mfukoni inaweza kutumiwa kwajali ya madhumuni mengine. Mifano: Inaweza kutumika kwaajili ya kununua kitu kingine, unaweza kukopesha au kuwekeza ili kuingiza riba au pesa zaidi katika siku zijazo. Katika uchumi, kanuni hii inaitwa Opportunity Costs (gharama za kukosa fursa). Tunapotumia pesa au muda kwa jambo limoja, tunapoteza pia fursa ya kuzitumia kwajili ya jambo lingine.

Methali hii huhusishwa na Benjamin Franklin, lakini si chimbuko halisi, wala hakuandika msemo huu kamili. Misemo karibu na huu ilichapishwa kabla yake. Kwa mfano: 

A penny spar'd is twice got.
Senti iliyookolewa hupatikana mara mbili.
- Outlandish Proverbs by George Herbert (1640)  
 
Katika Poor Richard's Almanac (1736), Benjamin Franklin alinukuu methali hii na alifafanua vizuri kanuni ya Opportuinty Cost hivi:

Vidokezo kwa Wale Wanaotaka kuwa Matajiri

Matumizi ya pesa ndiyo faida zote zinayopatikana ukiwa na pesa.
Kwa pound [£] sita kwa mwaka [yaani riba] unaweza kutumia  £ mia [yaani kupitia mkopo], kama unajulikana kama mwaminifu na mwenye busara.
Anayetumia groat [senti 4] kwa siku bure, hutumia pound ÂŁ zaidi ya sita kwa mwaka, ambazo ni bei ya kujipatia matumizi ya pound ÂŁ mia moja.
[Kwa hivyo] Anayepoteza muda wake wa thamani ya groat [senti 4] kwa siku, siku moja na nyingine, anapoteza fursa ya kutumia pound mia moja kila siku.
Anayepoteza muda wa shilingi tano kwa uvivu hupoteza shilingi tano, ni kama amezitupa tu baharini.
Anayepoteza shilingi tano sio tu kwamba anapoteza kiasi hicho, bali anapoteza pia faida yote ambayo ingeweza kupatikana kwa kuzitumia katika shughuli zake, ambayo, akiwa kijana, wakati wa uzee ingefikia kiasi kikubwa cha fedha.
Tena: anayeuza kwa mkopo huongeza bei ya kile anachokiuza kwa kiasi sawa riba angaliingiza na pesa hizo kwa kipindi ambacho atazikosa. Kwa hivyo, anayenunua kwa mkopo hulipa riba kwa kile anachonunua, na anayelipa pesa mara moja kwa kila anachonunua hukoa fursa ya kuzikopesha kwa wengine, kwa hivyo aliye na kitu alichonunua ameshalipa riba kwa matumizi yake.
Hata hivyo nasema kulipa mara moja unaponunua ni bora, kwa sababu anayeuza kwa mkopo anatarajia kupoteza asilimia tano ya mikopo; kwa hivyo anaongeza bei ya kile anachokiuza kwa asilimia ileile ili kuzuia hasara. Wanaolipa kwa mikopo hulipa kodi mara moja. Anayelipa kwa pesa mara moja anaweza kuzuia kodi hii
"Senti iliyohifadhiwa ni senti mbili hakika;
[haba] kwa siku ni [nne] kwa mwaka."
 
Basi, unapofikiria kutumia muda au pesa zako katika jamblo fulani, jiulize, ningekosa, ningepata fursa zipi? Pesa hizi zingeweza kutumikia vipi? Mifano: kumkopesha mwingine, kurudisha madeni uliyonayo, kubuni kitu kipya au kuwekeza katika kitu ambacho kinaweza kuleta faida kubwa mbeleni.
...
Updated ~1y ago
by
Kila kazi kubwa katika maisha huhitaji kufanyika kwa hatua ndogo, siku baada ya siku. 

Je, unajua methali zingine zinazofanana na hii au zinazotoa dhana hiyohiyo? 

Msemo huu unakumbusha shairi liitwalo "Vitu Vidogo" na Julia Abigail Fletcher Carney: 
Matone madogo ya maji,
Chembe kidogo za mchanga, 
hutengeneza bahari kubwa
Na ardhi ya kupendeza

Vivyo hivyo zile dakika ndogo,
ingawa ni ndogo,
hutengeneza enzi za milele. 
Julia Carney alitunga shairi hili mwaka wa 1845 darasani akiwa mwanafunzi darasani -- na alipewa dakika 10 tu kuliandika!
...
Updated ~1y ago
by
by Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Proverb Essay Contest 
🥉 Third Place Winner
(English translation from Kiswahili)
How many times have you heard “Mchumia juani hulia kivulini” (One who works in the sun, eats in the shade). This is a Swahili (Bantu) proverb meant to encourage people in their everyday activities, to have faith that there will be a day when they will enjoy the fruits of their work.

This proverb gives people strength, diligence, heart, courage, hope and skill in working. The worker believes that hard work brings a good harvest that will allow him to relax in the shade as he eats the fruits of his labor. 

The following poem shows “One who works in the sun” in their daily responsibilities.
I fear neither sun nor rain, making my tomorrow
I fear neither injuries nor pain, because all are temporary
Scorching sun and work are my custom, so that happiness comes in life
The street vendor, the farmer, the [port boys] and their fisherman and the sun, in search of tomorrow
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

It's noon, the sun overhead, in my head I have the harvest, sweat is dripping,
The sun has set now, the oar on the beach, exhausted in bed, nets in the sea,
At home on fourth street, captain of the family, may I pull happiness from hard labor
Now the sun is rising, walking the path to look for a bite,
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

Once there was a farmer. He spent his whole life in agriculture. Thus his times for pleasure were few. People in his village called him a skilled farmer. He built a house by selling part of his crops, he educated his children through farming.

This farmer was a diligent man, he always learned the principles of being a good farmer, so as time went by, he harvested many crops from his fields. Many people were really amazed to see the big changes in his family. He made many investments in his village, the farms, houses, and shops, and many livestock came from his farm.

Many people came to take wisdom from the skilled farmer. He always told them "One who works in the sun, eats in the shade. The hoe has given me respect in the village, me and my family. My life now is going on a path of certainty, I am in the shade, enjoying the fruits of my labor in the sun. I, the son of that skilled farmer, am proud of my upbringing, and his responsibility, because work in the sun today has made us rest and eat in the shade. The true meaning of “he who works in the sun” can be seen in actions. Your diligence is your sun and the shade is the fruit of your diligence.

This story is complemented by the story of "Mabala the Farmer" by Richard S. Mabala (1989). Mabala was a port worker then he was demoted, so he chose to return to the village of Morogoro. Mabala was careless, drunk and obstinate. Mabala went to the farm with a gallon of booze, he drank it and went to sleep, when he woke up, he called out to his wife but there was no answer except the sound of the hoe tik-tok, tik-tok.

Mabala was obstinate, he watered the fields with sugar, thinking it was fertilizer, but in the end he changed to become a skilled farmer, becoming “one who works” in the sun so that his family could eat in the shade. Do you feel that Mabala is “one who works in the sun”? In the family or in the community, what’s your image of a skilled farmer?

In conclusion, this story on the proverb "Work in the sun, eat in the shade" shows us a good vision in everything we do in our daily lives. Also proverbs like "Subira yavuta kheri” (Patience brings blessings), "Mgaa na Upwa hali wali mkavu” (He who combs the beach at low tide doesn’t eat dry rice) all have similar themes; they exist to give the community strength and hope each task undertaken to pursue their goals.

...
Updated ~1y ago
by

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Updated ~1y ago
by