You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Taarifa
Majadiliano
Methali

Ukitaka cha uvunguni sharti uiname

Ili kupiga KURA kwa Methali ya Mwezi
Kura
0
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Methali yetu ya leo inasemwa pia kama:
Mtaka cha mvunguni sharti ainame
Methali hii hutumika kuwahimiza watu kufanya kazi kwa bidii na kujitahidi. Hatupaswi kutarajia kupata vitu tunavyotafuta isipokuwa tumekubali kuvitafuta katika mahali ambapo ni vigumu kupafikia.

Hapa kuna hadithi fupi inayoeleza methali hii, juu ya Mulla Nasreddin, mhusika mcheshi katika ngano za Kisufi.
Mulla [Nasreddin] alikuwa amepoteza pete yake sebuleni. Aliitafuta kwa muda, lakini kwa kuwa hakuipata, alitoka nje hadi uani na kuanza kuchungulia pale. Mkewe, ambaye aliona alichokifanya, akamwuliza: “Mulla, umepoteza pete yako sebuleni , kwa nini unaitafuta uani?” Mulla alishika ndevu zake akisema: “Chumbani kuna giza na sioni vizuri. Nilitoka nje kwenda uani ili kutafuta pete yangu kwa sababu kuna mwanga mwingi zaidi hapa.
- Usimulizi wa Houman Farzad. Imetafsiriwa kwa Kiingereza kutoka lugha ya Kiajemi na Diane L. Wilcox (1989), halafu nimeitafsiri kwa Kiswahili.

Kwa Kiingereza, kuna hadithi inayosimuliwa juu ya mlevi anayetafuta pesa (au funguo) karibu na taa. Hili ni toleo liliochapishwa katika gazeti ya Boston Herald (mwaka wa 1924): 
[Afisa wa polisi alikutana na mwanamume akipapasa-papasa akipiga magoti] “Nilipoteza noti ya $2 kwenye barabara ya Atlantic,” kasema mwanamume huyo. "Nini kile?" aliuliza afisa aliyeshangaa. "Umepoteza notiya $2 kwenye barabara ya Atlantic? Kwa nini basi unaitafuta hapa Copley Square?" “Kwa sababu,” akasema akiendelea na utafutaji wake, “mwanga ni bora hapa."

Hadithi hii imekuja kujulikana kama "Streetlight effect" katika sayansi.

Asante kwa mshiriki mwenzetu kwa kupendekeza methali hii! Je, una methali ya kupendekeza? Shiriki hapa!
Maelezo Mchoro huu umetengenezwa kwa kutumia Akili Bandia (AI). Unafikiriaje?
Marejeleo
Streetlight Effect (Wikipedia)
A short story (Insha) about the essay in Kiswahili - https://middemb.com/insha-ya-mtaka-cha-mvunguni-sharti-ainame/
Nasreddin (Wikipedia)
History of the Streetlight Principle story on Quote Investigator
1989, Classic Tales of Mulla Nasreddin, Retold by Houman Farzad, Translated from Persian by Diane L. Wilcox, Looking for the Missing Ring, Quote Page 26, Mazda Publishers, Costa Mesa, California. (Verified with scans by Quote Investigator; thanks to Stephen Goranson and Duke University library system) 

1924 May 24, Boston Herald, Whiting’s Column: Tammany Has Learned That This Is No Time for Political Bosses, Quote Page
2, Column 1, Boston, Massachusetts. 
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Huwa tunatendewa kama tunavyowatendea wengine. Kwa kawaida methali hii hutumika kama onyo, au wakati mtu mbaya anapata alichostahili. Lakini pia inaweza kutumika kama tumaini la baraka kwa wale wanaofanya mema. Chimbuko halisi cha methali hiyo haijulikani, lakini ilianza Amerika miaka za 60 hivi. Inaendana na kanuni la Karma katika dini ya Kihindi.

Methali na nukuu zinazohusiana:
Shakespeare
Bado tunayo hukumu hapa (duniani);
Tunafundisha tu umwagaji damu, ambayo, ukifundishwa, hurudi
ili lipiza kisasi na kumtesa mvumbuzi: mkono wa haki
huweka viungo vya kikombe chetu cha sumu
Kwa midomo yetu wenyewe.  ( Makbeth Act I, Scene 7 )
Biblia:
Chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna ( Wagalatia 6:7 )
Kichina: 
善有善報,惡有惡報
Wema hulipwa kwa wema, na ubaya kwa ubaya. 
Kijerumani:
Wie man in den Wald hineinruft, so schallt es heraus
Unacholia msituni, kitasikika tena
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
na Rose Mwanri 🇹🇿 
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥈 Mshindi wa Pili 

Akiba Haiozi

Methali ni usemi wa kimafumbo unaotumika katika jamii. Maneno katika methali huwa na maana ya ziada na methali huwa na pande mbili. Upande wa kwanza hutoa wazo na upande wa pili humalizia wazo. Akiba haiozi ni miongoni mwa methali za kiswahili inayotumika sana katika jamii za kiafrika na kwa watumiaji wa lugha ya kiswahili duniani, ikiwa na lengo la kuwaasa watu juu ya umuhimu wa kujiwekea akiba.

 Dhima ya methali hii ni kutusisitiza sisi wanajamii kujianda vema na maisha ya leo pamoja na kesho huku tukiwa tayari kuzikabili changamoto mbalimbali za maisha.

 Methali hii hutuonyesha ni kawaida mwanadamu kupatwa na dharura mbalimbali katika maisha ya kila siku. Mfano kupatwa na maradhi, ajali, au hata kifo. Pale unapokuwa na akiba uliyojiwekea itakusaidia wakati umepatwa na changamoto ya ghafla ambayo hukuitarajia.

 Faida nyingine ya kuweka akiba ni kuboresha maisha. Cha kwanza nashauri tuwe na utaratibu wa kuweka akiba mara kwa mara ili kuweza kuboresha maisha yetu kwa ujumla. Tunavyozidi kuweka akiba ndivyo ambavyo akiba hiyo inaweza kutusaidia kuboresha makazi yetu na miundombinu kwa ujumla ndani ya jamii zetu. Mfano mzuri ni wazazi ambao akiba wanazoziweka huwasaidia kulipa karo za shule pamoja na kununua vifa mbalimbali vya shulena hata gharama zingine zinazojitokeza kwa wakati huo.

 Methali hii pia inatukumbusha kuwa kadri tunavyozidi kuweka akiba ndivyo tunavyokuza hazina yetu. Swa na ile methali inayosema “ Haba na haba hujaza kibaba” ukichambua methali hizi zinaendana maana na utagundua ni ukumbusho mkubwa kwetu kuhusu ujenzi wa hatma njema ya jamii yetu ya sasa na baadae. Kwa kuwa zinatuhimiza kuwekeza kwa kila chumo tulipatalo. Tunakuza hazina kwa kuwa kile tunachoweka akiba kipo kwaajili yetu.

 Chukua nafasi kujiuliza, ni mara ngapi umepatwa na changamoto na akiba ndiyo ikaokoa jahazi, ni mambo mangapi yametokea bila taarifa na akiba ndiyo imetumika kuweka mambo sawa. Naamini sote tunapaswa kuweka akiba bila kujali kipato ni kikubwa au kidogo. Mfano unaweza kuanza kuweka akiba kidogo kidogo kutokana na kile unachokipata na kufikia muda Fulani utakuwa na akiba kubwa.

 Vilevile methali hii inasaidia kukuza maarifa kwa mtu mmoja mmoja na jamii hasa pale ambapo pamekuwepo na tofauti ya uhifadhi wa akiba kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Hapo zamani tunaambiwa watu walikuwa wanahifadhi akiba zao kwa kuchimba chini ya ardhi, kuweka chini ya kitanda au hata sehemu zingine ambazo wao waliamini ni salama. Leo hii watu hawatumii sana njia za kienyeji kuweka akiba zao. Ukija kwenye fedha zipo benki zenye mifumo thabiti na salama katika kuhifadhi fedha. Kwa upande wa akiba ya mazao pia zipo njia salama za kuhifadhi tena hata kwa muda mrefu bila kuharibika. Kwa hakika akiba haiozi.

 Waswahili tunasema “akiba haiozi”, “haba na haba hujaza kibaba” ikimaanisha kwamba akiba yaweza kuonekana ndogo ila kadri inavyoongezeka ndivyo inavyokuwa kubwa. Kinyume chake tunaambiwa “Chovya chovya humaliza buyu la asali”, “Bandu bandu humaliza gogo”. Tukikumbushwa kuwa vile tunavyochukua akiba zetu kidogo kidogo bila sababu ya msingi ndivyo ambavyo iko siku tutahamaki na kuona akiba imeisha bila kuona kitu cha maana kilichofanyika. Tukumbuke “mali bila daftari huisha bila habari”, tuangalie mfano wa shairi hili linalotusisitiza kuhusu kuweka akiba.

Akiba kweli hazina, haijawahi saliti,
Kwetu ni muhimu sana, hutubeba kwa nyakati,
Kipindi kweli hatuna, inasimama kwa dhati,
Sote tuweke akiba, akiba ni mkombozi.

 Kwa hakika ni dhahiri yatupasa kutunza vitu vyetu vizuri na rasilimali tulizonazo kwa kuweka akiba ili tuweze kujinusuru pale ambapo tunapokumbwa na changamoto za kushtukiza kwa ajili ya maisha yetu ya sasa na ya baadae.

...
That which draws our attention, gets more attention. 

A wheel that makes noise is more likely to receive oil than other wheels (that also might need oil). We have limited attention, and thus we give our attention to people, projects and problems that stand out. This proverb asserts that there is not necessarily a correlation between the things we give our attention to and the things that actually need our attention.

Another version of the proverb is "the squeaky wheel gets the grease," and though the origin is unknown, American humorist Josh Billings is commonly attributed through his poem "The Kicker" in 1870
I hate to be a kicker,

I always long for peace,

But the wheel that squeaks the loudest,

Is the one that gets the grease.
 
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by
Large tasks in life need to tackled in small steps, day by day. This proverb comes from Swahili:
Haba na haba hujaza kibaba
Little by little fills up the jar

Can you think of other similar proverbs that encourage the same way of thinking? 

This saying reminds be of a poem called "Little Things" by Julia Abigail Fletcher Carney:
Little drops of water,
Little grains of sand,
Make the mighty ocean
And the pleasant land.
     
Thus the little minutes,
Humble though they be,
Make the mighty ages
Of eternity. 
Julia Carney composed this poem in 1845 as a student in class -- and she was given only 10 minutes to write it!
...
Iliharirishwa miezi 4 iliyopita
by