You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Fungua akaunti mpya

Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Taarifa
Majadiliano
Methali

A rising tide lifts all boats

Ili kupiga KURA kwa Methali ya Mwezi
Kura
1
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Widespread economic prosperity typically reaches all citizens of a country or region. A country cannot benefit without all of its citizens somehow benefitting, in the same way that an incoming tide will lift all boats including both the behemoth cruise ships and the tiny canoes.

Occasionally, the adage also may be used when referring to entire groups benefitting from a change in circumstances, particularly an influx of resources that seemingly might reach only individuals. I have heard co-workers respond to their co-workers receiving large sales commissions by saying, "a rising tide lifts all boats," implying that the increase in business for the company will expand the total opportunities for the company (and thus all employees). In this use case, clearly it is understood that the "rising tide" does not lift all boats equally.

Critics of this proverb may dispute its veracity claiming the phrase is erroneously used to justify any type of deal or arrangement that seems to benefit the few, but typically the expression is used with optimism or as a form of mild celebration by leaders, or members of the group themselves.

The proverb is often attributed to John F. Kennedy after he used it in a 1963 speech disputing the claim that a dam construction project had too much pork (wasteful spending). Kennedy's speechwriter (Ted Sorensen) revealed that the New England Council originally used the phrase, which Kennedy borrowed regularly.

A similar phrase is "to grow the pie," which means to make the entire set of opportunities greater, presumably so that everyone can appreciate a larger piece of pie, even if their percentage of the pie does not change.

Do you share the sentiment that broad economic prosperity reaches all?
Marejeleo
https://en.wikipedia.org/wiki/A_rising_tide_lifts_all_boats

https://en.wikipedia.org/wiki/Growing_the_pie

A somewhat similar Chinese phrase 水涨船高, which translates to "a thing grows as its foundation grows," has been used for centuries and first appeared in The Gallant Maid (兒女英雄傳), a novel by Wen Kang, a Manchu-born Qing dynasty author.
Loading...
Loading...
Ingia akaunti yako ili kuona na kutoa maoni
Methali hii inatoka Kiingereza "A penny saved is a penny earned." Maana yake, mia inayobaki mfukoni inaweza kutumiwa kwajali ya madhumuni mengine. Mifano: Inaweza kutumika kwaajili ya kununua kitu kingine, unaweza kukopesha au kuwekeza ili kuingiza riba au pesa zaidi katika siku zijazo. Katika uchumi, kanuni hii inaitwa Opportunity Costs (gharama za kukosa fursa). Tunapotumia pesa au muda kwa jambo limoja, tunapoteza pia fursa ya kuzitumia kwajili ya jambo lingine.

Methali hii huhusishwa na Benjamin Franklin, lakini si chimbuko halisi, wala hakuandika msemo huu kamili. Misemo karibu na huu ilichapishwa kabla yake. Kwa mfano: 

A penny spar'd is twice got.
Senti iliyookolewa hupatikana mara mbili.
- Outlandish Proverbs by George Herbert (1640)  
 
Katika Poor Richard's Almanac (1736), Benjamin Franklin alinukuu methali hii na alifafanua vizuri kanuni ya Opportuinty Cost hivi:

Vidokezo kwa Wale Wanaotaka kuwa Matajiri

Matumizi ya pesa ndiyo faida zote zinayopatikana ukiwa na pesa.
Kwa pound [£] sita kwa mwaka [yaani riba] unaweza kutumia  £ mia [yaani kupitia mkopo], kama unajulikana kama mwaminifu na mwenye busara.
Anayetumia groat [senti 4] kwa siku bure, hutumia pound £ zaidi ya sita kwa mwaka, ambazo ni bei ya kujipatia matumizi ya pound £ mia moja.
[Kwa hivyo] Anayepoteza muda wake wa thamani ya groat [senti 4] kwa siku, siku moja na nyingine, anapoteza fursa ya kutumia pound mia moja kila siku.
Anayepoteza muda wa shilingi tano kwa uvivu hupoteza shilingi tano, ni kama amezitupa tu baharini.
Anayepoteza shilingi tano sio tu kwamba anapoteza kiasi hicho, bali anapoteza pia faida yote ambayo ingeweza kupatikana kwa kuzitumia katika shughuli zake, ambayo, akiwa kijana, wakati wa uzee ingefikia kiasi kikubwa cha fedha.
Tena: anayeuza kwa mkopo huongeza bei ya kile anachokiuza kwa kiasi sawa riba angaliingiza na pesa hizo kwa kipindi ambacho atazikosa. Kwa hivyo, anayenunua kwa mkopo hulipa riba kwa kile anachonunua, na anayelipa pesa mara moja kwa kila anachonunua hukoa fursa ya kuzikopesha kwa wengine, kwa hivyo aliye na kitu alichonunua ameshalipa riba kwa matumizi yake.
Hata hivyo nasema kulipa mara moja unaponunua ni bora, kwa sababu anayeuza kwa mkopo anatarajia kupoteza asilimia tano ya mikopo; kwa hivyo anaongeza bei ya kile anachokiuza kwa asilimia ileile ili kuzuia hasara. Wanaolipa kwa mikopo hulipa kodi mara moja. Anayelipa kwa pesa mara moja anaweza kuzuia kodi hii
"Senti iliyohifadhiwa ni senti mbili hakika;
[haba] kwa siku ni [nne] kwa mwaka."
 
Basi, unapofikiria kutumia muda au pesa zako katika jamblo fulani, jiulize, ningekosa, ningepata fursa zipi? Pesa hizi zingeweza kutumikia vipi? Mifano: kumkopesha mwingine, kurudisha madeni uliyonayo, kubuni kitu kipya au kuwekeza katika kitu ambacho kinaweza kuleta faida kubwa mbeleni.
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Kwa kiingereza tunasema "One man's trash is another man's treasure," maana yake, kilichotupwa na mtu mmoja, kinaweza kutumikia mwingine na kuwa na thamani kwake.

Msemo huu hutumika ili kueleza jinsi mapendeleo ya watu hutofautiana, ama kuonyesha matumaini kwamba wanadamu ni wabunifu katika masuala ya kupanga upya au kuchakata vitu vilivyotupwa na wengine.

Kwa mfano, mjasiriamali Gibson Kiwago, mwanzilishi wa WAGA Tanzania, anachakata betri za laptop ili kuleta umeme kwa nyumba na maduka. Jifunze zaidi kuhusu E-Waste (Orodha ya Kusoma)!

Dhana kwamba thamani ya kitu hutegemea mtazamo wako ipo tangu zamani. Chimbuko cha msemo huu ni methali ya Kiingereza iliyotumika karne ya 17:
One man's meat is another man's poison
Nyama na mtu mmoja ni sumu ya mtu mwengine

Je umewahi kuona thamani katika kitu kilichotupwa na mwengine?
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Methali hii inahusiana na tabia ya kufikiria kwamba watu wengine wana vitu vizuri zaidi, hali nzuri zaidi nk... Kwa mfano kufikiri jirani yako ana majani mazuri kuliko wewe.

Chanzo cha methali hii ni "Sanaa ya Upendo" na Ovid, kitabu cha mashairi yaliyotungwa ili kutoa shauri kwa wanaume na wanawake kuhusu kutafuta na kudumisha mahusiano ya kimapenzi. Kitabu hiki kiliandikwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita, takribani 2 KK:
Watu hutaka furaha mpya. Huwa tunaona kuwa watu wengine wana bahati zaidi kuliko sisi wenyewe. Mazao daima ni bora katika shamba la jirani yetu; ng'ombe wake hutoa maziwa zaidi. 
 - Ovid Ars Amatoria (Sanaa ya Upendo), Ukurasa wa 24

Kwa upande mmoja, methali hii inamaanisha, bora kushika kile ulicho nacho, na kupuuza kile ambacho wengine wanacho, hata kama inaonekana ni bora zaidi. Lakini pia kwa mtazamo mwengine, inamaanisha bora kutumia akili yako katika kuboresha hali yako mwenyewe (kama kumwagilia shamba lako) badala ya kufikiria sana ukweli kwamba shamba lako, au hali kwa ujumla, ni duni. Methali nyingine ni "Majani huonekana ya kijani zaidi pale ambapo yalipomwagiliwa maji." 

Methali zinazofanana kikanuni:
Kihindi: 
दूर के ढोल सुहावने लगते हैं
Ngoma za mbali husikika vizuri
Kichina: 
隔籬飯香 
Wali wa jirani hunukia vizuri
Kijapani:
隣の芝生は青く見える
Majani ya jirani huonekana kijana zaidi
Kurusi:
соседняя очередь всегда движется быстрее
Foleni nyingine husogea kwa kasi zaidi
...
Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by
Habari zenu wapenzi wa lugha na hekima! Karibuni tena katika kipindi chetu cha leo cha Methali! Methali ya leo ni “Mtoto akilia wembe, mpe.” Je, unaijua? Kwa walezi wengi, inaweza kuonewa… kali sana, au sivyo? Ina maana gani kwako? Je, unakubaliana nayo? Tushirikiane mawazo. 

Nikisikia nitasahau, nikiona nitakumbuka, nikifanya nitaelewa.
-Mwalimu Amos 

Mtoto akitaka wembe, basi mpe ili aelewe kwanini alionywa dhidi ya kucheza nao. Methali hii inaonyesha umuhimu wa kuwapa watu nafasi za kujifunza kutokana na uzoefu wao wenyewe, hata kama wanaweza kuumiwa (kidogo). Vilevile, hata ukikataa kumpa, labda hatatiii na atacheza nao ukiwa nje. Methali hii inaweza kutumika pia kama onyo kwa mtu anayepuuza ushauri au kusisitiza njia yake. Ingawa ni muhimu kusikiliza ushauri na maonyo kutoka kwa wengine, wakati mwingine tunahitaji kuona matokeo ya vitendo vyetu wenyewe ili kuelewa madhara yake. 

Adhabu ya Asili  (Natural Consequences)

Katika eneo la malezi, methali hii inafundisha kanuni ya Natural Consequences (Adhabu Halisi au Adhabu ya Asili). Adhabu ya asili ni matokeo yatakayokuja kwa sababu ya tabia ya mtoto mwenyewe. Tofauti na adhabu ya kutolewa au adhabu ya viboko, adhabu ya asili hujitokeza bila mlezi kujiingilia. Kwa mfano, fikiria kama mwanako amesahau daftari yake nyumbani. Ungefanyaje? Wazazi wengine wanajibu “Singefanya chochote, maana atahitaji kueleza kwa mwalimu wake.” Wengine wanasema “Ningekimbia shuleni ili kumletea daftari, halafu jioni ningempa adhabu.” Ipi bora?  Jibuni hapo chini… 

Swali: Je, mtoto akilia nyoka utampa?

Sawa tumekubaliana mtoto akilia wembe, mpe. Lakini… fikiria kama mtoto analia kitu cha hatari zaidi— je utakubali? Yesu aliwauliza wazazi: “Mtoto akiomba samaki, je, atampa nyoka?” Akilia nyoka, utampa? Wembe unaweza kusababisha jeraha ndogo, lakini si hatari sana kama nyoka mwenye sumu. 
Wewe kama mzazi, utakubali kiasi gani cha hatari ili ajifunze mwenyewe? Kama anaomba kuacha masomo ili kucheza michezo za simu sikuzote? Kama anaomba kumwoa/kumwolewa na mtu ambaye haumwamini katika umri mdogo? Yaani pia kuna maamuzi muhimu ambayo watoto hawako tayari kujifanyia. 
Je wewe kama mzazi unawezaje kuamua au kutambua kama unapaswa kumwokoa / kumlinda mwanako, ama kama unapaswa kumwachia afunzwe na ulimwengu? Wazazi na walezi wote tunaomba maoni yenu!

Nyoka ana madhara.
-Mwalimu Shila  

Utekelezaji wa methali hii katika maisha ya kila siku

Elimu: Watu hukumbuka walichojifunza kwa vitendo kuliko walichoambiwa kwa maneno. Utafute nafasi za kutekeleza kile unachojifunza.
Malezi: Mpe mtoto uhuru na nafasi za kujifunza kupitia uzoefu. Usimtatulie kila jambo, na usiogope anapofeli, kama hakuna hatari wala madhara ya muda mrefu, maana kufeli ni nafasi ya kujifunza kwake.
Kusikiliza: Ukipuuza maonyo na shauri, usishangaye kuona madhara yaliyotabiriwa.
...

Picha hii imetengenezwa na akili bandia (AI)

Iliharirishwa miezi 5 iliyopita
by