You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Success has many fathers, failure is an orphan

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 4mo ago
by
View this proverb in Swahili
Ushindi una baba wengi ila kushindwa ni yatima
When a project is successful, people want to be associated with it and claim credit, even if their contribution was small. But when things go wrong, people tend to point fingers and downplay their involvement.

For example, suppose you take money from investors to start a business. If the business makes a lot of money, your investors might try to claim your success as their own, calling it "our business", and you will find it easy to raise money from many more investors. But if the business is a failure, your investors will probably call it "your business" and ask you to return their money.

You can often tell who is the real leader of a business, organization or group by observing who takes responsibility when things go poorly. A great leader shares the credit with others when the group has success, and takes the blame when the group fails.

This proverb is often incorrectly attributed to John F. Kennedy, who used it at a press conference after the Bay of Pigs. In fact, it seems to originate from the ancient Roman Historian, Tacitus, in his biography of Agricola, explaining the challenges that the Roman army faced in conquering Britain.
The credit of success is claimed by all, while a disaster is attributed to one alone.
- Tacitus, in Agricola

Do you have an example of this proverb? Share it!
Sources
John F. Kennedy - Transcript of Press Conference, April 21, 1961
JFK never claimed to be the originator of this proverb and preceded it with "There's an old saying..."
He did popularize the phrase, as you can see from this Ngram chart from Google books, which shows the explosion in usage of the phrase after 1961.

Tacitus

Daily Stoic (from email archives):
It is precisely when things are good that we should be considering the possibility that someday they might not be so good. We should be acquiring allies. We should be doing favors and good for other people—because someday, we’ll need them to do the same for us. 

Portions of the Image were made using AI, CC BY
Loading...
Loading...
Login to view and post comments

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Updated 4mo ago
by
Kila kazi kubwa katika maisha huhitaji kufanyika kwa hatua ndogo, siku baada ya siku. 

Je, unajua methali zingine zinazofanana na hii au zinazotoa dhana hiyohiyo? 

Msemo huu unakumbusha shairi liitwalo "Vitu Vidogo" na Julia Abigail Fletcher Carney: 
Matone madogo ya maji,
Chembe kidogo za mchanga, 
hutengeneza bahari kubwa
Na ardhi ya kupendeza

Vivyo hivyo zile dakika ndogo,
ingawa ni ndogo,
hutengeneza enzi za milele. 
Julia Carney alitunga shairi hili mwaka wa 1845 darasani akiwa mwanafunzi darasani -- na alipewa dakika 10 tu kuliandika!
...
Updated 4mo ago
by
Hapo zamani za kale, palikuwa na binti mrembo, mkarimu, mwenye akili aliyeitwa Poshia. Wanaume wengi walitaka kumuoa na walikuja ili kuomba uchumba. Baba Poshia alikuwa amefariki dunia. Alikuwa tajiri na aliacha wosia ulioelekeza kamba yeyote aliyetaka kumuoa Poshia, lazima achague kati ya masanduku tatu: sanduku la dhahabu, sanduku la fedha na sanduku la risasi. Atakayechagua sahihi ndiye atakayeruhusiwa kumuoa Poshiia na kurithi mali zote za Baba Poshia. Siku moja, Mfalme wa Moroko alikuja ili kuomba uchumba.

Mabepari wa Venisi

Tazama ▶️ YouTube


POSHIA: Kayavute mapazia masanduku yaonekane kwake mtukufu huyu mtoto wa mfalme. Haya sasa kachague.

MOROKO: La kwanza, ni la dhahabu, lenye maandiko haya:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
Na la pili, ni la fedha, linaloahidi hivi: 
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
La, tatu, risasi butu, na onyo lake ni butu:
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
Nitajuaje yakuwa nimechagua vizuri?

POSHIA: Moja lina picha yangu, mzawa wa mfalme: Ukilichagua hilo basi na mimi ni wako.

MOROKO: Muungu Fulani uniongoze. Hebu nione; nitayachagua tena maandiko toka mwisho. Nitaanzia la tatu: lasemaje, la risasi?
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
Itambidi atoe - atoleeni? Risasi? Na pia ahatarishe - kwa ajili ya risasi? Sanduku hili latisha: wahatarishao vyote hutumaini kupata faida iliyo nzuri: Wenye moyo wa dhahabu hawajali takataka; Kwa hiyo basi sitoi na wala sihatarishi chochote nilicho nacho kwa sababu ya risasi. La fedha lasema nini, lenye rangi ya baridi?
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
Apate astahilicho! Subiri hapa, Moroko. Upime thamani yako kwa mkono wa mwadilifu: Kama ukithaminiwa vile ujifanidivyo wastahili kutosha; walakini ya kutosha inaweza isitoshe kumpata siti huyu. Bali nikitia shaka kuwa simstahili,Basi hapo nitakuwa najiumbua mwenyewe. Stahili yangu ni nini? Bila shaka ni bibie. Namstahili, hakika, kwa nasaba na kwa mali, kwa madaha na kwa sifa zote za malezi mema na kuzidi yote hayo namstahili kwa pendo. Vipi, nisiendelee, nichague papa hapa?
Hebu tuyaone tena ya sanduku la dhahabu:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Naam, ni siti huyu; anotamaniwa kote. Toka pande zote nne za dunia wanakuja kubusu sanamu hii takatifu ilo hai: Majangwa ya Hirikani na nyika pana ajabu, za Uarabuni kote, sasa zimekuwa njia ziletazo watawala kumwona Poshia bora. Nayo dola ya bahari ambayo inapofura hutemea hata mbingu, haiwezi kuzuia nia ya wageni hao; ila wanazidi kuja, kama wavuka kijito, kumwona Poshia bora. Moja la matatu haya lina picha yake nzuri. Itawezekana kweli liwe lile la risasi? Wazo chafu kama hilo lingekuwa ni laana. Halifai japo kuwa sanda yake ya kaburini.
Au niwaze ya kuwa kawekwa ndani ya fedha? Moja ya kumi na moja ya thamani ya dhahabu? Hilo ni wazo la dhambi! Kito cha thamani hivi hakiwekeki po pote ila ndani ya dhahabu. Uingereza wanayo sarafu tu ya dhahabu, ambayo kwa juu yake imechapwa malaika. Bali hapa malaika mwenyewe hasa yu ndani ya sanduku hili hapa, na bahati nijaliwe!

POSHIA: Ni huu hapa, chukua, mzawa wa mfalme; kama sura yangu imo nimekuwa mali yako.

[Anafungua sanduku la dhahabu]
MOROKO: Mama yang! Nini hii? Ni fuu tupu la kichwa, ambalo katika jicho lina hati ma’ndiko. Nitasoma maandiko.
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.
Nimefarikiwa kweli. Bure nimejitanibu. Basi buriani, joto; nawe, makiwa, karibu. Basi kwa heri Poshia. Ninayo
huzuni sana siwezi kwa heri ndefu: Ndivyo wanavyoagana watu waliopoteza.
[Aondoka na Wafuasi wake. Tarumbeta]
...
Updated 4mo ago
by

Ufafanuzi


Methali hii ya Kiingereza inatafsirika pia kama "Kalamu ina nguvu kuliko upanga au jambia" au " Kalamu ni kali kuliko upanga." Katika methali hii, jambia au upanga unaashiria nguvu na ukatili, na maana ya kalamu ni maneno. Ingawa upanga unaweza kushinda kwa nguvu, kalamu inaweza kuwashawishi, kuwahamasisha, na kuwaelimisha watu. Sio kila mtu ana silaha za kuwalazimisha watu wengine kufanya kile anachotaka, lakini kila mtu ana uwezo wa kubadilisha ulimwengu kupitia kile anachofikiria, kusema na kuandika kwa maneno. 

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
 - Methali ya Kiswahili

Methali hii ni kweli kwa sababu mara nyingi maneno huchochea na kudhibiti jinsi watu wanavyotumia nguvu na silaha zao. Kwa mfano, kupitia sheria, maneno ya viongozi, mahakimu na majaji yana uwezo wa kuwafunga watu gerezani au hata kuwaua. Kutoa hotuba ya moto kwa umati wa watu wenye hasira kunaweza kuleta ghasia kali na madhara mengine (ona Juliasi Kaizari).

"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)

Lakini pia, methali hiyo inatukumbusha nguvu ya upinzani usio na vurugu kwenye kuleta mabadiliko ya kudumu, kanuni iliyotetewa na kuonyeshwa na watu kama Mahatma Gandhi, Martin Luther King, na Nelson Mandela.  Angalia pia: Insha ya "Civil Disobedience"  na Henry David Thoreau, pamoja na Tamthilia mashuhuri ya "Antigone" na Sophocles.

Chimbuko


Nukuu hii ya "kalamu ina nguvu kuliko upanga" ilipata umaarufu kupitia tamthilia ya "Richelieu: au The Conspiracy"  na Edward Bulwer-Lytton (mwaka wa 1839, ukurasa wa 47). Lakini hakika wazo lilikuwepo kabla.

Wengine wanasema chimbuko halisi la methali hii ni Hadithi ya Ahikar. Kitabu hiki kiliandikwa takriban miaka 600 kabla ya kristu, na ni chimbuko la methali zingine kama "Ndege mkononi ana thamani ya wawili mtini"). Katika toleo letu, mfasiri hakuweza kusoma maandishi kutokana na hali ya karatasi, na maneno yalikatika. (Ukurasa 171/274
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na  ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa  ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Je, hili ndilo chimbuko halisi la methali hii, miaka zaidi ya 2,500 iliyopita? Muwe majaji...

Chanzo karibu na methali hii pia kinaonekana katika Agano la Kale:
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia

Na vilevile katika Shakespeare: 
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)

 Je, unakubali kalamu hushinda jambia? Toa maoni yako hapo chini!
...

CC BY Unaruhusiwa kunakili & kusambaza mchoro huu na makala hii bila idhini, ukitaja tu chanzo (www.maktaba.org)

Updated 4mo ago
by