You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Haba na haba hujaza kibaba

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 4mo ago
by
View this proverb in English
Little by little fills up the jar
Kila kazi kubwa katika maisha huhitaji kufanyika kwa hatua ndogo, siku baada ya siku. 

Je, unajua methali zingine zinazofanana na hii au zinazotoa dhana hiyohiyo? 

Msemo huu unakumbusha shairi liitwalo "Vitu Vidogo" na Julia Abigail Fletcher Carney: 
Matone madogo ya maji,
Chembe kidogo za mchanga, 
hutengeneza bahari kubwa
Na ardhi ya kupendeza

Vivyo hivyo zile dakika ndogo,
ingawa ni ndogo,
hutengeneza enzi za milele. 
Julia Carney alitunga shairi hili mwaka wa 1845 darasani akiwa mwanafunzi darasani -- na alipewa dakika 10 tu kuliandika!
Sources
"Little Things" na Julia Abigail Fletcher Carney
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Siku moja, mfanyabiashara mashuhuri alitafuta msaidizi. Alipokea maombi na CV za watu wengi sana, lakini wawili tu walikidhi vigezo: Amina na Baraka. Ili kuamua kati yao, aliwaita wote wawili, na akawaalika waje kwaajili ya mahojiano ya ajira, kesho yake asubuhi. "Saa tatu kamili -- vaa mavazi ya kazi, na usichelewe!" Akawaonya.

Kesho yake Ali aliwahi kuamka, akavaa suti yake nzuri, na alipanda basi kijijini kwake saa 2. "Bora kinga kuliko tiba" alifikiria. Njiani kuelekea mjini, basi ilianza kutoa moshi. Abira wote walishuka na waliachwa porini. Hapo hapo mvua ilianza kunyesha. Kila basi lililompita, Ali akaomba nafasi, lakini, kutokana na hali ya hewa, mabasi yote yalikuwa yameshajaa. Kwa hivyo ikabidi atembee kwa miguu. Ilipotimia saa tatu, bado Ali alikuwa mbali na mji, na mvua ikawa kali zaidi na zaidi. "Lazima niendelee" akajiambia, "Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa."

Wakati huohuo mjini, Baraka aliamka ghorofani kwake, na akashtuka ghafla akiona jua lilikuwa limeshafika mbali angani. "Aisee! Niliweka alarm! Simu yangu ina shida gani sasa?" Alitazama saa ukutani: Saa tatu kamili. "Bora niache tu. Hata nikiondoka saivi, bado nitachelewa kufika. Si alisema usichelewe? Hatamwajiri aliyechelewa." Kwa hivyo Baraka, akiwa na huzuni, akalala tena.

Saa nne na nusu, hatimaye, Ali alifika ofisini kwa mfanyabiashara na kugonga mlango, suti yake ikichuruzika maji na matope sakafuni. Mfanyabiashara akajibu. "Si nilikwambia vaa mavazi yanayofaa na usichelewe? Sasa umechelewa zaidi ya saa limoja na mavazi yako yamechafuka. Niambie nitawezaje kukuajiri baada ya hapo?" Kisha Ali akaeleza yote yaliyomtokea. Mfanyabishara akamjibu "Nimejifunza mengi kuhusu wewe kutoka kwa hadithi yako Ali. Ukiwa na kusudi kichwani, utafanya kazi kwa bidii, na pale unapokutana na vikwazo hukati tamaa, hata kama umechelewa. Nakwambia, wewe ndiye wa kwanza kufika leo. Mwingine alikosa kabisa. Nitakuajiri wewe."

Mafanikio makubwa huanza na makosa mengi, lakini baada ya muda, uvumilivu na ustahilimilu huleta matunda. Kukosa ni uanadamu, lakini Mungu ni mvumilivu sana kwetu. Anatupa nafasi nyingi za kujifunza na kujaribu tena, ilimradi tusikate tamaa.

Wengine wanasema methali ya "Better late than never never" inatoka kwa kitabu cha The Canterbury Tales, kilichoandikwa na Chaucer miaka ya 1390.
Better than never is late
“Bora kuliko kamwe ni kuchelewa
-The Canterbury Tales, The Canon's Yeoman's Tale
Wengine wanasema chimbuko la kweli ni kitabu cha Historia ya Roma, kilichoandikwa na Livy takriban mwaka wa 20 KK.
Lilatini: potiusque sero quam numquam
Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa
- History of Rome, Book 4

Methali ya Kiingereza inayoendana ni:
It's never too late
Hakuna kuchelewa
 Methali ya Kiingereza inayopinga:
Don't close the gate after the horse has bolted.
Usifunge mlango baada ya farasi kukimbia

Methali ya Kihindi: 
जब जाति तब सवेरे
Wakati wowote unapoamka, ndo asubuhi yako

...

Fikiria kama umechelewa Mahojiano ya Ajira. Ungefanyaje? Next time unapofikiri "Nimeshachelewa" jiambie "Bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa." Kwa mfano makala hii ya Methali ya Siku ilichelewa, lakini sasa unaisoma - Asante!

Updated 4mo ago
by
"na Ibrahim Nyanda
🏆 Shindano la Insha ya Methali
“Ni kwa nini kijiji chetu hakina maendeleo ukilinganisha na vijiji vingine vinavyotuzunguka? Vijana wengi kutoka vijiji vingine wa umri wetu wamesoma na wengine wana kazi zao za maana huko mjini. Pamoja na kwamba kuna shule kijijini kwetu lakini vijana hatufanyi vizuri shuleni na hata walimu wanapoajiriwa hawakai muda mrefu wanahama. Kuna nini hapa Bombambili?" Haya ni maswali ambayo kijana Akilimali alimwuliza rafiki yake Manase wakiwa machungani wakilisha ng’ombe. 

Mara baada ya swali hili Manase alionekana amezama katika wimbi kubwa la mawazo na mara baada ya kufikiri kwa muda alimgeukia rafiki yake Akilimali na kumtazama kwa kina kiaha akamwuliza, “Unaamini kuhusu ushirikina” Akilimali alijibu kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubaliana na swali aliloulizwa na kisha akasema “Naamini kwani mara kadhaa nimekua nikiona watu wakienda kwa waganga na wengine wanapopitia magumu huamini wamerogwa, si unakumbuka juzi bibi Andunje tulivyoambiwa kuwa amekutwa juu ya paa la mzee Masanja uchi wa mnyama akiwanga, sasa mpaka hapo naachaje kuamini mshikaji wangu” 

Manase alimwangalia Akilimali kwa makini kisha akamwambia, "Nataka nikueleze siri moja ambayo huwezi amini……. hivi unajua kama mama yako na dada yako ni wachawi?” Akilimali alibaki ameduwaa mithili ya mjusi aloyebanwa na mlango halafu akiwa amefura kwa hasira akamwambia Manase “Aisee mwanangu usianze kuniletea habari zako za udwanzi hapa, tena koma kabisa kumwambia mama yangu mchawi vinginevyo ntakuja kukufanyia kitu mbaya hutokuja kuamini macho yako, ohoooo!!” 

Manase alimtuliza rafiki ake Akilimali halafu akamwambia, “Ngoja niwarudishe ng’ombe jirani afu nikupe mchapo mzima ulivyo, najua utanielewa we punguza jaziba kwanza” 

Mara baada ya kurudisha mifugo jirani Manase akaanza kumweleza Akilimali, “Rafiki angu nataka nikupe siri hii ambayo nimekaa nayo kwa muda mrefu, chochote unachokiona hapa hata kutokuwepo kwa naendeleo kijijini ni kwa sababu ya ushirikina, kila siku mama yako na dada yako huwa ninawaona wakija nyumbani wamepanda fisi wakimpitia mama kwenda kuwanga…..” Manase alitulia kidogo halafu akaendelea 

“Huwezi kuamini kwani hata mimj nilikua siamini mpaka nilipopakwa dawa na kuwaona, nitakupa hiyo dawa utapaka machoni na utakuja kunipa majibu kesho.” 

Mara baada ya mlo wa usiku Akilimali alikua ameketi akiota moto nje ya nyumba yao ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi wakati huo mama yake na dada yake wakiwa ndani na yeye akiwa na baba yake pale nje. Alipaka ile dawa kama alivyoelekezwa na baada ya dakika kumi alimwona dada yake na mama yake wamepanda juu ya fisi mithili ya pikipiki tayari kwa safari ya kwenda kuwanga. 

“Nisamehe sana rafiki angu, ilikua ni hasira tu” aliongea maneno haya Akilimali huku akilengwa na machozi, 

“Mimi nilijua, sasa unavyoona kijijj chetu hakiendelei hata mama yako pia na dada yako wanahusika, inaumiza sana kila mwanakijiji anayetaka kuleta maendeleo anaishia kufa, lazima kuna siku watakuja kuumbuka kama ilivyokua kwa bibi Andunje” 

“Nina uhakika hata baba yako hajui kama mama yako na dada yako ni wachawi na kila siku huwa wanaenda kuwanga na ninyi kuwaachia mauzauza mkijua wapo, nenda kampake baba yako hiyo dawa alafu utanipa majibu” alieleza Manase 

Jioni kwa siri Akilimali alimweleza baba yake kuwa dada yake na mama yake ni wachawi kitu ambacho alipinga vikali. 

“Mama leo baba anatuona, angalia anvyotutumbulia macho” dada yake na Akilimali alimwabia mama yake wakiwa juu ya fisi kama ilivyo ada wakati baba yake na kaka yake wakiwa nje wanaota moto kama ilivyo kawaida yao. 

“Sidhani kama anatuona, hebu geuza fisi tuwe kama tunawaelekea wao” ailisema mana yake na Akilimali.

Akilimali anasema hiyo ndiyo ilikua siku ya mwisho kumwona baba yake kwani baada ya kuona fisi aliyewabeba mke wake na binti yake alitimua mbio kama anashundana mashindano ya mbio za mita mia. Ama kweli usilolijua ni kama usiku wa giza, Akilimali alibaki haamini kama kwa muda wote huo ameishi na mama yake na dada yake bila kujua kuwa ni wachawi. 
...

Meaning 


In this proverb, the sword signifies force and violence, and the pen stands for words. While the sword can conquer with force, the pen can persuade, inspire, enlighten and motivate people. Not everyone has weapons to force other people to do what they want, but everyone has the power to influence the world through what they think, say and write with words.

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
Today's weapons are pen and paper.
 - Swahili proverb

Part of the reason this proverb is true is that words often motivate and regulate how people use violence and force. For example, through law, the words of leaders, judges and juries have the power to jail people or even kill them. Making a fiery speech to an angry mob might cause a violent riot (see Julius Caesar). 

You furnish the pictures and I'll furnish the war.
- William Randolph Hearst

The proverb also reminds us of the power of nonviolent resistance to bring about lasting political change, a principle advocated and demonstrated by figures like Mahatma Gandhi, Martin Luther King, and Nelson Mandela. (Check out Henry David Thoreau's classic Essay, "Civil Disobedience" and Sophocles famous play, "Antigone")

Origin


The phrase "the pen is mightier than the sword" became popular after Edward Bulwer-Lytton used it in his 1839 play "Richelieu: Or the Conspiracy" (page 47).  But the idea likely originated much earlier.

Some sources attribute the proverb to the Story of Ahikar (which is also the source of the proverb "A bird in the hand is worth two in the bush"). In this edition, the translator was unable to decipher the damaged manuscript and left the sentence unfinished. (Page 171/274
(FRAGMENTS)
Watch carefully over thy mouth ...... and make thy heart slow(?), for the word spoken is like a bird, and he who utters it is like a man without ...
... the craft of the mouth is mightier than the craft of ...... 
Could this be the original source of the proverb from over 2500 years ago? You be the judge...

A similar phrase also appears in the Old Testament: 
For the word of God is quick, and powerful, and sharper than any two-edged sword.
Hebrews 4:12 (KJV)

And in Shakespeare:
 Many wearing rapiers are afraid of goosequills.
-William Shakespeare Hamlet Act 2, scene II (page 59)

Do you agree that the pen is mightier than the sword? Share your opinions below!

...
Updated 4mo ago
by
Kuna vitu ambavyo huwezi kufanya peke yako. Tango ni mchezo (densi) ya watu wawili, kwa hivyo huwezi kucheza tango peke yako.

Methali hii inatoka wimbo ulioimbwa 1952, It Takes Two to Tango:
Unaweza kusafiri kwa meli peke yako,
kulala au kupumzika peke yako.
Unaweza kuingia kwenye deni peke yako.
Kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya peke yako.
Lakini ni lazima muwe wawili ili kucheza tango, muwe wawili ili kucheza tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning na Pearl Bailey) Ona vyanzo/sources ili kusikiliza wimbo huu!

Methali hii ina maana nyingi tofauti ambazo unaweza kutekeleza katika mahusiano na maisha yako ya kila siku. Mambo mengi huhitaji watu zaidi ya mmoja: Wawili wanatakiwa ili kushirikiana, kufanya biashara ama kupigana. Ukitaka kucheza na mtu ambaye hataki kucheza na wewe, bora kumtafuta mchezaji mwengine.. Vivyo hivyo, ukiwa kwenye mgogoro au magomvi, itabidi ufikirie jinsi tabia yako inavyoweza kuchangia katika kuendeleza shida. katika dance, lengo si kuwa mkamilifu, bali ni kuendana na mwenzako na kufurahia pamoja.
Methali zinazofanana kutoka Afrika: 
Kimisri (Kiarabu): 
ايد لوحدها ماتسقفش‎
Mkono mmoja hauwezi kupiga makofi
Kiswahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Kidole kimoja hakiuwi chawa
...
Updated 4mo ago
by