You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Lazima muwe wawili ili kucheza tango

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 4mo ago
by
View this proverb in English
It takes two to tango
Kuna vitu ambavyo huwezi kufanya peke yako. Tango ni mchezo (densi) ya watu wawili, kwa hivyo huwezi kucheza tango peke yako.

Methali hii inatoka wimbo ulioimbwa 1952, It Takes Two to Tango:
Unaweza kusafiri kwa meli peke yako,
kulala au kupumzika peke yako.
Unaweza kuingia kwenye deni peke yako.
Kuna mambo mengi ambayo unaweza kufanya peke yako.
Lakini ni lazima muwe wawili ili kucheza tango, muwe wawili ili kucheza tango...
- It Takes Two to Tango (1952, Al Hoffman, Dick Manning na Pearl Bailey) Ona vyanzo/sources ili kusikiliza wimbo huu!

Methali hii ina maana nyingi tofauti ambazo unaweza kutekeleza katika mahusiano na maisha yako ya kila siku. Mambo mengi huhitaji watu zaidi ya mmoja: Wawili wanatakiwa ili kushirikiana, kufanya biashara ama kupigana. Ukitaka kucheza na mtu ambaye hataki kucheza na wewe, bora kumtafuta mchezaji mwengine.. Vivyo hivyo, ukiwa kwenye mgogoro au magomvi, itabidi ufikirie jinsi tabia yako inavyoweza kuchangia katika kuendeleza shida. katika dance, lengo si kuwa mkamilifu, bali ni kuendana na mwenzako na kufurahia pamoja.
Methali zinazofanana kutoka Afrika: 
Kimisri (Kiarabu): 
ايد لوحدها ماتسقفش‎
Mkono mmoja hauwezi kupiga makofi
Kiswahili:
Bila mtu wa pili ugomvi hauanzi
Kidole kimoja hakiuwi chawa
Sources
It Takes Two to Tango (song)
1952 recording by Pearl Bailey : YouTube Video
(Wikipedia) by Al Hoffman and Dick Manning

It takes two to tango (proverb) on Wikipedia

Image source:  "El Tango" by Pedro Figari, 1930s, public domain (Wikimedia)
Tango (dance) (UNESCO) (Wikipedia)
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Have you ever noticed that time seems to pass more slowly when you are waiting for something? On the other hand, if you distract yourself with other engaging activities, time goes by quickly.

For example, if you're in a waiting room for a doctor, the wait will seem shorter if you check your phone or read a magazine, rather than just waiting for your name being called.

This proverb was attributed by Benjamin Franklin to Poor Richard's Almanac, however it doesn't actually appear there. Instead, Franklin used it in an essay on animal magnetism in 1785.

I was very Hungry; it was so late; “a watched pot is slow to boil,” as Poor Richard says.

...
Updated 4mo ago
by
Hapo zamani za kale, palikuwa na binti mrembo, mkarimu, mwenye akili aliyeitwa Poshia. Wanaume wengi walitaka kumuoa na walikuja ili kuomba uchumba. Baba Poshia alikuwa amefariki dunia. Alikuwa tajiri na aliacha wosia ulioelekeza kamba yeyote aliyetaka kumuoa Poshia, lazima achague kati ya masanduku tatu: sanduku la dhahabu, sanduku la fedha na sanduku la risasi. Atakayechagua sahihi ndiye atakayeruhusiwa kumuoa Poshiia na kurithi mali zote za Baba Poshia. Siku moja, Mfalme wa Moroko alikuja ili kuomba uchumba.

Mabepari wa Venisi

Tazama ▶️ YouTube


POSHIA: Kayavute mapazia masanduku yaonekane kwake mtukufu huyu mtoto wa mfalme. Haya sasa kachague.

MOROKO: La kwanza, ni la dhahabu, lenye maandiko haya:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana.’
Na la pili, ni la fedha, linaloahidi hivi: 
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho.’
La, tatu, risasi butu, na onyo lake ni butu:
‘Anichaguaye mimi itambidi atoe, na pia ahatarishe chochote alicho nacho.’
Nitajuaje yakuwa nimechagua vizuri?

POSHIA: Moja lina picha yangu, mzawa wa mfalme: Ukilichagua hilo basi na mimi ni wako.

MOROKO: Muungu Fulani uniongoze. Hebu nione; nitayachagua tena maandiko toka mwisho. Nitaanzia la tatu: lasemaje, la risasi?
‘Anichaguaye mimi itambidid atoe na pia ahatarishe cho chote alicho nacho.’
Itambidi atoe - atoleeni? Risasi? Na pia ahatarishe - kwa ajili ya risasi? Sanduku hili latisha: wahatarishao vyote hutumaini kupata faida iliyo nzuri: Wenye moyo wa dhahabu hawajali takataka; Kwa hiyo basi sitoi na wala sihatarishi chochote nilicho nacho kwa sababu ya risasi. La fedha lasema nini, lenye rangi ya baridi?
‘Anichaguaye mimi apate astahilicho’.
Apate astahilicho! Subiri hapa, Moroko. Upime thamani yako kwa mkono wa mwadilifu: Kama ukithaminiwa vile ujifanidivyo wastahili kutosha; walakini ya kutosha inaweza isitoshe kumpata siti huyu. Bali nikitia shaka kuwa simstahili,Basi hapo nitakuwa najiumbua mwenyewe. Stahili yangu ni nini? Bila shaka ni bibie. Namstahili, hakika, kwa nasaba na kwa mali, kwa madaha na kwa sifa zote za malezi mema na kuzidi yote hayo namstahili kwa pendo. Vipi, nisiendelee, nichague papa hapa?
Hebu tuyaone tena ya sanduku la dhahabu:
‘Anichaguaye mimi atakuwa amepata kile wanaume wengi wakitamanicho sana!’
Naam, ni siti huyu; anotamaniwa kote. Toka pande zote nne za dunia wanakuja kubusu sanamu hii takatifu ilo hai: Majangwa ya Hirikani na nyika pana ajabu, za Uarabuni kote, sasa zimekuwa njia ziletazo watawala kumwona Poshia bora. Nayo dola ya bahari ambayo inapofura hutemea hata mbingu, haiwezi kuzuia nia ya wageni hao; ila wanazidi kuja, kama wavuka kijito, kumwona Poshia bora. Moja la matatu haya lina picha yake nzuri. Itawezekana kweli liwe lile la risasi? Wazo chafu kama hilo lingekuwa ni laana. Halifai japo kuwa sanda yake ya kaburini.
Au niwaze ya kuwa kawekwa ndani ya fedha? Moja ya kumi na moja ya thamani ya dhahabu? Hilo ni wazo la dhambi! Kito cha thamani hivi hakiwekeki po pote ila ndani ya dhahabu. Uingereza wanayo sarafu tu ya dhahabu, ambayo kwa juu yake imechapwa malaika. Bali hapa malaika mwenyewe hasa yu ndani ya sanduku hili hapa, na bahati nijaliwe!

POSHIA: Ni huu hapa, chukua, mzawa wa mfalme; kama sura yangu imo nimekuwa mali yako.

[Anafungua sanduku la dhahabu]
MOROKO: Mama yang! Nini hii? Ni fuu tupu la kichwa, ambalo katika jicho lina hati ma’ndiko. Nitasoma maandiko.
Kila kitu king’aacho usidhani ni dhahabu,
umekisikia hicho ni kiambo cha mababu.
Kuniona kwa nje tu, wengi wameuza utu;
Makaburi ya dhahabu yana mafunza ajabu.
Ungekuwa na werevu ulivyo na ushupavu,
kijana kiwiliwili na mzee kwa akili,
usingelistahili kulipewa jibu hili:
Basi buriani dawa; pposa umefarikiwa.
Nimefarikiwa kweli. Bure nimejitanibu. Basi buriani, joto; nawe, makiwa, karibu. Basi kwa heri Poshia. Ninayo
huzuni sana siwezi kwa heri ndefu: Ndivyo wanavyoagana watu waliopoteza.
[Aondoka na Wafuasi wake. Tarumbeta]
...
Updated 4mo ago
by
Maana yake, afadhali kuridhika na ulicho nacho, badala ya kuiweka hatarini kwa ajili ya kupata kitu kubwa zaidi.

 Methali hii ni ya zamani sana. Chanzo cha methali hii ni kitabu cha kale kiitwacho  "Hadithi ya Ahikar." (Kinajulikana pia kama "Methali za Ahiqar.")
Mwanangu, mguu wa kondoo katika mkono wako mwenyewe ni bora kuliko bega zima katika mkono wa mwengine; Afadhali kondoo mdogo aliye karibu na wee kuliko ng'ombe aliye mbali; Afadhali shomoro aliyeshikwa mkononi kuliko ndege elfu warukao angani; vazi ulilo nalo ni afadhali kuliko vazi la zambarau usiloliona.
- Hadithi ya Ahikar (ukurasa wa 110)
Kitabu hiki kinasimulia hadithi ya mshauri wa wafalme wa kale wa Ashuru na Misri. Inadhaniwa kuwa hadithi hii ilitungwa takribani 600 KK, na kuna nakala iliyochapishwa mwaka wa 500 KK. 

Methali karibu na hii kutoka nchi mbalimbali:
French:
Un tiens vaut mieux que deux tu l'auras
'Shika-hii-hapa" moja ina thamana kuliko 'nitakuletea-baadaye' mbili
Japanese
明日の百より今日の五十
Hamsini leo ni bora kuliko mia kesho
Italian
Meglio un uovo oggi che una gallina domani
Bora yai leo kuliko kuku kesho

Mnaonaje -- methali hii ni ushauri mzuri? Ni bora kuridhika na kitu kinachopatikana kwa hakika, ama kutafuta kitu bora zaidi kisicho na hakika?
...
Updated 4mo ago
by
The winner of a competition or conflict receives the majority or entirety of the rewards, and possibly additional benefits beyond what was being fought over. 

In war, the spoils could refer to land, gained power or other sought after resources. In other pursuits the spoils typically refer to accolades, money or opportunities.

The proverb is typically used to explain unequal outcomes or to remind others that the stakes of many conflicts are winner take all, zero sum, or at the very least, disproportionately favorable to the few winners.

Check out the sources section for a description of the context and information about the US politician who was credited with the phrase (in the 1830s).
...
Updated 4mo ago
by