Publisher Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Serikali ya Tanzania)
Serikali imekuwa ikitoa maelekezo kupitia Sera, Sheria, Miongozo, Kanuni na Taratibu mbalimbali na kuhuisha ile iliyopo kulingana na mahitaji ya wakati huo kwa nia ya kuimarisha utendaji kazi wa Taasisi na watumishi wa Umma. Serikali imeona ipo haja ya kutoa malekezo juu ya uandishi wa nyaraka mbalimbali iii kuongeza umakini na heshima inayobebeka katika mawasiliano ya maandishi. Kutokana na azma ya kuwa na viwango vya pamoja, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeandaa Mwongozo wa Uandishi wa Nyaraka Mbalimbali za Kiserikali.
Mwongozo wa Uandishi wa Nyaraka Mbalimbali za Kiserikali unalenga kuzielekeza Taasisi za Umma mambo yakuzingatiwa katika uandishi wa nyaraka iii kuboresha nyaraka zinazoandaliwa na Taasisi za Umma. Mwongozo huu unatoa maelekezo ya uandishi wa nyaraka za aina tatu (3) ambazo ni barua, dokezo na taarifa.
Ni mategemeo yetu kuwa Mwongozo wa Uandishi wa Nyaraka Mbalimbali za Kiserikali utatumiwa na watumishi katika Taasisi za Umma kujifunza na kujikumbusha misingi ya uandishi wa nyaraka mbalimbali za Serikali iii kuwa na utendaji unaozingatia viwango.
...