You are now browsing in English. Switch to Swahili
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiingereza. Rudi kwa Kiswahili"
You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs
Mchumia juani, hulia kivulini
Join
or login
to VOTE
Votes
60
View this proverb in English
Work in the sun, eat in the shade
na Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Shindano la Insha ya Methali 
🥉 Mshindi wa Tatu
Ni mara ngapi umesikia Mchumia juani hulia kivulini? Hii ni methali ya kiswahili (kibantu) yenye maana ya kuwatia moyo watu katika shughuli mbalimbali wanazozifanya Kila siku wawe na Imani kuwa ipo siku watayafurahia matunda ya kazi yao. 

Methali hii huwapa watu nguvu, bidii, moyo, ujasiri, tumaini na weledi katika kufanya kazi. Mfanyakazi huamini kuwa baada ya kazi ngumu zenye surubu basi huleta mavuno mazuri yenye kumfanya astareheke kivulini akila matunda ya kazi yake. Shairi lifuatalo linaonesha kwa namna gani mchumia juani huwa katika majukumu ya Kila siku.

Siogopi jua wala mvua, nikiitengeneza kesho yangu
Siogopi maumivu Wala majeraha, maana yote ni ya muda
Jua kali na kazi ndiyo desturi yangu, ili kheri kuja maishani
Machinga,mkulima, makuli na mvuvi wao na jua, Ili kuitafuta kesho
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.
Ni mchana jua la utosi, kichwani nina mavuno, jasho linatiririka
Jua limezama Sasa kasia ufukweni, hoi kitandani, nyavu zi baharini
Nyumbani mtaa wa nne, nahodha wa familia surubu nivute  kheri
Jua Sasa la chomoza, Kiguu na njia kulitafuta tonge
Mchumia juani, hulia kivulini bado nakitafuta kivuli.

Bwana mmoja alikuwa mkulima. Maisha yake yote alitumia katika kilimo. Hivyo kupendeza kwake kulikuwa mara chache. Watu kijijini kwake walimuita mkulima stadi. Alijenga nyumba kwa kuuza sehemu ya mazao yake, alisomesha wanae kwa kilimo.

Bwana huyu alikuwa mtu mwenye bidii alijifunza siku zote kanuni za mkulima bora, hivyo kadri muda unavyokwenda mashamba yake alivuna mazao mengi. Watu wengi walistaajabu sana kuona mabadiliko makubwa ndani ya familia yake. Aliwekeza vitu vingi kijijini kwake, mashamba, nyumba, maduka na mifugo mingi vilitoka shambani.

Watu wengi walikuja kujichukulia hekima kwa mkulima stadi. Siku zote aliwaambia "Mchumia juani, hulia kivulini. Jembe limeniheshimisha kijijini Mimi na familia yangu. Maisha yangu sasa yanakwenda barabara kwa hakika niko kivulini nafurahia matunda ya kazi yangu ya juani. Mimi leo kijana wa mkulima huyo stadi najivunia malezi, uwajibikaji wake kwa sababu kazi za juani leo zimetufanya tupumzike na kula kivulini. Kwa hakika maana ya mchumia juani inaonekana kwa vitendo. Bidii yako ndilo jua lako na kivuli ndiyo matunda ya bidii yako.

Hadithi hii inashibishwa na hadithi ilee ya "Mabala the Farmer" yaani Mabala Mkulima iliyoandikwa na Richard S. Mabala(1989). 

Mabala alikuwa mfanyakazi bandarini Kisha akapunguzwa hivyo akachagua kurudi kijijini Morogoro. Mabala alikuwa mzembe,mlevi na mbishi. Mabala alikwenda shambani na galoni ya pombe alikunywa na kulala, alipoamka alimwongelesha mkewe lakni hakujibiwa zaidi ya  sauti ya jembe tik-tok, tik-tok .

Mabala alikuwa mbishi, alimwagilia sukari shambani alifikiri ni mbolea, lakni mwisho alibadilika na kuwa mkulima stadi akawa mchumia juani ili familia yake ije kulia kivulini. Je wewe unahisi Mabala ni mchumia juani? Ndani ya familia au kwenye jamii mkulima stadi anakupa picha gani?

Mwisho hadithi hii kutoka katika methali ya mchumia juani hulia kivulini hutuonyesha dira njema katika kila tunachokifanya katika maisha ya kila siku. Huku methali kama Subira yavuta kheri, Mgaa na Upwa hali wali mkavu zote hufanana kimaudhui, zipo katika kuipa jamii nguvu na matumaini kwa kila jambo lifanyikalo katika malengo.
Sources

Juu ya Insha hii

Insha hii ilishinda nafasi ya tatu 🥉 katika Shindano la Methali ya Insha la Maktaba.org 🏆 7/7/2023
Magreth Lazaro Mafie ni mwanafunzi Mtanzania 🇹🇿 

Hakimiliki

Creative Commons Attribution (CC BY 4.0)
na Magreth Lazaro Mafie
Ilichapishwa na Maktaba.org
Mchoro/Image: CC BY Maktaba.org

The original essay included the following image, which is not included in the Creative Commons license.
Mchoro huu na / This image from: Honey Bee Arts - YouTube


Loading...
Loading...
Login to view and post comments
That which draws our attention, gets more attention. 

A wheel that makes noise is more likely to receive oil than other wheels (that also might need oil). We have limited attention, and thus we give our attention to people, projects and problems that stand out. This proverb asserts that there is not necessarily a correlation between the things we give our attention to and the things that actually need our attention.

Another version of the proverb is "the squeaky wheel gets the grease," and though the origin is unknown, American humorist Josh Billings is commonly attributed through his poem "The Kicker" in 1870
I hate to be a kicker,

I always long for peace,

But the wheel that squeaks the loudest,

Is the one that gets the grease.
 
...
Updated 5mo ago
by

Do you have a big dream?

A dream too big for you to ever accomplish on your own? Maybe even too big to be accomplished in one generation?

Some gothic cathedrals in Europe took over 600 years -- more than 20 generations -- to complete! Although the Great Pyramid of Giza seems to have been built much faster (in a single generation), it also took tens of thousands of people.

In Tanzania, the Great Mosque of Kilwa was built in the 11th-14th centuries, rebuilt after earthquake damage, and continued to be remodeled up to the 18th century. It was described in the 1300s by Ibn Battuta. (You can take a 3D virtual tour of Kilwa! Check out the link in sources.)

The wonders of the world, modern and ancient, began as big dreams, dreams that took many generations to fulfill. Each generation continued the work of the past and also contributed to revising the blueprints for the future.

So if you are trying to do something great -- something that will really change the world -- don't expect to do it in one day. And don't try to do it alone. 

Related proverbs:


 Swahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako
If you want to go fast, go alone, if you want to go far, go together 

French:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
from Li Proverbe au Vilain, published around 1190
Modern French: Rome ne s'est pas faite en un jour
Rome wasn't built in a day

Chinese:
冰凍三尺,非一日之寒
Three feet of ice is not the result of one cold day

Scottish Gaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
It is not with the first strike that the tree will fall
...

Image credit: Screenshot from 3D virtual tour of Kilwa Kisiwani created by Zamani Project

Updated 5mo ago
by

Je, una ndoto kubwa?

Ndoto ambayo huwezi kuitimiza peke yako? Labda hata ambayo haiwezi kukamilika katika kizazi kimoja?

Kuna makanisa ya kigothi barani Ulaya ambayo yalichukua zaidi ya miaka 600 -- zaidi ya vizazi 20 -- ili kukamilisha ujenzi!

Ingawa Piramidi kubwa zaidi ya Giza imejengwa kwa kasi (ndani ya kizazi kimoja), ila pia ilichukua makumi ya maelfu ya watu.

Nchini Tanzania, Msikiti Mkuu wa Kilwa Kisiwani ulijengwa katika karne za 11-14, ukajengwa upya baada ya tetemeko la ardhi, na uliendelea kufanyiwa ukarabati hadi karne ya 18. Ulitajwa pia miaka ya 1300 na msafiri Ibn Battuta. (Je ulijua unaweza kuona Kilwa Kisiwani kupitia "ziara ya mtandaoni" yaani 3D Virtual Tour? Ona kiungo chini kwenye "Rasilimali")

Maajabu ya dunia, ya kisasa na ya kale, yalianza kama ndoto kubwa, ndoto ambazo zilichukua vizazi vingi kutimiza. Kila kizazi kiliendeleza kazi ya zamani na pia walitoa mchango wao kwa kubadilisha mipango ya siku zijazo. 

Hivyo bhasi, kama unajaribu kufanya jambo kubwa -- jambo ambalo hakika litabadilisha ulimwengu - usitarajie litafanyika kwa siku moja. Na usijaribu kuijenga peke yako. 

Methali Zinazohusiana:


 Kiswahili:
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako

Kifaransa:
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja

Kichina:
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi

Kigaelic
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
...

Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!

Updated 5mo ago
by
Ustawi wa kiuchumi huenea na huwafikia raia wote wa nchi au eneo. Nchi haiwezi kufaidika bila raia wake wote kufaidika kwa namna moja au nyingine, kama vile baharini, maji yakijaa boti zote zitapanda, wimbi linalokuja litainua boti zote ziwe mitumbwi, jahazi, meli au mashua.

Msemo huo hutumiwa kumaanisha makundi yote yalinufaika kutokana na mabadiliko ya hali, hasa utitiri wa rasilimali, hata kama inaonekana kama zinawafikia matajiri wachache pekee. Nimesikia wafanyakazi wakiona wenzao wamepokea bonasi au kamisheni kubwa wanasema, "A rising tide lists all boats," ikimaanisha mauzo yakipanda, mapato ya kampuni yataongezeka na fursa kwa kampuni, na kwa hivyo, kwa wafanyikazi wote pia. Katika kesi hii, ni wazi wimbi halizinui boti zote kwa usawa au kiasi kilekile.

Wakosoaji wa methali hii wanaweza kulalamika kwamba methali hii inatumika pia ili kuhalalisha mpango au makubaliano yoyote hata kama yatawanufaisha wachache tu. Lakini kwa kawaida msemo huo husemwa  na viongozi kwa matumaini au kama pongezi.

Methali hiyo mara nyingi huhusishwa na John F. Kennedy rais wa Marekani, ambaye aliiitumia katika hotuba yake, mwaka wa 1963 akijitetea baada ya baada ya kukosolewa juu ya ujenzi wa bwawa ulitumia pesa nyingi sana (matumizi ya fujo). Mwandishi wa hotuba za Kennedy (aliyeitwa Ted Sorensen) alifichua kwamba Rais Kennedy alitumia methali hii baada ya kuisoma katika jarida la "New England Council."

Msemo karibu na huu ni "to grow the pie" yaani "kukuza keki" ambayo inamaanisha, kama keki ni kubwa zaidi, washiriki wote watapata keki zaidi hata kama uwiano/asilimia haibadiliki.

Je, unakubali kwamba ustawi mpana wa kiuchumi huwafikia wote?
...
Updated 5mo ago
by