You are now browsing in English. Switch to Swahili
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiingereza. Rudi kwa Kiswahili"
You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Ushindi una baba wengi ila kushindwa ni yatima

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 5mo ago
by
View this proverb in English
Success has many fathers, failure is an orphan
Nyakati za mafanikio, watu wanapenda kuhusishwa na kudai pongezi, hata kama mchango wao ulikuwa mdogo. Lakini mambo yanapoharibika, watu wanakimbia na hulaumiana. Hii ndo maana ya methali "Ushindi una baba wengi, kushindwa ni yatima." (Success has many fathers, failure is an orphan.)

Kwa mfano, fikiria kama umepokea pesa za wawekezaji ili kuanzisha biashara. Biashara ikifanikiwa, wawekezaji wataiona kama mafanikio yao, wataiita "biashara yetu", na itakuwa rahisi sana kutafuta wawekezaji wengi zaidi. Lakini ikiwa biashara imefeli, wawekezaji wako wataiita "biashara yako" na kuomba urudishe pesa zao.

Mara nyingi unaweza kutambua kiongozi halisi wa biashara, shirika au kikundi kwa kuona ni nani anayewajibika nyakati za changamoto na matatizo. Kiongozi bora ni yule ambaye anashiriki sifa na pongezi na wenzake nyakati za kufanikiwa, na anakubali kuwajibika na kulaumiwa nyakati za kushindwa.

Methali hii ilitumika na Rais wa Marekani, John F. Kennedy, mwaka wa 1961, akiongea na waandishi wa habari baada ya mgogoro wa "Bay of Pigs". Lakini inaonekana kwamba chanzo halisi cha methali hii ni cha kale zaidi... inatoka Mwanahistoria wa Roma ya Kale aliyeitwa Tasitus, katika biografia ya jenerali Agrikola kilichoandikwa miaka 98 baada ya kuzaliwa Kristo, akieleza changamoto ambazo jeshi la Roma lilikabiliana nazo katika ukoloni wa Uingereza. 
[Katika vita] sifa ya mafanikio hudaiwa na wote, wakati maafa yanahusishwa na mtu mmoja peke yake.
- Tacitus, Agricola

Je umewahi kuona mfano wa methali hii katika maisha yako? Tunaomba mawazo yako!
Sources
Dr. Makirita Amani - Kisima cha Maarifa
Roma ya Kale

Kiingereza:
John F. Kennedy - Transcript of Press Conference, April 21, 1961
JFK never claimed to be the originator of this proverb and preceded it with "There's an old saying..."
He did popularize the phrase, as you can see from this Ngram chart from Google books, which shows the explosion in usage of the phrase after 1961.

Tacitus

Daily Stoic (from email archives):
It is precisely when things are good that we should be considering the possibility that someday they might not be so good. We should be acquiring allies. We should be doing favors and good for other people—because someday, we’ll need them to do the same for us. 

Portions of the image were made using AI, CC BY
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Kwa kiingereza tunasema "One man's trash is another man's treasure," maana yake, kilichotupwa na mtu mmoja, kinaweza kutumikia mwingine na kuwa na thamani kwake.

Msemo huu hutumika ili kueleza jinsi mapendeleo ya watu hutofautiana, ama kuonyesha matumaini kwamba wanadamu ni wabunifu katika masuala ya kupanga upya au kuchakata vitu vilivyotupwa na wengine.

Kwa mfano, mjasiriamali Gibson Kiwago, mwanzilishi wa WAGA Tanzania, anachakata betri za laptop ili kuleta umeme kwa nyumba na maduka. Jifunze zaidi kuhusu E-Waste (Orodha ya Kusoma)!

Dhana kwamba thamani ya kitu hutegemea mtazamo wako ipo tangu zamani. Chimbuko cha msemo huu ni methali ya Kiingereza iliyotumika karne ya 17:
One man's meat is another man's poison
Nyama na mtu mmoja ni sumu ya mtu mwengine

Je umewahi kuona thamani katika kitu kilichotupwa na mwengine?
...
Updated 5mo ago
by
Many people are afraid to ask questions because they don't want to be seen as stupid. But asking questions is the best way to learn from others.

Asking questions also helps others around you. Have you ever hesitated to ask a question because you thought others already understood... but later you realized they didn't either? 

This proverb is similar to the English saying, “There's no such thing as a stupid question.”
...
Updated 5mo ago
by
Habari zenu wapenzi wa lugha na hekima! Karibuni tena katika kipindi chetu cha leo cha Methali! Methali ya leo ni “Mtoto akilia wembe, mpe.” Je, unaijua? Kwa walezi wengi, inaweza kuonewa… kali sana, au sivyo? Ina maana gani kwako? Je, unakubaliana nayo? Tushirikiane mawazo. 

Nikisikia nitasahau, nikiona nitakumbuka, nikifanya nitaelewa.
-Mwalimu Amos 

Mtoto akitaka wembe, basi mpe ili aelewe kwanini alionywa dhidi ya kucheza nao. Methali hii inaonyesha umuhimu wa kuwapa watu nafasi za kujifunza kutokana na uzoefu wao wenyewe, hata kama wanaweza kuumiwa (kidogo). Vilevile, hata ukikataa kumpa, labda hatatiii na atacheza nao ukiwa nje. Methali hii inaweza kutumika pia kama onyo kwa mtu anayepuuza ushauri au kusisitiza njia yake. Ingawa ni muhimu kusikiliza ushauri na maonyo kutoka kwa wengine, wakati mwingine tunahitaji kuona matokeo ya vitendo vyetu wenyewe ili kuelewa madhara yake. 

Adhabu ya Asili  (Natural Consequences)

Katika eneo la malezi, methali hii inafundisha kanuni ya Natural Consequences (Adhabu Halisi au Adhabu ya Asili). Adhabu ya asili ni matokeo yatakayokuja kwa sababu ya tabia ya mtoto mwenyewe. Tofauti na adhabu ya kutolewa au adhabu ya viboko, adhabu ya asili hujitokeza bila mlezi kujiingilia. Kwa mfano, fikiria kama mwanako amesahau daftari yake nyumbani. Ungefanyaje? Wazazi wengine wanajibu “Singefanya chochote, maana atahitaji kueleza kwa mwalimu wake.” Wengine wanasema “Ningekimbia shuleni ili kumletea daftari, halafu jioni ningempa adhabu.” Ipi bora?  Jibuni hapo chini… 

Swali: Je, mtoto akilia nyoka utampa?

Sawa tumekubaliana mtoto akilia wembe, mpe. Lakini… fikiria kama mtoto analia kitu cha hatari zaidi— je utakubali? Yesu aliwauliza wazazi: “Mtoto akiomba samaki, je, atampa nyoka?” Akilia nyoka, utampa? Wembe unaweza kusababisha jeraha ndogo, lakini si hatari sana kama nyoka mwenye sumu. 
Wewe kama mzazi, utakubali kiasi gani cha hatari ili ajifunze mwenyewe? Kama anaomba kuacha masomo ili kucheza michezo za simu sikuzote? Kama anaomba kumwoa/kumwolewa na mtu ambaye haumwamini katika umri mdogo? Yaani pia kuna maamuzi muhimu ambayo watoto hawako tayari kujifanyia. 
Je wewe kama mzazi unawezaje kuamua au kutambua kama unapaswa kumwokoa / kumlinda mwanako, ama kama unapaswa kumwachia afunzwe na ulimwengu? Wazazi na walezi wote tunaomba maoni yenu!

Nyoka ana madhara.
-Mwalimu Shila  

Utekelezaji wa methali hii katika maisha ya kila siku

Elimu: Watu hukumbuka walichojifunza kwa vitendo kuliko walichoambiwa kwa maneno. Utafute nafasi za kutekeleza kile unachojifunza.
Malezi: Mpe mtoto uhuru na nafasi za kujifunza kupitia uzoefu. Usimtatulie kila jambo, na usiogope anapofeli, kama hakuna hatari wala madhara ya muda mrefu, maana kufeli ni nafasi ya kujifunza kwake.
Kusikiliza: Ukipuuza maonyo na shauri, usishangaye kuona madhara yaliyotabiriwa.
...

Picha hii imetengenezwa na akili bandia (AI)

Updated 5mo ago
by
Widespread economic prosperity typically reaches all citizens of a country or region. A country cannot benefit without all of its citizens somehow benefitting, in the same way that an incoming tide will lift all boats including both the behemoth cruise ships and the tiny canoes.

Occasionally, the adage also may be used when referring to entire groups benefitting from a change in circumstances, particularly an influx of resources that seemingly might reach only individuals. I have heard co-workers respond to their co-workers receiving large sales commissions by saying, "a rising tide lifts all boats," implying that the increase in business for the company will expand the total opportunities for the company (and thus all employees). In this use case, clearly it is understood that the "rising tide" does not lift all boats equally.

Critics of this proverb may dispute its veracity claiming the phrase is erroneously used to justify any type of deal or arrangement that seems to benefit the few, but typically the expression is used with optimism or as a form of mild celebration by leaders, or members of the group themselves.

The proverb is often attributed to John F. Kennedy after he used it in a 1963 speech disputing the claim that a dam construction project had too much pork (wasteful spending). Kennedy's speechwriter (Ted Sorensen) revealed that the New England Council originally used the phrase, which Kennedy borrowed regularly.

A similar phrase is "to grow the pie," which means to make the entire set of opportunities greater, presumably so that everyone can appreciate a larger piece of pie, even if their percentage of the pie does not change.

Do you share the sentiment that broad economic prosperity reaches all?
...
Updated 5mo ago
by