Publisher Taasisi ya Elimu Tanzania (TET)
Mafunzo kazini kwa walimu ni muhimu ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji. Mafunzo haya humwezesha mwalimu kujenga umahiri wa kutekeleza mtaala wa darasa la I na II kwa ufanisi. Moduli hii imeandaliwa ili kukujengea umahiri wa kufundisha masuala mtambuka. Aidha, utajifunza namna ya kumwezesha mwanafunzi kujenga umahiri wa Elimu ya mazingira, Mazingira salama kwa mtoto, Haki za mtoto, Elimu ya jinsia, Stadi za maisha, VVU na UKIMWI na Elimu jumuishi.
Lengo la moduli
Lengo la moduli hii ni kukuwezesha kujenga umahiri wa kufundisha masuala mtambuka kwa wanafunzi wa darasa la I na II kwa ufanisi.
...