Publisher Policy Forum Tanzania
Watanzania wamekuwa na desturi ya kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuboresha maisha yao. Desturi hii ilikuwepo na ilisimamiwa kwa kiasi kikubwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere. Kitabu hiki kinaeleza jinsi ya kushirikiana katika Mipango Shirikishi Jamii wa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (Opportinities and Obstacles to Development). Aidha Mfumo huo ulisisitiza umuhimu wa kuhakikisha kwamba mipango ya maendeleo inahusisha mahitaji halisi ya jamii katika ngazi za msingi (Kata, Vijiji, Mitaa). Mfumo wa O&OD ulioboreshwa unasisitiza umuhimu wa kuijengea uwezo jamii ili iweze kuanzisha na kutekeleza miradi yao wenyewe.
...