You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Umeshafungua akaunti? Ingia

Ingia
Umesahau nenosiri lako?
Sijapata barua pepe ya kuthibitisha

Fungua akaunti mpya

Mafunzo ya Kuboresha Ujuzi na Stadi za Kazi kwa Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa Tanzania Bara
Mchapishaji Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Mwaka 2012
sw
Kurasa 251
Pakua 3.0 MB
Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imeandaa Programu ya Mafunzo ya Maafisa Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa. Kitabu cha kufundishia kimefanyiwa mapitio ili kuweza kuhusisha mambo yote mapya ya muhimu yaliyojitokeza wakati wa kuendesha Mafunzo. Tayari mafunzo kwa Watendaji wa Kata yamefanyika kote nchini; na sehemu kubwa ya Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa. Yote haya yanafanyika kwa ajili ya kuboresha utoaji wa huduma bora kwa Wananchi. Shabaha au lengo kuu la mafunzo haya ni kuwawezesha Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa kuelewa na kuzingatia misingi na utaratibu wa utekelezaji wa majukumu yao kulingana na malengo ya Serikali. Aidha, madhumuni mahsusi ya mafunzo haya ni kuwawezesha Maafisa hao: • Kuelewa Sheria, Muundo na mfumo wa Uendeshaji wa Serikali za Mitaa; • Kuelewa dhana ya Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa; • Kuelewa Muundo wa Utumishi wa Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa; • Kuelewa Kazi , Wajibu na Haki za Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa; • Kuelewa Wajibu wa Afisa Mtendaji wa Kijiji na Mtaa kama Mlinzi wa Amani; • Kuelewa mbinu za Menejimenti na Uongozi, Sheria za Kazi na Usuluhishi wa Migogoro; 10 • Kuelewa Kanuni na Taratibu za Uendeshaji wa Ofisi na Mikutano, Utunzaji wa Kumbukumbu, na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano; • Kuelewa Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini, Ujasiliamali na Uanzishwaji wa Vikundi; • Kuelewa Utaratibu wa Uandaaji wa Mipango Shirikishi Jamii katika ngazi ya Kijiji na Mtaa; • Kuelewa Mbinu za Uandikaji na Usimamizi wa Miradi; • Kuelewa Misingi ya Usimamizi wa Fedha na Taratibu za Manunuzi; • Kuelewa umuhimu wa kuzingatia Sheria na Kanuni za Maadili ya Watumishi wa Umma katika utekelezaji a majukumu yao; • Kuelewa masuala mtambuka yanayohusu Utawala Bora na Demokrasia, Uchambuzi wa Kijinsia na Makundi yenye Mahitaji Maalumu na Usimamizi wa Majanga (Ukimwi na Hifadhi Endelevu ya Mazingira)
...
Shukrani kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
Una maoni juu ya kitabu hiki?
Toa maoni yako ili kuanzisha majadiliano!
Kabla ya kuona na kutoa maoni, lazima uingie kwenye akaunti. Kutengeneza akaunti ni rahisi na bure,na huchukua chini ya dakika 1!
Vitabu vinavyohusiana: Browse all