Tafiti hii ina malengo mahususi matatu:
1. Kuchunguza ikiwa matumizi ya kiingereza katika mazingira ya Afrika ni kikwazo katika ukuaji na kufanikiwa kwa watafiti wa sayansi ya Afya katika ngazi za binafsi, kitaifa na kimataifa, na katika ukuaji wa sayansi ya Afya katika eneo zima la Afrika.
2. Kuchunguza ikiwa matumizi ya kiingereza katika mazingira ya Afrika, yanachangia katika kuletea uwiano usio sawa katika mfumo wa tafiti za sayansi ya afya.
3. Kutoa maoni ya mbinu thabiti za kukabiliana na changamoto zilizoainishwa.
Katika kukamilisha utafiti huu mbinu tofauti zilitumika katika kukusanya taarifa. Kama vile mbinu ya mkabara wa kiubora (qualitative) na mbinu ya mkabara wa kiidadi (Quantitative) katika ukusanyaji wa taarifa.
...