You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Umeshafungua akaunti? Ingia

Ingia
Umesahau nenosiri lako?
Sijapata barua pepe ya kuthibitisha

Fungua akaunti mpya

Kushiriki kwa Wananchi katika Mchakato wa Bajeti Katika Kaunti Zao
Mchapishaji Kituo cha Sheria, Kenya
sw
Kurasa 20
Pakua 3.0 MB
Kama mwananchi, umepewa mamlaka katika mfumo wa ugatuzi. Mamlaka haya pia yana majukumu. Unastahili kushiriki katika maamuzi yanayohusu maisha yako kama vile kuchangia katika kubuniwa kwa bajeti na mipangilio ya serikali. Jukumu lako ni kuelewa kinachofanywa na serikali na kuhakikisha kuwa umehusika kikamilifu katika maamuzi inavyowezekana. Ugatuzi ni kubadili namna uamuzi unavyofanywa na utoaji wa huduma nchini Kenya. Fikiria huduma unazozijali kama vile, afya, maji, masomo au makao. Ni nani anaye amua na kutahmini huduma itakayopewa kipaumbele kifedha? Katika mfumo mpya wa ugatuzi kuna sehemu mbili za utawala; ile ya Kaunti na ile ya Kitaifa. Kaunti zina majukumu ya baadhi za huduma. Serikali ya kitaifa vile vile. Lakini serikali zote mbili zinafaa kufanya kazi kwa pamoja zikishirikiana. Kaunti zina majukumu juu ya elimu ya kimsingi ya utotoni (kama vile ya chekechea), soko, vituo vya afya vya Kaunti, makao, maji, usafi, na zinginezo. Kaunti zinastahili kutunga fedha kwa ajili ya huduma hizi kila mwaka. LAZIMA wananchi wahusishwe katika michakato ya bajeti.
...
Shukrani kwa Kituo cha Sheria, Kenya
Una maoni juu ya kitabu hiki?
Toa maoni yako ili kuanzisha majadiliano!
Kabla ya kuona na kutoa maoni, lazima uingie kwenye akaunti. Kutengeneza akaunti ni rahisi na bure,na huchukua chini ya dakika 1!
Vitabu vinavyohusiana: Browse all