You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Umeshafungua akaunti? Ingia

Ingia
Umesahau nenosiri lako?
Sijapata barua pepe ya kuthibitisha

Fungua akaunti mpya

Mirathi Nchini Tanzania
Mwongozo Kuhusu Mirathi, Wosia na Taratibu za Kimahakama Tanzania
Kimeandikwa na Simon Swai
Mchapishaji Mahakama ya Tanzania
Mwaka 2021
sw
Kurasa 65
Pakua 1.4 MB
"Maisha ni zawadi kutoka kwa Mungu Muumba wetu, zawadi hii ya maisha sio ya milele kuna siku nitakufa. Kifo kinapotokea pamoja na mambo mengine kuna maswali mawili ya msingi huzaliwa; (i) Wapi inakwenda roho yangu? na (ii) Mali na ndugu zangu wanabaki vipi? Kitabu hiki kinajikita kwenye kipengele cha pili tu kwa kuwa kipengele cha kwanza kina watu maalumu wa kukiongelea." - Simon O. Swai (Mwandishi) "Mirathi na taratibu zake ni eneo nyeti kwa sababu linawahusu wafu na walio hai. Licha ya kuwepo sheria zinazosimania eneo hili, ufafanuzi wa sheria hizo na maelekezo mahususi ya Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu kupitia hukumu mbalimbali, bado usimamizi wa mirathi ni changamoto kubwa katika jamii yetu. Wajane, na Watoto hasa waliozaliwa nje ya ndoa bado wanapitia changamoto nyingi kufikia haki zao kupitia mirathi. Kitabu hiki kinajaribu kuelezea kwa lugha nyepesi taratibu za kuzingatia ili kifo kisiwe chanzo cha migogoro katika jamii zetu. Kwa muktadha huo, mwandishi amesisitiza umuhimu wa kuandika wosia na utaratibu wa kufuata. Ameelezea pia, kwa ufasaha mkubwa, taratibu za kimahakama za usimamizi wa mirathi tangu Mahakama za Mwanzo hadi Mahakama ya Rufani. Ni matumaini yangu, kama yalivyo matumaini ya mwandishi, kwamba kitabu hiki ni kwa manufaa na kinaweza kusomwa na kueleweka kwa kila mwanajamii. Chafaa pia wa matumizi ya Wanasheria wanaosimamia mashauri ya mirathi, Mahakimu, Majaji na kufundishia vyuoni kama kitabu cha rejea." -Ilvin Claud Mugeta, Jaji, Mahakama Kuu Kigoma
...
Shukrani kwa Tanzania Legal Information Institute
Una maoni juu ya kitabu hiki?
Toa maoni yako ili kuanzisha majadiliano!
Kabla ya kuona na kutoa maoni, lazima uingie kwenye akaunti. Kutengeneza akaunti ni rahisi na bure,na huchukua chini ya dakika 1!
Vitabu vinavyohusiana: Browse all