Publisher Climax Solutions Arusha
Maisha yangu hapo nyuma hayakuwa mazuri, maana yalikosa ushuhuda na hayakuwa na uhalisia wa MUNGU ndani yake. Ni kwa sababu nilifanya mambo mengi ya kijinga, na yote hayo yalitokea sio kwa kupenda ila ni kwa sababu nilikuwa na ujinga mwingi. Yaani sikuwa nafahamu vitu vingi vya muhimu, na nilikosa mafundisho mengi sahihi kuhusu maisha. Nilikuwa msichana mjinga kwa sababu nilifanya mambo mengi nisiyo na uelewa nayo, na mengi pia sikufahamu madhara yake, na hayo yote yalinipelekea kufanya uovu mwingi ulioniumiza sana.
...