You are now browsing in English. Switch to Swahili
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiingereza. Rudi kwa Kiswahili"
You need to login to view profiles OR to update your profile

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
New announcements
Discussions
Proverbs

Chema chajiuza, kibaya chajitembeza

Join
or login
to VOTE for Proverb of the Month
Votes
0
Updated 4mo ago
by
Tofautisha na linganisha matunda na pipi. Matunda yameiva, yana ladha halisi, yamejaa virutubisho na vitamini -- kweli yanajiuza yenyewe.

Kwa upande mwingine, mfuko wa pipi unalia “nisikilize!”, kwa rangi kali, na kauli mbiu zinazolipuka *BOOM*! Lakini chini au nyuma ya kinachong'aa, tunajua kwa kkweli pipi ni sukari tupu tu yenye rangi na ladha bandia ya matunda.

Kama nyani, binadamu hupenda matunda kwa sababu yanatupatia nishati pamoja na lishe na virutubisho. Pipi hutoa nishati bila lishe halisi (Kalori tupu). Pipi huiga tunda. Usidanganywe!

Kizuri hakihitaji kutangazwa, maana ubora hujieleza yenyewe. Kama wachumi wasemavyo, “demand” inazidi “supply”. Matangazo yanaweza kutuahidi furaha, uzuri, upendo, mali au heshima. Lakini jiulize, je, inawezekana kwa kweli? Coca-Cola sio dawa ya upendo.

Methali hii inatukumbusha thamani ya ubora wa kweli kuliko muonekeano maridadi. Methali hii hutumika wakati msemaji ana mashaka juu ya mtu anayejisifu au kujivunia kupita kiasi.

Tuwe kama kikapu cha matunda: mwazi na mwema. Sifa hizi zitawavuta wengine kwako — angalau wao wanaoelewa kwamba “Chema chajiuza, kibaya chajitembeza!”

Methali zinazohusiana:
Vingaravyo vyote si dhahabu

Don’t judge ya book by it’s cover
Usihukumu kitabu kwa kava yake (muonekeno)

Appearances are deceptive
Maonekano hudanganya
 
高嶺の花
Hana yori dango
Chakula [ni bora] kuliko maua
Loading...
Loading...
Login to view and post comments
Methali hii ya Kiingereza "To the victor go the spoils" inatafsirika pia kama "Mshindi ndiye anayechukua vyote" au "Mshindi hupokea nyara zote."

Mshindi wa shindano ndiye anayepokea tuzo. Huwa anachukua asilimia kubwa ya faida ama faida zote, na hata manufaa zaidi ya yale yaliyokuwa yakipiganiwa.

Katika vita, nyara zinaweza kuwa ardhi, mamlaka au rasilimali nyingine zinazotafutwa. Katika shughuli zingine nyara zinaweza kuwa sifa, pesa au fursa. Methali hii hutumika ili kueleza matokeo yasiyo sawa au kutukumbusha kwamba katika migogoro mingi ni mshindi ndiye atakayechukua yote, asilimia kubwa, au angalau, kupendelewa. Angalia sehemu ya vyanzo kwa maelezo ya muktadha kuhusu chimbuko la methali hii, mwanasiasa wa Marekani katika miaka ya 1830 (Kiingereza).
...
Updated 4mo ago
by

Ufafanuzi


Methali hii ya Kiingereza inatafsirika pia kama "Kalamu ina nguvu kuliko upanga au jambia" au " Kalamu ni kali kuliko upanga." Katika methali hii, jambia au upanga unaashiria nguvu na ukatili, na maana ya kalamu ni maneno. Ingawa upanga unaweza kushinda kwa nguvu, kalamu inaweza kuwashawishi, kuwahamasisha, na kuwaelimisha watu. Sio kila mtu ana silaha za kuwalazimisha watu wengine kufanya kile anachotaka, lakini kila mtu ana uwezo wa kubadilisha ulimwengu kupitia kile anachofikiria, kusema na kuandika kwa maneno. 

Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
 - Methali ya Kiswahili

Methali hii ni kweli kwa sababu mara nyingi maneno huchochea na kudhibiti jinsi watu wanavyotumia nguvu na silaha zao. Kwa mfano, kupitia sheria, maneno ya viongozi, mahakimu na majaji yana uwezo wa kuwafunga watu gerezani au hata kuwaua. Kutoa hotuba ya moto kwa umati wa watu wenye hasira kunaweza kuleta ghasia kali na madhara mengine (ona Juliasi Kaizari).

"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)

Lakini pia, methali hiyo inatukumbusha nguvu ya upinzani usio na vurugu kwenye kuleta mabadiliko ya kudumu, kanuni iliyotetewa na kuonyeshwa na watu kama Mahatma Gandhi, Martin Luther King, na Nelson Mandela.  Angalia pia: Insha ya "Civil Disobedience"  na Henry David Thoreau, pamoja na Tamthilia mashuhuri ya "Antigone" na Sophocles.

Chimbuko


Nukuu hii ya "kalamu ina nguvu kuliko upanga" ilipata umaarufu kupitia tamthilia ya "Richelieu: au The Conspiracy"  na Edward Bulwer-Lytton (mwaka wa 1839, ukurasa wa 47). Lakini hakika wazo lilikuwepo kabla.

Wengine wanasema chimbuko halisi la methali hii ni Hadithi ya Ahikar. Kitabu hiki kiliandikwa takriban miaka 600 kabla ya kristu, na ni chimbuko la methali zingine kama "Ndege mkononi ana thamani ya wawili mtini"). Katika toleo letu, mfasiri hakuweza kusoma maandishi kutokana na hali ya karatasi, na maneno yalikatika. (Ukurasa 171/274
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na  ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa  ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Je, hili ndilo chimbuko halisi la methali hii, miaka zaidi ya 2,500 iliyopita? Muwe majaji...

Chanzo karibu na methali hii pia kinaonekana katika Agano la Kale:
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia

Na vilevile katika Shakespeare: 
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)

 Je, unakubali kalamu hushinda jambia? Toa maoni yako hapo chini!
...

CC BY Unaruhusiwa kunakili & kusambaza mchoro huu na makala hii bila idhini, ukitaja tu chanzo (www.maktaba.org)

Updated 4mo ago
by
Methali hii inatoka Kiingereza "A penny saved is a penny earned." Maana yake, mia inayobaki mfukoni inaweza kutumiwa kwajali ya madhumuni mengine. Mifano: Inaweza kutumika kwaajili ya kununua kitu kingine, unaweza kukopesha au kuwekeza ili kuingiza riba au pesa zaidi katika siku zijazo. Katika uchumi, kanuni hii inaitwa Opportunity Costs (gharama za kukosa fursa). Tunapotumia pesa au muda kwa jambo limoja, tunapoteza pia fursa ya kuzitumia kwajili ya jambo lingine.

Methali hii huhusishwa na Benjamin Franklin, lakini si chimbuko halisi, wala hakuandika msemo huu kamili. Misemo karibu na huu ilichapishwa kabla yake. Kwa mfano: 

A penny spar'd is twice got.
Senti iliyookolewa hupatikana mara mbili.
- Outlandish Proverbs by George Herbert (1640)  
 
Katika Poor Richard's Almanac (1736), Benjamin Franklin alinukuu methali hii na alifafanua vizuri kanuni ya Opportuinty Cost hivi:

Vidokezo kwa Wale Wanaotaka kuwa Matajiri

Matumizi ya pesa ndiyo faida zote zinayopatikana ukiwa na pesa.
Kwa pound [£] sita kwa mwaka [yaani riba] unaweza kutumia  £ mia [yaani kupitia mkopo], kama unajulikana kama mwaminifu na mwenye busara.
Anayetumia groat [senti 4] kwa siku bure, hutumia pound £ zaidi ya sita kwa mwaka, ambazo ni bei ya kujipatia matumizi ya pound £ mia moja.
[Kwa hivyo] Anayepoteza muda wake wa thamani ya groat [senti 4] kwa siku, siku moja na nyingine, anapoteza fursa ya kutumia pound mia moja kila siku.
Anayepoteza muda wa shilingi tano kwa uvivu hupoteza shilingi tano, ni kama amezitupa tu baharini.
Anayepoteza shilingi tano sio tu kwamba anapoteza kiasi hicho, bali anapoteza pia faida yote ambayo ingeweza kupatikana kwa kuzitumia katika shughuli zake, ambayo, akiwa kijana, wakati wa uzee ingefikia kiasi kikubwa cha fedha.
Tena: anayeuza kwa mkopo huongeza bei ya kile anachokiuza kwa kiasi sawa riba angaliingiza na pesa hizo kwa kipindi ambacho atazikosa. Kwa hivyo, anayenunua kwa mkopo hulipa riba kwa kile anachonunua, na anayelipa pesa mara moja kwa kila anachonunua hukoa fursa ya kuzikopesha kwa wengine, kwa hivyo aliye na kitu alichonunua ameshalipa riba kwa matumizi yake.
Hata hivyo nasema kulipa mara moja unaponunua ni bora, kwa sababu anayeuza kwa mkopo anatarajia kupoteza asilimia tano ya mikopo; kwa hivyo anaongeza bei ya kile anachokiuza kwa asilimia ileile ili kuzuia hasara. Wanaolipa kwa mikopo hulipa kodi mara moja. Anayelipa kwa pesa mara moja anaweza kuzuia kodi hii
"Senti iliyohifadhiwa ni senti mbili hakika;
[haba] kwa siku ni [nne] kwa mwaka."
 
Basi, unapofikiria kutumia muda au pesa zako katika jamblo fulani, jiulize, ningekosa, ningepata fursa zipi? Pesa hizi zingeweza kutumikia vipi? Mifano: kumkopesha mwingine, kurudisha madeni uliyonayo, kubuni kitu kipya au kuwekeza katika kitu ambacho kinaweza kuleta faida kubwa mbeleni.
...
Updated 4mo ago
by
by Magreth Lazaro Mafie 🇹🇿
🏆 Proverb Essay Contest 
🥉 Third Place Winner
(English translation from Kiswahili)
How many times have you heard “Mchumia juani hulia kivulini” (One who works in the sun, eats in the shade). This is a Swahili (Bantu) proverb meant to encourage people in their everyday activities, to have faith that there will be a day when they will enjoy the fruits of their work.

This proverb gives people strength, diligence, heart, courage, hope and skill in working. The worker believes that hard work brings a good harvest that will allow him to relax in the shade as he eats the fruits of his labor. 

The following poem shows “One who works in the sun” in their daily responsibilities.
I fear neither sun nor rain, making my tomorrow
I fear neither injuries nor pain, because all are temporary
Scorching sun and work are my custom, so that happiness comes in life
The street vendor, the farmer, the [port boys] and their fisherman and the sun, in search of tomorrow
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

It's noon, the sun overhead, in my head I have the harvest, sweat is dripping,
The sun has set now, the oar on the beach, exhausted in bed, nets in the sea,
At home on fourth street, captain of the family, may I pull happiness from hard labor
Now the sun is rising, walking the path to look for a bite,
One who works in the sun, eats in the shade, I am still searching for shade.

Once there was a farmer. He spent his whole life in agriculture. Thus his times for pleasure were few. People in his village called him a skilled farmer. He built a house by selling part of his crops, he educated his children through farming.

This farmer was a diligent man, he always learned the principles of being a good farmer, so as time went by, he harvested many crops from his fields. Many people were really amazed to see the big changes in his family. He made many investments in his village, the farms, houses, and shops, and many livestock came from his farm.

Many people came to take wisdom from the skilled farmer. He always told them "One who works in the sun, eats in the shade. The hoe has given me respect in the village, me and my family. My life now is going on a path of certainty, I am in the shade, enjoying the fruits of my labor in the sun. I, the son of that skilled farmer, am proud of my upbringing, and his responsibility, because work in the sun today has made us rest and eat in the shade. The true meaning of “he who works in the sun” can be seen in actions. Your diligence is your sun and the shade is the fruit of your diligence.

This story is complemented by the story of "Mabala the Farmer" by Richard S. Mabala (1989). Mabala was a port worker then he was demoted, so he chose to return to the village of Morogoro. Mabala was careless, drunk and obstinate. Mabala went to the farm with a gallon of booze, he drank it and went to sleep, when he woke up, he called out to his wife but there was no answer except the sound of the hoe tik-tok, tik-tok.

Mabala was obstinate, he watered the fields with sugar, thinking it was fertilizer, but in the end he changed to become a skilled farmer, becoming “one who works” in the sun so that his family could eat in the shade. Do you feel that Mabala is “one who works in the sun”? In the family or in the community, what’s your image of a skilled farmer?

In conclusion, this story on the proverb "Work in the sun, eat in the shade" shows us a good vision in everything we do in our daily lives. Also proverbs like "Subira yavuta kheri” (Patience brings blessings), "Mgaa na Upwa hali wali mkavu” (He who combs the beach at low tide doesn’t eat dry rice) all have similar themes; they exist to give the community strength and hope each task undertaken to pursue their goals.

...
Updated 4mo ago
by