Watu hutaka furaha mpya. Huwa tunaona kuwa watu wengine wana bahati zaidi kuliko sisi wenyewe. Mazao daima ni bora katika shamba la jirani yetu; ng'ombe wake hutoa maziwa zaidi.
दूर के ढोल सुहावने लगते हैं
Ngoma za mbali husikika vizuri
隔籬飯香
Wali wa jirani hunukia vizuri
隣の芝生は青く見える
Majani ya jirani huonekana kijana zaidi
соседняя очередь всегда движется быстрее
Foleni nyingine husogea kwa kasi zaidi
Mwanangu, mguu wa kondoo katika mkono wako mwenyewe ni bora kuliko bega zima katika mkono wa mwengine; Afadhali kondoo mdogo aliye karibu na wee kuliko ng'ombe aliye mbali; Afadhali shomoro aliyeshikwa mkononi kuliko ndege elfu warukao angani; vazi ulilo nalo ni afadhali kuliko vazi la zambarau usiloliona.
- Hadithi ya Ahikar (ukurasa wa 110)
Un tiens vaut mieux que deux tu l'auras
'Shika-hii-hapa" moja ina thamana kuliko 'nitakuletea-baadaye' mbili
明日の百より今日の五十
Hamsini leo ni bora kuliko mia kesho
Meglio un uovo oggi che una gallina domani
Bora yai leo kuliko kuku kesho
Ukitaka kwenda haraka, nenda peke yako, ukitaka kwenda mbali, nenda na wenzako
Rome ne fu[t] pas faite toute en un jour
Kutoka kitabu cha Li Proverbe au Vilain kilichochapishwa takriban mwaka wa 1190
Kifaransa cha kisasa: Rome ne s'est pas faite en un jour
Maana yake: Roma haikujengwa kwa siku moja
冰凍三尺,非一日之寒
Mita ya barafu sio kwa sababu ya siku moja ya baridi
Chan ann leis a’ chiad bhuille a thuiteas a’ chraobh
Sio pigo la kwanza linaloangusha mti
Picha: Shukran kwa Zamani Project waliounda ziara ya mtandaoni ya Kilwa Kisiwani!
Silaha za siku hizi ni kalamu na karatasi.
- Methali ya Kiswahili
"Ukinipa picha, nitakupa vita."
- William Randolph Hearst
(Mwandishi wa habari na mchapishaji wa magazeti, Marekani)
Dhibiti kinywa chako kwa uangalifu ...[ILIKATA]... na ufanye moyo wako kuwa mzito(?), kwa maana neno linalosemwa ni kama ndege, naye alitamkaye ni kama mtu asiye na ...[ILIKATA]... ufundi wa maneno una nguvu zaidi kuliko ufundi wa ...[ILIKATA]...
- Hadithi ya Ahikar, Ukurasa wa 171/274
Kwa maana neno la Mungu ni hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Waebrania 4:12, Biblia
Wengi wanaovaa panga huogopa kalamu.
-William Shakespeare
Tamthilia ya Hamlet, Sehemu ya 2, Onyesho la II (ukurasa wa 59)
CC BY Unaruhusiwa kunakili & kusambaza mchoro huu na makala hii bila idhini, ukitaja tu chanzo (www.maktaba.org)