You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Umeshafungua akaunti? Ingia

Ingia
Umesahau nenosiri lako?
Sijapata barua pepe ya kuthibitisha

Fungua akaunti mpya

Mshamba Fani Hivi
Riwaya ya Vijana
Kimeandikwa na Brother Elihuruma Maruma
Mwaka 2020
sw
Kurasa 176
Pakua 0.8 MB
Visa na mikasa ya Mapenzi, Usaliti, Utekaji, Siasa na Imani. ilisikika kwa mbali sauti nzuri za ndege pamoja na majogoo machache yakiwika japo kwa uchovu kwa sababu ya baridi na upepo mkali wa kiangazi. Giza nalo lilikuwa bado totoro na hapakuwa na mwanga wa aina yeyote nje. Hivi ilikuwa ni mishale ya saa kumi usiku kuelekea saa kumi na moja. Katika hali hiyo ilisikika pia sauti ya mguno na mahangaiko ya mwanamke mmoja aliyekuwa katika nyumba ndogo ya udongo yenye vyumba viwili iliyoezekwa kwa nyasi. Mwanamke huyu makamo mwenye umri wa miaka 44 aliyejulikana kwa jina la Wankembeta alikuwa mjamzito, na ukulele huu ulikuwa ni wa uchungu wa kujifungua. Mama huyu mjane alifiwa na mumewe miezi nane iliyopita alikuwa amejilaza kwenye kitanda chake cha Kamba pamoja na mdogo wake aliyeitwa Lumba....
...
Kitabu hiki kinasambazwa na Maktaba.org bila malipo kwa idhini ya Mwandishi Bro. Elihuruma Maruma. Tunamshukuru sana.
...
Shukrani kwa Brother Elihuruma Maruma
nakala 1
Kinapatikana Arusha bila malipo! Omba
Kimechangiwa na
Una maoni juu ya kitabu hiki?
Toa maoni yako ili kuanzisha majadiliano!
Kabla ya kuona na kutoa maoni, lazima uingie kwenye akaunti. Kutengeneza akaunti ni rahisi na bure,na huchukua chini ya dakika 1!
Vitabu vinavyohusiana: Browse all