Visa na mikasa ya Mapenzi, Usaliti, Utekaji, Siasa na Imani.
ilisikika kwa mbali sauti nzuri za ndege pamoja na majogoo machache yakiwika japo kwa uchovu kwa sababu ya baridi na upepo mkali wa kiangazi. Giza nalo lilikuwa bado totoro na hapakuwa na mwanga wa aina yeyote nje. Hivi ilikuwa ni mishale ya saa kumi usiku kuelekea saa kumi na moja. Katika hali hiyo ilisikika pia sauti ya mguno na mahangaiko ya mwanamke mmoja aliyekuwa katika nyumba ndogo ya udongo yenye vyumba viwili iliyoezekwa kwa nyasi.
Mwanamke huyu makamo mwenye umri wa miaka 44 aliyejulikana kwa jina la Wankembeta alikuwa mjamzito, na ukulele huu ulikuwa ni wa uchungu wa kujifungua. Mama huyu mjane alifiwa na mumewe miezi nane iliyopita alikuwa amejilaza kwenye kitanda chake cha Kamba pamoja na mdogo wake aliyeitwa Lumba....
...