Publisher Taasisi ya Elimu Tanzania (TET)
UJUMBE KUTOKA TAASISI YA ELIMU TANZANIA : Miaka ya awali ya mtoto ni kipindi muhimu katika ukuaji na ujifunzaji wake. Katika kipindi hiki, mtoto anajenga misingi ya ujifunzaji endelevu inayomwezesha kukua kiakili, kimwili, kijamii na kimaadili. Ufanisi katika kujenga misingi hii unategemea kwa kiasi kikubwa ubora wa mtaala unaotumika katika Elimu ya Awali. Ni suala la kujivunia kuwa na mtaala wa Elimu ya Awali unaoakisi jitihada za serikali katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi nchini, kupitia sekta ya elimu kama inavyobainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025. Natumaini kuwa maudhui ya mtaala huu yatamwongoza mtumiaji katika kumwezesha mtoto kujenga umahiri muhimu utakaomsaidia kujifunza na kujitawala. Ninafahamu kuwa tunaishi katika jamii inayobadilika ambayo mahitaji yake pia hutegemea mabadiliko ya sayansi, teknolojia na vigezo vya kiuchumi. Hivyo mtaala huu utahakikiwa na kuboreshwa pindi inapobidi ili uweze kuendana na mabadiliko hayo
...