You are now browsing in Swahili. Switch to English
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiswahili. Rudi kwa Kiingereza"
Lazime uingie akaunti ili kubadilisha wasifu wako au kuona wasifu wa wengine

Umeshafungua akaunti? Ingia

Ingia
Umesahau nenosiri lako?
Sijapata barua pepe ya kuthibitisha

Fungua akaunti mpya

Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Tathmini ya Hali ya Lishe, Unasihi na Huduma za Lishe (NACS)
Kitabu cha Mwezeshaji wa Mafunzo kwa Watoa Huduma katika Ngazi ya Jamii
Mchapishaji Ghala la Mkulima
Mwaka 2017
sw
Pakua
4.3 MB
Lishe ina uhusiano mkubwa na afya. Lishe duni au utapiamlo unaotokana na ulaji duni na maradhi ni mojawapo ya matatizo makubwa ya afya nchini Tanzania. Utapiamlo unawaathiri zaidi watoto wenye umri chini ya miaka mitano na akina mama walio katika umri wa kuzaa hasa wajawazito na wanaonyonyesha. Utapiamlo kwa wanawake wajawazito na wanaonyonyesha unaweza kusababisha madhara ya muda mrefu kwa watoto wao. Pia, utapiamlo unahusishwa na magonjwa sugu kama vile kifua kikuu (TB) na UKIMWI, ambayo ni matatizo makuu hapa nchini Tanzania. Upungufu wa lishe katika kipindi cha miaka miwili (siku 1,000) ya mwanzo ya maisha ya mtoto unahusishwa na maradhi, vifo na uchelewaji wa ukuaji wa mwili na maendeleo ya akili. Upungufu huo unaweza kuathiri utendaji wa akili, matokeo ya uzazi, afya na tija ya kiuchumi wakati wa utu uzima. Watoto wachache tu wenye utapiamlo pamoja na watu wazima wametambuliwa na kutibiwa kwa kupitia vituo vya kutolea huduma ya afya. Lakini wengi wa watu hawa wakisha ruhusiwa toka vituo vya kutolea huduma ya afya baada ya kutibiwa utapiamlo huwa hawarejei tena kwa ajili ya ufuatiliaji. Watoa huduma katika ngazi ya jamii watasaidia katika kuimarisha utoaji wa huduma kati ya vituo vya kutolea huduma ya afya na jamii ili watu wenye utapiamlo waweze kutambuliwa, kutibiwa na kufuatiliwa mapema na hivyo kuboresha hali zao za lishe, kugundua dalili za utapiamlo mapema na kuepuka maambukizi. Shughuli hizi zitaimarisha mwendelezo wa utoaji wa huduma kati ya vituo vya kutolea huduma ya afya na jamii.
...
ISBN: 9789976910933
Shukrani kwa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania
Una maoni juu ya kitabu hiki?
Toa maoni yako ili kuanzisha majadiliano!
Kabla ya kuona na kutoa maoni, lazima uingie kwenye akaunti. Kutengeneza akaunti ni rahisi na bure,na huchukua chini ya dakika 1!
Vitabu vinavyohusiana: Browse all