You are now browsing in English. Switch to Swahili
In Swahili: "Sasa unavinjari kwa Kiingereza. Rudi kwa Kiswahili"
You need to login to view profiles OR to update your profile

Have an account? Login

Log in
Forgot your password?
Didn't receive your confirmation email?

Create a new account

Shungu Mtukutu
Written by Simon Kasubi
Publisher Readit Books
Published 2001
sw
Pages 26
Hapo zamani za kale katika kijiji cha Mjimwema, aliishi Mzee mmoja na mke wake. Mzee Butamo na mkewe Mama Masare walipata watoto wawili. Wa kike aliyeitwa Ng'washi na wa kiume aliyeitwa Shungu. Ng'washi aliyekuwa mkubwa kwa Shungu alikuwa ni mtoto mwenye adabu na msikivu. Licha ya kuwa na heshima kwa watu wote pia alikuwa n.i mchapa kazi hodari. Siku zote alifuatana na wazazi wake kwenda shamba ambako alilima bila uvivu hadi muda wa kurudi nyumbani ulipowadia. Kutokana na tabia yake nzuri na uchapakazi alioonyesha, watu wote pale kijijini wakampenda na kuwa mfano bora wa watoto wengine. Shtmgu alikuwa mkaidi, mvivu na asiyekuwa na heshima. Kila ilipowadia muda wa kwenda shamba ndiyo kwanza alivuta shuka na kujidai kukoroma. Alipoamshwa alitoa visingizio chungu nzima iii mradi tu aendelee kulala. Wazazi wake wakishaondoka alichukua manati yake na kuanza kuzurura ovyo kijijini. Huko mitaani akawa ni mtoto mwenye sifa mbaya na alikuwa mgomvi. Akawa hawaamk.ii watu waliomzidi umri wala kuwasaidia mizigo kama wanavyofanya watoto wengine.
...
ISBN: 9987210341
Create an account to...
View comments and discuss this book!
Before viewing or adding comments, you must create an account. It takes just seconds!
Related books: Browse all