Hapo zamani za kale katika kijiji cha Mjimwema, aliishi Mzee mmoja na mke wake. Mzee Butamo na mkewe Mama Masare walipata watoto wawili. Wa kike aliyeitwa Ng'washi na wa kiume aliyeitwa Shungu. Ng'washi aliyekuwa mkubwa kwa Shungu alikuwa ni mtoto mwenye adabu na msikivu. Licha ya kuwa na heshima kwa watu wote pia alikuwa n.i mchapa kazi hodari. Siku zote alifuatana na wazazi wake kwenda shamba ambako alilima bila uvivu hadi muda wa kurudi nyumbani ulipowadia. Kutokana na tabia yake nzuri na uchapakazi alioonyesha, watu wote pale kijijini wakampenda na kuwa mfano bora wa watoto wengine. Shtmgu alikuwa mkaidi, mvivu na asiyekuwa na heshima. Kila ilipowadia muda wa kwenda shamba ndiyo kwanza alivuta shuka na kujidai kukoroma. Alipoamshwa alitoa visingizio chungu nzima iii mradi tu aendelee kulala. Wazazi wake wakishaondoka alichukua manati yake na kuanza kuzurura ovyo kijijini. Huko mitaani akawa ni mtoto mwenye sifa mbaya na alikuwa mgomvi. Akawa hawaamk.ii watu waliomzidi umri wala kuwasaidia mizigo kama wanavyofanya watoto wengine.
...