Mchapishaji Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Tanzania - Ministry of Health and Social Welfare
Maambukizo ni moja ya vyanzo vinavyoongoza katika kusababisha maradhi na vifo nchini Tanzania. Pia ni miongoni mwa vyanzo vitano vya vifo vya akina mama wakati wa uzazi. Kutibu maambukizo ni gharama kubwa na hata matibabu yakifanikiwa yanaweza kuacha madhara ya muda mrefu. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ina wajibu wa kuhakikisha kwamba huduma za afya zinazotolewa ni bora na salama kwa watu wote. Kukinga maambukizo ni suala muhimu katika utoaji wa huduma bora za afya.
...