Ugonjwa wa Parkinson ni nini?
Ugonjwa wa Parkinson ni ugonjwa unaozidi polepole katika mfumo wa neva ya kati. Watu wenye ugonjwa wa Parkinson, polepole hupoteza uwezo wa kudhibiti kabisa harakati za usogezaji wa mwili. Ilielezwa kwa mara ya kwanza mwaka 1871, na Daktari wa Kiingereza kwa jina Daktari Parkinson ambaye aliuita “Shaking Palsy”.Hatimaye, ugonjwa huu ambao Dkt. Parkinson aliuelezea kwa mara ya kwanza ukaitwa baada yake. Duniani kote, watu milioni minne hadi sita wanakabiliwa na hali hii na katika Afrika kuna ongezeko la idadi ya watu wanaoripotiwa kuwa wanaishi na ugonjwa wa Parkinson.
...