Atlasi hii ya Tanzania inasisitiza kwenye mahitaji mahususi kwa wanafunzi na waalimu wa Shule za Msingi za Tanzania. Atlasi inatoa taarifa kwa upana na kinaganaga kuzingatia Muhtasari Mpya wa Jiografia kwa Darasa la 3 mpaka la 7.
Atlasi ya Ujifunzaji Shirikishi ina tofauti ya pekee kwa sababu inampa mwanafunzi ufafanuzi unaohitajika kuhusu dhana muhimu za ramani:pamoja na shughuli nyingi ambazo zimewasilishwa katika viwango mbalimbali kwa kila darasa kulingana na ugumu wa maudhui yaliyomo kwenye Muhtasari.