Jiandikishe upate habari na vitabu bure!
Uwazi na Ukweli: Kitabu cha Tatu
Kimeandikwa na Benjamin W. Mkapa
Mchapishaji Mkuki na Nyota
sw
Hiki ni kitabu cha Tatu katika mfululizo wa vitabu vya Uwazi na Ukweli vyenye mkusanyo wa hotuba za kila mwisho wa mwezi za Mheshimiwa Rais Benjamin W. Mkapa anazotoa kwa Taifa. Sambamba na kuendeleza falsafa yake ya “Uwazi na Ukweli”, Rais Mkapa anaeleza na kufafanua kwa mapana na marefu masuala mbalimbali yanayogusa maslahi ya Taifa katika maeneo kama vile: • Utandawazi na Ushirikiano baina ya mataifa duniani; • Demokrasia na wajibu wa viongozi wa mataifa mbalimbali kwa wananchi wao; • Usalama wa chakula na matatizo ya misaada kutoka mataifa makubwa; • Maendeleo na ufikiwaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia; na Tathmini ya ubinafsishaji. Pia anaeleza juu ya Mpango wa kurasmisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) ambao Rais anaamani utafungua njia kwa makabwela kujipatia mikopo na mitaji ya kuanzishia na kuendeshea miradi midogomidogo ya kujikimu kimaisha na hivyo kupambana na umaskini. Kitabu hiki kitawafaa Watanzania wote hasa wanapotaka kufuatilia kwa karibu utendaji kazi wa serikali waliyoiweka madarakani. Ni kumbukumbu muhimu kwa maendeleo ya Taifa na katika kuelewa maswala ya siasa, jamii na uchumi wa jamii ya Tanzania.
...
link: https://mkukinanyota.com/product/uwazi-na-ukweli-3/
...
ISBN: 9789987417391
Shukrani kwa Mkuki na Nyota
nakala 1
Kinapatikana Arusha bila malipo! Omba
Una maoni juu ya kitabu hiki?
Toa maoni yako ili kuanzisha majadiliano!
Kabla ya kuona na kutoa maoni, lazima uingie kwenye akaunti. Kutengeneza akaunti ni rahisi na bure,na huchukua chini ya dakika 1!
Vitabu vinavyohusiana: Browse all

No Books Found

Based on the filters you selected, there are currently no books.