Publisher Beeline Printing Ltd., Nairobi
Kufatana na Msingi ambao makanisa yote yenye uanachama katika Baraza la Makanisa Duniani yamidhini, Baraza hilo ni "ushirika wa makanisa yanayomkiri Bwana Yesu Kristo akiwa Mungu na Mwokozi kufuatana na Maandiko Matakatifu, na kwa hiyo yanayojaribu kwa pamoja kutekeleza wito wao ulio mmoja kwa utukufu wa Mungu aliye mmoja, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu."
Tumaini (maono ya umoja wa makanisa halikutoweka kupitia karne nyingi za kutengana na kugombana kati ya Wakristo. lakini mwishoni mwa karne ya kumi na tisa, watu wa sehemu kadhaa walisikia wito wa kuteneneza mitengano, ambayo wakati wote imedhuru ushuhuda wa Kikristo. Ndio mwanzo wa oikumene wa siku hizi ambao ushirika wa pekee wa Baraza la Makanisa Duniani una mizizi yake.
...