You need to login to view profiles OR to update your profile

Have an account? Login

Log in
Forgot your password?
Didn't receive your confirmation email?

Create a new account

Sign up for news and free books by email!
Diwani ya Ustadh Andanenga
Publisher Benedictine Publications Ndanda
Published 1993
sw
Pages 114
Diwani ya Ustadh Andanenga imetumia vipengele vya mchomozo ambavyo ni takriri na ukengeushi. Kipengele cha takriri silabi / mizani ndicho kimejitokza zaidi. Diwani hii iliandikwa katika cha mwaka 1990, msanii akiwataka wananchi kufanya kazi na kujitegemea ili kuepuka kutegemea misaada kwa Wazungu. Diwani inawataka watu waishi kwa kupendana , wathamini lugha ya Kiswahili kwani huo ni ukombozi wa kifikra endapo tutathamini utamaduni wetu. Mifano ya mashairi: 63. Fanya ulizio 1. Leo ninajambo, nataka kwambia Sikiza mrembo, badili tabia Mapenzi ya shombo, sitavumilia Nataka mapambo, sitaki udhia. 2. Mapenzi ni ladha, iso mithilika Hayana karadha, yataka hakika Na kitu bughudha, penzi hufumuka Hayataki adha, mapenzi ni shuka. 3. Mapenzi ni dawa, ya watu wawili Wagonjwa hupowa, wakawa sahali Wakavuta hewa, hata ilo mbali Kama hujajuwa, kaa ujadili. 4. Na wala si haja, wengi kuambata Mmoja ni tija, ni huyo limbata Lumbata mmoja, pendo la mashata Pendo la faraja, liwe la kumeta. 5. Kama huyajui, fanya ulizio Pendo makuri, halina shikio Nasema sizui, naapa apio Kama hutambui, uliza wenzio. 6. Na hapa ni mwisho, shika yangu haya Lisipate chosho, ukaja limwaya Fanya linganisho, meno na mataya Penzi suluhisho, katika kayaya. 64. Ai ghalibi ya ria 1. Shairi lako shababi, somo bingwa wa utunzi Nakiri yako kalibi, ya kwamba ukimfunzi Akuzidishe Wahabi, umanju katika nyenzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 2. Penzi kwa mtu ajabi, huhasimu wake wenzi Akakana uswahibi, mfanyanayo hayafanzi Akageuka usubi, akutobowe ja mwanzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 3. Ukimwamba ya kitabi, ligaja lenu lijenzi Hudhania wake bibi, unataka akuenzi Atapandisha ghadhabi, akupakaze masinzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 4. Huyakana matilabi, hukuletea magenzi Mwambie ziba hazibi, uso akakunja sunzi Hadi atokwe kidabi, akajuta kwa majonzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 5. Hata aweke bawabi, na mabingwa wa ulinzi Na waimbaji ayebi, nyimbo za Kongo za dansi Asemapo audhnbi, amekwamisha kitanzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 6. Wameshindwa matabibi, wa hilo hulifinyanzi Waloweza kwa hesabi, kulipia bora kanzi Walichovuna dhunubi, uhasama na simanzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 7. Ziimarishwe nasabi, kama lombe na kigunzi Kwa mshiko tabitabi, ja maua na kisonzi Penzi lendapo gudubi, hakuna mshikwa ganzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 8. Tamati ya kuratibi, penzi nyama ya mawinzi Linapoza na kusibi, lina kiza lina lenzi Kwa nguvu mtu hubebi, hufiki nalo Chamanzi Ai ni sumu ya wenzi, penzi kwa mtu ajabi. 65. Pendo la pesa 1. Pendo la pesa si pendo, mbali nalo jitengee Pendo lanuka uvundo, mbali nalo lisogee Pendo halina uhondo, katu usilichekee Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo. 2. Pendo halina utamu, lina harufu jamee Pendo ninalilaumu, mimi lisinilemee Pendo halina kudumu, hadi pesa umwekee Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo. 3. Pendo lataka kupenda, bila kupiga kengee Pendo mfano wa tunda, ukila unenepee Pendo la pesa huvyonda, tupa usilipokee Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo. 4. Pendo la kwa kila hali, ubora nalipotee Pendo kutumia mali, ndipo aitike bee Pendo hilo ni dhalili, mbali nalitokomee Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo. 5. Pendo kutumia hela, mifuko iteketee Pendo hilo lahaula, ni zigo ujibebee, Pendo wawili ni kula, nyama ndimi mnenee Pendo alina sheree, pendo la pesa si pendo. 6. Pendo kwa watu chaguo, lazima nielezee Pendo ni sawa funguo, kufuli imngojee Pendo la kupenda nguo, bora lichekwe heehee Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo. 7. Pendo ni la pale zama, wanahadithi wazee Pendo lao likiuma, bila kusema nigee Pendo sasa limelema, ukipanda lisimee Pendo halina sherce, pendo la pesa si pendo. 8. Pendo hapa nakomesha, mbele nisiendelee Pendo la pesa lafisha, ni gonjwa usipokee Pendo hadhi linafisha, la pesa sipendelee Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo. 66. Kimada 1. Bini Adamu amri, kamwe hazihifadhiki Haziwekeki dahari, na kamwe hazilindiki Kama vile za Kahari, ziloshushwa hazitoki Kimada kakosa haki, kwani si ndoa kamili. 2. Halingani na wa ndoa, kimada kakosa haki Aweza kujiondoa, kama yeye hakutaki Na mume kamchondoa, si shoti kumtaliki Kkwani amekosa haki, sio wa ndoa kamili. 3. Kwa kuwa kakosa hadhi, na ndipo hatamaniki Muwekaji huwa radhi, watu wakimdhihaki Kwa nakama na maudhi, bwana wake hashituki Kwani kalemwa na haki, kakosa ndoa kamili. 4. Sababu zake hususa, si radhi yake Maliki Kuviweka vibubusa, kwa njia ya uzandiki Jambo jema yatupasa, machafu kutoafiki Na kimada hana haki, kama wa ndoa kamili. 5. Umeoneka ukweli, mwezi juzi siyo wiki Kimada kapewa feli, mbaya hazielezeki Bwanawe akawa tuli, hakujali laizeki Kimada kakosa haki, kwani si ndoa kamili. 6. Ni maneno ya malenga, ya wapuzi siandiki Maburudi na maanga, mazima hayatenguki Bali kwa yule mjinga, atachimbia handaki Kimada kakosa haki, kwani si ndoa kamili. 7. Mfifi wa taadhima, yeye baya hatosheki Huwenda nduu kugema, anywe tumbole husaki Jaribu mwambie tema, atakukita mkuki Na kimada hana haki, kwani si ndoa kamili. 8. Na wenziwe mabwelele, manene ja pikipiki Kapa ya masiku kale, ya leo hayaoneki Hae! Najuta salale, kuwamo kindakindaki Kimada kakosa haki, kwani si ndoa kamili. 9. Ingawa kweli andiko, najuwa hatosadiki Na pindi aje kwa foko, mwendo usio burcki Asione ajabiko, kwa tungo akighariki Mpinzi aonyesha haki, kwani si ndoa kamili.
...
Kimetungwa na Amiri A. Sudi Andanenga ; utangulizi wa Jumanne M. Mayoka.
...
ISBN: 9976633696
Thank you to Benedictine Publications Ndanda
1 copy
Available for free in Arusha! Request
Donated by
Have thoughts on this book?
Add a comment to get the conversation started!
Before viewing or adding comments, you must create an account. It takes just seconds!
Related books: Browse all