Publisher Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Tanzania - Ministry of Health and Social Welfare
Ukatili wa kijinsia (UWAKI) ni tatizo la kiafya, kijamii na ni ukiukwaji wa haki za binadamu; pia ni tatizo kubwa linaloathiri afya ya jamii na husababisha madhara makubwa dhidi ya maisha ya watu hususan watoto, wanawake, wasichana na wavulana katika nchi nyingi duniani. Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimekumbwa na tatizo hili kwa miaka mingi. UWAKI unarudisha nyuma juhudi zinazofanyika kupambana na kuzuia maambukizo ya Virusi vya UKIMWI (VVU) na kuboresha afya ya uzazi na mtoto. Kwa hali hii, sekta ya afya haina budi kuchukua hatua thabiti katika kuzuia matukio ya UWAKI na kuwapa huduma za afya wanaopata madhara ya UWAKI. Mwongozo wa Taifa wa Sekta ya Afya Kuhusu Kinga na Huduma Dhidi ya UWAKI umetayarishwa ili kuwawezesha watoa huduma kujihusisha zaidi katika jitihada za kuzuia UWAKI na kuwahudumia waathirika.
...