Kitini hiki cha mafunzo ya mwalimu anayefundisha Kiswahili darasa la kwanza na pili ni kwa ajili ya kukuwezesha wewe mwalimu kufahamu ufundishaji bora ni upi, na wanafunzi wanajifunza kwa kufuata mchakato upi. Hali kadharika, kitini hiki kitamsaidia mwalimu kuandaa somo lake vizuri kwa kuzingatia mzunguko wa somo, ufundishaji na ujumuisho hususan katika kufundisha usomaji.
Soma kwa makini kitini hiki sanjari na mwongozo wa kufundisha usomaji wa mwalimu ili kupata ufafanuzi wa mawanda na mtiririko wa masomo kwa darasa husika. Baada ya mafunzo andaa ratiba ya kupitia kitini hiki na mwongozo wa kufundisha usomaji kwa makini.
...