Publisher Kikundi cha Maarifa na Ujifunzaji, Kanda ya Afrika, Benki ya Dunia
Chapisho hili ni matokeo ya ushirikiano wa kimataifa wa mtandao wa wakuzaji, watendaji na watetezi wa maarifa asilia. Wahariri wanawashukuru wale wote waliochangia kwa makala zao. Kwa zaidi ya miaka mitano, waandishi wa Tini za MA wametumia muda na juhudi zao kuchangiana uzoefu, maoni na mafunzo waliyojifunza. Wahariri wanaamini kwamba waandishi watapeleka shukrani zao kwa wale ambao ndio chanzo cha maarifa yanayojadiliwa hapa: jumuia, wakulima wanawake, waganga wa jadi, wakunga, wazee wa vijiji, wafugaji na wengine wengi. Wahariri wanatoa shukurani za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin W. Mkapa, ambaye ameandika utangulizi wa chapisho hili na ambaye ujumbe wake mkuu tumeutumia kwenye jina la kitabu hiki: Mbinu za Wenyeji za Kuleta Maendeleo ya Dunia.
...